Quantcast
Channel: MTAA KWA MTAA BLOG
Viewing all 39120 articles
Browse latest View live

CAMFED YAUNGA MKONO SERIKALI KUWAREJESHA WANAFUNZI SHULENI

$
0
0

Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania, Bi. Lydia Wilbard akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, ambapo mkutano huo umeipongeza Serikali kwa kitendo cha kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni.Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania, Bi. Lydia Wilbard akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, ambapo mkutano huo umeipongeza Serikali kwa kitendo cha kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni

Sehemu ya washiriki Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, ambapo umeipongeza Serikali kwa kitendo cha kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni.
Sehemu ya washiriki Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, ambapo umeipongeza Serikali kwa kitendo cha kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni.
Sehemu ya washiriki Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, wakiwa katika majadiliano kuangalia kusaidia utekelezaji wa waraka no mbili wa Serikali.
Programu Meneja wa Shirika la CAMFED Tanzania, Anna Sawaki (kulia) akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Ukumbi wa Msimbazi Center jijini Dar es Salaam.
Mwalimu Mshauri wa Wanafunzi Shule ya Sekondari Viwege Ilala, Bi. Ruth Saibull akizungumza na wanahabari mara baada ya mkutano huo kuchangia maoni yake kufuatia uamuzi wa Serikali.
Learnerguide wa CAMA, Bi. Mzizi Rashidi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano huo kuelezea namna watakavyoshiriki kusaidia utekelezaji wa agizo la Serikali.
Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania, Bi. Lydia Wilbard (wa pili kulia) akifurahi pamoja na wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, ambao kwa sasa wamepata shahada mbalimbali.
Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania, Bi. Lydia Wilbard akizungumza nawanahabari mara baada ya Mkutano Mkuu wa mwisho wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa kwa msaada na Shirika la CAMFED, kuelezea namna watakavyoshiriki kusaidia utekelezaji wa Waraka No. 2 wa Serikali wa kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni.

Na Joachim Mushi, Dar
SHIRIKA lisilo la kiserikali la CAMFED Tanzania limeipongeza Serikali na kuunga mkono uamuzi wa kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shuleni.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania, Bi. Lydia Wilbard kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa watoto wasichana waliosomeshwa na Shirika la CAMFED, alisema uamuzi wa Serikali ni mafanikio makubwa katika sekta ya elimu kwani umefungua fursa kwa kundi hilo la jamii kurejea shuleni na kupambania ndoto zao.

Alisema CAMFED inaamini kurejeshwa kwa wanafunzi hao shuleni kwenye mfumo rasmi ni mafanikio makubwa, kwani ni jambo ambalo lilikuwa kikwazo kikubwa hasa kwa wanafunzi wa kike ambao ndio waliokuwa waathiriwa wakubwa kwa sababuza kupata ujauzito.

"Sisi kwetu ni kitu kikubwa sana, unajua tumefanya michakato mingi, tumeshiriki katika mijadala mbalimbali kupambania hii fursa kupitia kwenye mtandao wetu wa elimu TEN/MET na pia kama CAMFED kwa kushirikiana na jamii tumejaribu kuonesha ni lini mtoto anapopata ujauzito na kuacha masomo jamii itaamini ni sababu za kutowajibika vema kwa jamii husika (watu wazima)," alieleza Bi. Lydia Wilbard katika mkutano huo.

Alisema CAMFED inaamini hatua ya Serikali inaonesha wazi kuwa changamoto zilizokatisha masomo ya wanafunzi hao zimechangiwa na jamii inayowazunguka kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo.

Aidha aliongeza kuwa uamuzi huo wa Serikali kurejesha kundi hilo la wanafunzi kwenye mfumo rasmi kumeongeza wigo kwa wanafunzi waliokubwa na vikwazo kwenye masomo kabla ya kukatizwa masomo hivyo wanapata fursa ya kuamua wenyewe kulingana na mazingira na pia ndoto zake kwamba arejee katika mfumo upi kati ya rasmi na usio rasmi kumalizia masomo yao.

Hata hivyo, amebainisha kuwa suala la Serikali kutoa tamko hilo ni moja, lakini utekelezaji wake ni eneo lingine ambapo wao kama wadau wanashiriki kuangalia ni nini cha kufanya ili kuhakikisha utekelezaji unafanikiwa na hatimaye wanafunzi hao wanarejea masomoni na kukamilisha ndoto zao kielimu.

"Mimi nafikiri sasa tujikite kwenye utekelezaji...Serikali, wanajamii, sisi wakereketwa wa elimu, wasichana wenyewe, vijana tuanze kujipanga ni namna gani tunatekeleza suala hili na lifanikiwe, tusikae madarasani kusubiri wanafunzi hao warejee wenyewe kwani hawata kuja," alisema Bi. Wilbard.

Wito wetu kama CAMFED kila mmoja wetu alichukulie suala hili kwa mtazamo chanya na kisha kushiriki katika utekelezaji wake, kila mmoja wetu afanye ni jukumu lake hivyo kuchukua hatua sehemu alipo.

"Mfano viongozi wa dini wapaze sauti kwenye nyumba za ibada kushawishi jamii kuunga mkono suala hilo kwa vitendo, wanasiasa nao walisemee suala hili kupitia majukwaa yao, viongozi wa shule nao walitangaze vizuri suala hili na pia kuangalia namna nzuri ya kudhibiti vitendo vya unyanyapaa kwa wanafunzi watakao rejea shuleni." Alisisitiza Mkurugenzi huyo wa CAMFED Tanzania.

Kwa mujibu wa tamko la Waraka namba 2 wa Mwaka 2021 Serikali hivi karibuni ililiridhia kuwarejesha shuleni wanafunzi wote waliokatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali kama vile utoro, utovu wa nidhamu na kupata ujauzito.

WAKULIMA ARUSHA WAPEWA ELIMU YA USAJILI WA VYAMA VYA UMWAGILIAJI NA UCHANGIAJI WA ADA NA TOZO

$
0
0

 


Na Mwandishi wetu – Arusha

Wakulima katika skimu za kilimo cha umwagiliaji Mkoani Arusha, wamepewa elimu kuhusiana na namna ya kusajili vyama vya umwagiliaji na utoaji wa ada na tozo na kupewa utaratibu wa kulipia ada hizo zitakazosaidia kuboresha na kurekebisha  miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji pale itakapokumbwa na madhara yatokananyo na athari za  mabadiliko ya tabianchi au uchakavu.

Bi Fatuma Mwera Afisa Kilimo kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akizungumza na baadhi ya viongozi wa skimu za kilimo cha umwagiliaji katika Halmashauri ya Arusha katika kata ya Ilikiding’a alibainisha kuwa, usajili wa vyama vya umwagiliaji utasaidia skimu kutambulika na kupata fursa zinazojitokeza ikiwa ni pamoja na kupelekewa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji.

Aidha aliwaasa viongozi hao kuwa vinara katika swala zima la usimamizi na utunzaji wa mazingira hususan vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na kutokufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo hivyo.

Aliendelea kusema kuwa, skimu zote za kilimo cha umwagiliaji zitafanyiwa maboresho kwa awamu lakini , skimu ambazo zimesajiliwa ndizo zitakazopewa kipaombele kwanza wakati wa maboresho hayo. “ Ni vizuri kusajili wote kwa pamoja ili tupange mipango ya kazi kirahisi na kuzifikia skimu kwa awamu, Alisisitiza.”

Picha ikionesha wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika kikao cha pamoja na Afisa Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya ya Arusha,hayupo pichani wakijadili kwa pamoja maswala ya tozo za Umwagiliaji.

Bi. Fatuma Mwera,Afisa Kilimo toka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akiongea na viongozi wa skimu za umwagiliaji katika wilaya ya Arusha kuhusiana na maswala ya Tozo na Ada za umwagiliaji.

Kulia Kaimu Mkurugenzi wa Mipango toka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Reginald Diyamet na Mhandisi Naomi Mcharo, wakijadili jambo linalohusu Kilimo cha Umwagiliaji kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020.
 

 

SHULE YA BILIONEA LAIZER NA O'BRIEN ZAANZISHA USHIRIKIANO

$
0
0


Na Mwandishi wetu, Simanjiro
SHULE ya msingi ya Bilionea Saniniu Laizer ya Kata ya Naisinyai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara na O'Brien ya Kia Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro zimeanzisha ushirikiano rasmi kwa ajili ya maendeleo ya wanafunzi wa maeneo yao.

Mchimbaji maarufu wa madini ya Tanzanite, Bilionea Saniniu Laizer ambaye alijenga shule hiyo ya mtaala wa kiingereza na kuikabidhi Serikali amesema ushirikiano huo utanufaisha shule hizo.

Bilionea Laizer amewashukuru viongozi wa shule ya O'Brien kwa kuwapa mhandisi wa kusimamia ujenzi wa bwalo kwa ajili ya kula chakula wanafunzi wa shule hiyo.

"Tunashukuru pia kwa kuwapatia wanafunzi wetu mipira wamefurahi mno na ahadi ya kuwafungia bembea ili wakati wa mapumziko ya masomo wajiburudishe," amesema bilionea Laizer.

Amesema ushirikiano mpya wa shule hizo mbili utasababisha maendeleo makubwa kwa jamii za maeneo hayo kwani hivi sasa mwamko wa elimu umekuwa mkubwa kwao.

"Tupo tayari kwa ushirikiano mpya wa shule hizi mbili kwani lengo letu ni kujifunza na kuhakikisha tunafika mbali zaidi kwenye elimu," amesema bilionea Laizer.

Pia, ameishukuru serikali kwa kuipatia shule hiyo walimu watano japokuwa wanasubiri kupatiwa walimu wengine watano ili wafundishe wanafunzi wao.

Mwalimu mkuu wa shule ya O'Brien, Nimla Mbangu amesema ushirikiano wa shule yao na shule ya Saniniu Laizer, utazidi kufanikisha maendeleo ya pande zote.

Mwalimu Mbangu amempongeza bilionea Laizer kwa namna anavyojitoa kuzisaidia shule zote mbili kwa manufaa ya wanafunzi wa jamii wa maeneo hayo.

"Endelea kuwa na moyo huo huo wa kusaidia jamii ya maeneo haya kwani Mungu amekujalia uwezo mkubwa wa kiuchumi na umesambaza upendo kwa kutumia na jamii inayokuzunguka," amesema.

BAADHI YA WAISLAMU WAMEASWA KUACHA KULALAMIKA

$
0
0
NA BALTAZAR MASHAKA, Mwanza
BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Mwanza ,limewataka waumini wa dini ya Kiislamu kuacha kulalamika na kuilaumu serikali, wafanye shughuli za maendeleo,wasisumbuliwe na vyeo (madaraka).

Pia limewataka kusomesha watoto wao na kufanya mambo ya maendeleo badala ya kusubiri hisani ya serikali kwa kuwa yanayofanywa na BAKWATA, madhehebu mengine yametangulia,hivyo wakipuuza watabaki nyuma. 

Rai hiyo ilitolewa jana na Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza Alhaji Sheikhe Hasani Kabeke, alipozungumza na waumini wa Msikiti wa Jihad Nyabusalu, Kiseke katika Wilaya ya Ilemela,kwenye Sherehe ya Maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W.

Alisema Waislamu wanapaswa kujitambua kwa kuchangia na kufanya maendeleo kwa maslahi yao badala ya kulalamika na kuilaumu serikali.

“Hatuwezi kuwa watu wa kulalamika tu,tufanye maendeleo ya waislamu, haiwezekani serikali ichukue sh. milioni 4 itupe tu, za nini? Tuseme ukweli, serikali itatuunga mkono kama kuna jambo la maendeleo,hivyo tufute mambo ya kulalamika,”alisema Sheikhe Kabeke.

Alitahadharisha Mwanza kuna tatizo kubwa la ushirikiano kwenye elimu bado hawajaitumika vizuri na kusistiza ujenzi wa vituo vya afya unaoendelea,waendeleze mshikamano na kusameheana kwani hakuna mkamilifu,”alishauri.

Naye Sheikhe wa Wilaya ya Tabora, Sheikhe Ramadhan Rashid, alimmwagia sifa Sheikhe Kabeke kwa anayoyafanya ni makubwa ili kuchochea maendeleo, hafanyi ili kulinda nafasi yake bali maslahi ya waislamu na kwa jinsi hiyo Mwanza itabadilika na itaendelea kwa sababu hafanyi maigizo kuhamasisha maendeleo.

Mgeni rasmi kwenye maulidi hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Massala, alisema lipo jambo la kujifunza kwa Sheikhe Kabeke,amekuwa mwanaharakati wa maendeleo na dini hata serikali inapokwama amekuwa kinara wa kuikwamua kwenye changamoto zinazoikabili likiwemo suala la chanjo ya Uviko-19.

Alisema jamii kupitia kwa kiongozi huyo wa kiroho ilihamasika kuchanja baada ya upotoshaji uliofanywa na watu wasioitakia mema nchi yetu na kuwaomba viongozi wengine wa dini na kisiasa kuendelea kuhamasisha chanjo ya kujikinga na ugonjwa huo na kuwataka waislamu waitumie tunu hiyo, wasiyaone mapungufu bali mazuri yake kwa maslahi mapana ya uislamu.

“Sheikhe Kabeke umefanya kazi kubwa ya kuhamasisha ujenzi wa vituo vya afya,unahisi unawajengea waislamu tu bali Watanzania wote na serikali hatutakuacha pekee yako, tutakuunga mkono kutafuta matofali ya ujenzi huo,binafsi nitakuunga mkono kwenye jambo hili la heri, pia ” alisema Massala.
Aliongeza kuwa “waislamu tusione shida kwenye suala la maendeleo,waliofanikiwa walijitoa kwa fedha na nguvu zao (kusomba maji ama kufyatua matofali), tusilalamike,tunapoteza muda mwingi na hakuna mtu anatuonea kwani zipo shule nyingi za dini na haya yanayofanyika yawe chachu ili mwisho tusikwame kwenye maendeleo.”

Aidha alisema ujenzi wa vituo vya afya vya waislamu unaunga mkono jitihada za serikali ambapo imetoa sh. milioni 250 za tozo kujenga kituo kama hicho Kayenze, hivyo wamwombee Rais Samia Suluhu Hassan afya njema kwani anayoyafanya yanagusa maisha ya Watanzania.
Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Sheikhe Hasani Kabeke, akizungumza jana na waumini wa dini ya Kiislamu wakati wa maulidi na harambee ya kuchangia ununuzi wa kiwanja cha upanuzi wa Msikiti wa Jihad, Nyabusalu, Kiseke wilayani Ilemela.
Sheikhe Mohamed Mbega , kutoka kushoto wa tatu akizungumza jana kwenye eneo la ujenzi wa kituo cha afya Kiseke,wilayani Ilemela, kinachojengwa kwa nguvu na michango ya Waislamu.Wa nne kutoka kushoto ni Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza,Alhaji Sheikhe Hasani Kabeke.

MERIDIAN GAMING GROUP KUSHIRIKI MAONESHO YA BRAZIL iGAMING SUMMIT

$
0
0

*Bidhaa Mpya Kemkem Kuzinduliwa Disemba Hii Kule Sao Paolo.

WAKALI wa michezo ya kubashiri duniani wapo tayari kwa maonesho nchini Brazili, kutakuwa na ofa mpya za kubashiri sambamba na habari motomoto za jakipoti ya kasino.

Meridian Gaming Group ambao ni kampuni kubwa ya michezo ya kubashiri duniani na waasisi wa soko la America Kusini, watashiri kwenye maonesho ya Brazil iGaming Summit (BiS) 2021, maonesho makubwa zaidi kufanyika Sao Paolo, Disemba 1-2.


Ukizungumzia michezo ya kubashiri, Meridian Gaming inavitu vingi vipya kwenye soko la Brazili na Amerika Kusini, kubwa zaidi ni Tiketi ya Malipo kwenye akaunti za mtandaoni na sifa ya nafasi tatu. Kampuni hii ni miongoni mwa kampuni za mwanzo kuanza kufanya kazi kisheria kwenye ukanda huu na, ubobezi wake utachangia sana kwenye majadiliano ya kiuchumi na namna bora ya usimamizi kwenye hili soko.

 

Kutakua na safu tofauti za kasino, sloti ya Meridian Casinoitaonekana kule Sao Paolo. Tayari ni kampuni inayojulikana zaidi duniani kutokana na upekee wa michezo yake na bonasi za aina mbili.

Kwa miezi mingi sasa, Meridian imekuwa ikilipa mamilioni ya ushindi na jakipoti za kasino lakini, ushindi mmoja uliweka rekodi kwenye michezo ya sloti duniani na, pengine itaendelea kubaki kwenye rekodi.

 

Kwa siku za hivi karibuni, Meridian imelipa jakipoti ya €1,129,692.15 kwenye mchezo wa sloti ya Wild Crusade: Empire Treasures. Haya ni malipo makubwa kwenye soko la Ulaya kwa siku za hivi karibuni.


Mtandao makini michezo na teknolojia ya kubashiri wa B2C na B2B, upo tayari kwa maonesho ya Brazili. Kwa taarifa zaidi na kupata tiketi yako, tuwasiliane kupitia https://meridian.bet/contact.html na info@meridianbet.com 

NSSF YATUNIKIWA TUZO KUTHAMINI MCHANGO WAKE KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ekwabi Mujungu (kushoto), ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, akipokea tuzo na cheti kutoka kwa Mgeni Rasmi, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, kwa ajili ya kuthamini mchango wa NSSF katika mapambano dhidi ya UKIMWI. Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya. Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS Dkt. Leonard Maboko.

Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu  na Utawala (NSSF), Ekwabi Mujungu (wa tatu kulia) ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa NSSF baada ya kupokea tuzo na cheti kwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuthamini mchango katika katika mapambano dhidi ya UKIMWI.  Wa tatu kushoto ni Meneja wa  NSSF  Mkoa wa Mbeya, Deus Jandwa.
Tuzo na cheti kutoka TACAIDS cha  kuthamini mchango wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika mapambano dhidi ya UKIMWI
HUDUMA: Wananchi walipokuwa wanahudumiwa kwenye banda la NSSF wakati wa maonesho  ya Maadhimisho  ya siku ya UKIMWI Duniani yenye kauli mbiu 'Zingatia usawa. Tokomeza UKIMWI. Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko ' , yanayofanyika kitaifa Mkoani Mbeya, ambapo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) unashiriki kutekeleza Sera  ya  Utumishi wa Umma kuhamasisha elimu juu ya VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukizwa mahala pa kazi
Katibu Mahsusi ambaye pia Mwelimishaji rika wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF) Mkoa wa Mbeya,  Happy Gwimile (wa kwanza Kulia) akiwakumbusha  baadhi ya wananchi waliotembelea banda  la NSSF kuhusu kuendelea kujikinga na maambukizi VVU na UKIMWI hasa mahali pa kazi ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.
Afisa Mkuu Utawala Daniel Shaidi (kushoto) wa NSSF Makao  Makuu ambaye pia ni Mwelimishaji  rika mahala pa kazi, alipokuwa anamuelekeza Fatma Fungo (kulia), namna ya kutumia mifumo mbalimbali inayomwezesha  mwanachama kuangalia taarifa zake kupitia simu ya kiganjani bila kulazimika kufika katika Ofisi za NSSF. Mifumo hii ni pamoja na NSSF Taarifa , Whatsapp na ujumbe mfupi wa maneno yaani SMS. Mifumo hii ya kidigitali inamrahisishia mwanachama kupata huduma kwa haraka  kwa kujihudumia mwenyewe, inampunguzia  gharama za usafiri. Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duaniani Kitaifa yanafanyika katika Mkoa wa Mbeya.
Katibu Mahsusi ambaye pia Mwelimishaji rika wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF), Ng’walu Mihambo kutoka NSSF Tarime, akitoa maelezo kwa wananchi juu ya mbinu za kuzuia magonjwa ya VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukiza ikiwa ni pamoja na ulaji unaofaa, mazoezi ya mwili, kuwa na uzito usiozidi kiasi kulingana urefu, kuepuka matumizi ya pombe na sigara, VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyo ambukizwa
Afisa Mwandamizi Utawala, Naphisa Jahazi ambaye pia  ni Mwelimishaji  rika mahala pa kazi kutoka  NSSF, Mkoa wa Temeke akielezea kwa baadhi ya wananchi namna NSSF ilivyojielekeza katika kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukizwa mahala pa kazi, wakati wa  Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duaniani Kitaifa yanafanyika katika Mkoa wa Mbeya
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya  Jamii  (NSSF), haujawaacha nyuma makundi yenye mahitaji maalum, Mkalimani wa Lugha ya alama Baraka Bakari (wa kwanza kulia) akiwatafsiria  walemavu wa usikivu  elimu kuhusu hifadhi ya jamii, walipotembelea banda la NSSF wakati wa  Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo  Kitaifa yamefanyika Mbeya

NSSF YATUNIKIWA TUZO KUTHAMINI MCHANGO WAKE KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI 

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepewa tuzo kama ishara ya kuthamini mchango wake katika mapambano ya VVU na UKIMWI. 

Tuzo hiyo ilitolewa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na kukabidhiwa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa maadhimisho ya siku ya UKiMWI duniani yaliyofanyika jijini Mbeya.

NSSF imekuwa ikitekeleza Sera ya UKIMWI mahala pa kazi na imekuwa ikisimamia miongozo yote inayohusu VVU na UKIMWI

Pia, Mfuko ulishiriki katika maonesho na maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ili kuendelea kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Taifa kuendelea kujikinga na masuala ya VVU na UKIMWI.

Mkurugenzi Mkuu Bw. Masha J. Mshomba katika salamu zake kwa wafanyakazi wa Mfuko katika siku ya UKIMWI duniani alisema  “Nasisitiza kuwa, ni wajibu wa kila mfanyakazi kuchukua hatua katika kudhibiti VVU na UKIMWI ili kuokoa nguvu kazi ya Mfuko na Taifa”. 

Aidha, Mshomba alifafanua zaidi na kusema kwamba NSSF inayo sera inayohusu masuala ya VVU na UKIMWI ambayo inasisitiza kujilinda, kujikinga, kumlinda mfanyakazi aliyeathirika, kuzuia unyanyapaa na kumsaidia mfanyakazi aliyeathirika.
Kauli Mbiu ya mwaka huu ilikuwa “Zingatia Usawa, Tokomeza Ukimwi, Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko”. 







WAWEKEZAJI ZAIDI YA 140 KUTOKA ITALIA WAWEKEZA TANZANIA

$
0
0
Naibu Waziri, Wizara ya Madini Prof. Shukrani Manya akihutubia Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika leo Jijini Roma
Naibu Waziri, Wizara ya Madini Prof. Shukrani Manya akihutubia wafanyabiashara na wawekezaji walioshiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika leo Jijini Roma.
Balozi wa Tanzania Nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo akiongea na wafanyabiashara waliojitokeza kushiriki Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika leo Jijini Roma.
Balozi wa Tanzania Nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo akiongea na wafanyabiashara waliojitokeza kushiriki Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika leo Jijini Roma.
Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Edwin Rutageruka akitoa hotuba yake kwa wafanyabiashara (hawapo pichani) walioshiriki Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.
Mwenyekiti wa Chama Wawekezaji katika Sekta ya Hoteli Zanzibar, Bw. Paulo Rosso akiongea na Wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.
Mmoja wa Wafanyabiashara kutoka Italia akiongea na Wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Bw. Abdulmajid Nsekela akitoa hotuba yake kwa wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma
Sehemu ya Wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma

………………………………………………………

Na Mwandishi wetu, Roma

Wawekezaji zaidi ya 140 kutoka Italia wamewekeza katika miradi mbalimbali nchini Tanzania

Takwimu hizo zimetolewa na Naibu Waziri Wizara ya Madini, Prof. Shukrani Manya alipokuwa akifungua jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika leo Jijini Roma, Italia.

Prof. Manya amasema kuwa miradi hiyo inathamani ya Shilingi bilioni 5 inayotoa ajira kwa watanzania zaidi ya 4000.

“Jukwa hili tunataka liendelee kuwa sababu ya kuchagiza uwekezaji mwingine kutoka Italia kwa kutumia teknolojia waliyonayo, kwa kutumia utalaamu walionao wa ‘designing’…….na sasa waone kuwa Tanzania ni sehemu salama ya kuwekeza na Tanzania inaendelea kuweka mazingia wezeshe ya kukuza sekta ya uwekezaji na biashara,” Amesema Prof. Manya

Ameongeza kuwa kupitia jukwaa la biashara na uwekezaji biashara na uwekezaji utaendelea kuongezeka na kuongeza zaidi na hasa katika maeneo ambayo tumawaeleza hapa kupitia jukwaa hili.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania Nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo amesema kuwa kufanyika kwa kongamano hili la biashara na uwekezaji lengo lake kubwa ni kuwavutia wafanyabiashara na wewekezaji wa sekta mbalimbali kutoka Italia kuwekeza zaidi Tanzania.

“mwitukio ni mkubwa na tumeitikiwa na jumuiya za kibiashara na wafanyabiashara na wawekezaji zaidi ya 250 kutoka nchi zote mbili wameshiriki katika kongamano hili,” amesema Balozi Kombo

Balozi Kombo ameongeza kuwa, Wafanyabiashara kutoka italia ni wabobezi katika sekta ya madini lakini pia katika utalii hivyo ni matumanini yake kuwa mara baada ya kumalizika kwa kongamano hilo wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Italia wataongezeka zaidi Tanzania.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Wawekezaji katika Hoteli Zanzibar, Bw. Paulo Rosso amewasihi wawekezaji kutoka Italia kuwekeza kwa wingi Tanzania kwa kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji ni tulivu na salama.

“Tanzania ni sehemu salama kuwekeza…..nawahakikishia mimi nimewekeza Tanzania na ninaona ni sehemu salama ya kuwekeza karibuni sana kuwekeza kwa maendeleo ya Tanzania na Italia,” amesema Bw. Rosso

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela amewahakikishia wafanyabiashara na wawekezaji walioshiriki katika jukwaa hilo kuwa CRDB ipo tayari kutoa mikopo kwa watakao kuwa tayari kuwekeza Tanzania.

“Nawahakikishia kuwa Benki ya CRDB itawawezesha mikopo ya kuwekeza katika sekta mbalimbali hivyo msiwe na wasiwasi kuhusu mitaji ya kuwekeza ipo karibuni sana tuijenge Tanzania,” Amesema Bw. Nsekela.

Jukwa hilo la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia limehudhuriwa na Wafanyabiashara na Wawekezaji takribani 250 kutoka nchi zote mbili. Wafanyabiashara na wawekezaji hao ni wa sekta za utalii, kilimo, madini, na ujenzi.

Pamoja na mambo mengine, jukwaa hilo limewawezesha wafanyabiashara na wawekezaji kujadili fursa, uwezekano wa ubia, changamoto zinazokabili mazingira ya biashara na njia ya kuboresha mahusiano ya kibiashara kati ya nchi hizo mbili.

Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia limeandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Italia kwa kushirikiana na Kituo cha Taifa cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Taifa ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA).

KICHANGA CHAOKOLEWA KWENYE SHIMO LA CHOO KIKIWA HAI KAGERA

$
0
0

Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji S/Sgt Karata Ramadhani Karata akimpatia huduma ya kwanza mtoto mchanga aliyemuokoa kutoka katika shimo la choo alikokuwa ametupwa huko Mkoani Kagera, Wilaya ya Karagwe Kata ya Bugene tarehe 01 Desemba, 2021.
 
 ======  =====  =====

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera limefanikiwa kumuokoa mtoto mchanga aliyekuwa ametupwa chooni jana tarehe 01 Desemba, 2021 huko wilayani Karagwe kata ya Bugene katika Mtaa wa Lukajage. 
 
Mtoto huyo wa Kiume anayesadikiwa kuwa na umri wa Siku Mbili alitupwa katika choo hicho na mtu ambaye hakufahamika mara moja na sasa yupo katika Hospitali ya Kayanga Wilayani Karagwe akiendelea na matibabu. 
 
Jeshi la Polisi Mkoani Geita linaendelea na uchunguzi ili kumbaini mama wa mtoto huyo. Kaimu Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji (M) Kagera Mkaguzi Thomas Majuto amesema, walipata taarifa kwa njia ya simu na kuwahi kufika eneo la tukio kisha kufanikiwa kumuokoa Mtoto huyo.

Benki ya CRDB yaahidi Mitaji na Mikopo kwa wafanyabiashara, wawekezaji kutoka Italia

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Bw. Abdulmajid Nsekela akitoa hotuba yake kwa wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.
Sehemu ya Wafanyabiashara na Wawekezaji walishiriki katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Chama Wawekezaji katika Sekta ya Hoteli Zanzibar, Paulo Rosso walipokutana katika Jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia lililofanyika Jijini Roma.
Benki ya CRDB imewahakikishia wafanyabiashara na wewekezaji wa Tanzania na Italia utayari wake wa kutoa mikopo na mitaji ya kutosha watakapo kuwa tayari kuwekeza nchini Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati wa jukwaa la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Itali liloandaliwa na ubalozi wa Tanzania lililofanyika Jijini Roma, nchini Italia.

Nsekela amesema Benki ya CRDB ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Sita pamoja na wawekezaji katika kuhakikisha kuwa changamoto zinazoendana na huduma za kibenki zinatatuliwa.

“Nawahakikishia kuwa Benki ya CRDB itawawezesha mikopo ya kuwekeza katika sekta mbalimbali hivyo msiwe na wasiwasi kuhusu mitaji ya kuwekeza ipo karibuni sana tuijenge Tanzania,” amesema Nsekela.

Nsekela ameongezea kuwa Benki ya CRDB inafarijika kuona wawekezaji wengi wameonesha nia ya kuwekeza zaidi Tanzania, huku akimpongeza Balozi wa Tanzania nchini Itali, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo kwa kuandaa Jukwaa hilo ambalo limetoa fursa ya kueleza sekta mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana Tanzania.

“Benki ya CRDB pamoja na mambo mengine tutahakikisha kuwa sisi kama benki tunawawezesha wawekezaji wanaowekeza nchini na kuwapa mitaji ya biashara pamoja na biashara za kimataifa kati ya nchi moja na nyingine…,” alisisitiza.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo ameipongeza Benki ya CRDB kwa utayari wake wa kusaidiana Serikali kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini kupitia utoaji wa mikopo na mitaji, pamoja na huduma nyengine za kifedha zinazoongeza ufanisi katika uendeshaji wa biashira.

“Benki ya CRDB imeonyesha uzalendo mkubwa kwa kushirikiana na Serikali kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza nchini, binafsi sina shaka na uwezo wao kimtaji. Nimefurahi pia wamekwenda mbele zaidi kwa kutoa huduma za ushauri katika uwekezaji, hii inaonyesha ni jinsi gani wamejipanga vizuri,” amesema Balozi Kombo.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Wawekezaji katika Hoteli Zanzibar, Bw. Paulo Rosso amewasihi wawekezaji kutoka Italia kuwekeza kwa wingi Tanzania kwa kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji ni tulivu na salama.

“Tanzania ni sehemu salama kuwekeza….nawahakikishia mimi nimewekeza Tanzania na ninaona ni sehemu salama ya kuwekeza karibuni sana kuwekeza kwa maendeleo ya Tanzania na Italia,” amesema Bw. Rosso

Jukwa hilo la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia limehudhuriwa na Wafanyabiashara na Wawekezaji takribani 250 kutoka nchi zote mbili. Wafanyabiashara na wawekezaji hao ni wa sekta za utalii, kilimo, madini, na ujenzi.

Pamoja na mambo mengine, jukwaa hilo limewawezesha wafanyabiashara na wawekezaji kujadili fursa, uwezekano wa ubia, changamoto zinazokabili mazingira ya biashara na njia ya kuboresha mahusiano ya kibiashara kati ya nchi hizo mbili.

ELIMU KWA WATOTO WENYE ULEMAVU MKOANI SINGIDA BADO NI CHANGAMOTO

$
0
0
Wanafunzi hawa wameweza kufikia hatua hii kutokana na juhudi za Mwalimu mwenye Elimu Maalum.

Wanafunzi hawa wa Shule ya Msingi Kizega wilayani Iramba mkoani hapa wakiwa darasani wakifurahia matunda ya uwepo wa Walimu wenye Elimu Maalum.
Ufundishaji wa aina hii hufanywa kwa ufanisi zaidi na Walimu wa Elimu Maalum na si vinginevyo.

Na Abby Nkungu, Singida
SUALA la kupata elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum bado ni changamoto kubwa kutokana na uhaba wa walimu wenye taaluma ya lugha ya alama na ukosefu wa miundombinu rafiki ya kujifunzia na kufundishia katika shule za msingi zinazotoa elimu jumuishi mkoani Singida.

Hayo yamebainika katika kipindi hiki cha Siku ya Kimataifa ya Watu wenye ulemavu inayoadhimishwa Desemba 03, kila mwaka ili kukuza uelewa kwa jamii juu ya kundi hilo na kuhamasisha misaada ya kiutu, Haki na Ustawi kwa watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali.

Hata hivyo, wakati dunia ikiadhimisha siku hii, katika shule ya msingi mchanganyiko Mgori mkoani Singida, wanafunzi wenye mahitaji maalum wanasema wanakabiliwa na changamoto kubwa kupata elimu.

Mmoja wa wanafunzi hao, Amiri Mohamed alisema kuwa shuleni hapo hakuna vifaa muhimu vya kujifunzia kwa wenye ulemavu kama vile Mashine au vitabu vya maandishi ya nukta nundu, hali inayosababisha wasioona kutegemea hisani ya wenzao wanaoona kuwasomea maandishi ya kawaida ubaoni ili waweze kuandika kwenye vibao vyao.

“Mtihani unaletwa kwa maandishi ya kawaida kwa wote, wenye mahitaji maalum na wanaoona. Sasa sisi mpaka mwenzio anayeona akusomee ndipo uweze kuandika. Isitoshe, hapo hakuna mwalimu wa lugha ya alama ambaye anaweza kukusaidia” alisema Amiri.

"Hakuna bweni hapa. Tunakolala ni chumba ambacho awali lilikuwa darasa kabla ya kukarabatiwa kuwa Ofisi ya walimu na sasa ndilo 'bweni' letu" alisema Obed Williard, mwanafunzi mwingine.

“Mimi angalau nina uoni hafifu lakini wapo wenzangu ambao hawaoni kabisa. Tunaishi kwenye hili 'bweni' ambalo vyoo vyake ni vya nje. Fikiria changamoto zinazowakumba wasioona.....Wanaweza kuumwa na wadudu wenye sumu, nyoka au hata kudhuriwa na watu wabaya"

Mwalimu wa Kitengo cha elimu maalum katika shule hiyo, Hemed Kilango anakiri kukabiliwa na changamoto kubwa katika kuwafundisha watoto hao kwani hakuna vifaa muhimu na bajeti yao ni ndogo kiasi kwamba haiwezi kununua hata kofia, miwani ya jua au mafuta ya ngozi kwa wanafunzi wenye ualbino.

Ofisa elimu Maalum katika Halmashauri hiyo, Huruma Funda alisema kuwa wanahitaji jumla ya walimu 20 wa elimu maalum lakini waliopo ni sita tu, wawili kati yao wakiwa ni wa lugha ya alama.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida, Elia Digha anasema halmashauri yake ilikwisha kuomba walimu wa elimu maalum kutoka Serikali Kuu lakini walijibiwa kuwa idadi ya walimu wa aina hiyo ni ndogo; hivyo wasubiri hadi hapo watakapopatikana, ndipo watapatiwa.

Hivi sasa Serikali inatekeleza Sera ya elimu Jumuishi inayotaka wanafunzi wenye mahitaji maalum na wenye ulemavu wa aina mbalimbali kusoma na wenzao katika shule moja bila kubaguliwa.

SIMBA YAIFUATA RED ARROWS KWA TAHADHARI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Michuzi TV
KIKOSI cha Simba kimeondoka leo kuelekea nchini Zambia kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa mtoano wa Kombe la Shirikisho la Afrika dhidi ya Red Arrows utakaochezwa Jumapili Desemba 05.

Kocha Mkuu wa Simba Pablo Franco amesema wamejipanga vizuri kwa mchezo wa marudiano japo wanafahamu utakuwa ni mgumu kwao.

Pablo amesema anajua Red Arrows wanataka kupata matokeo katika Uwanja wao wa nyumbani, ila Simba wanamtaji wa mabao hivyo wamejipanga kuhakikisha wanalinda ushindi.

Kauli hiyo ameitoa leo wakati akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere pamoja na kikosi wakiwa tayari kuelekea Zambia kwa ajili ya mchezo huo.

"Tunajua mchezo utakuwa mgumu Red Arrows watataka kushinda lakini tumejipanga kupambana nao, kikubwa tunahitaji kulinda ushindi wetu tuliopata katika mchezo uliopita"amesema.

" Wachezaji wote wako kwenye hali nzuri na morali ipo juu na tunafahamu kitu gani tunatakiwa kufanya kuelekea mchezo wa jumapili ili kuwapa furaha mashabiki wetu"amesema

Katika mchezo wa awali uliopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Simba walipata ushindi wa goli 3-0 na Red Arrows wanatakiwa kushinda goli 4-0 au na zaidi ili kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Simba walitolewa katika mchezo wa raundi ya kwanza ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy na kupangiwa kucheza mchezo wa Play Off dhidi ya Red Arrows.

Kamati ya siasa (CCM) yakagua miradi inayojengwa kwa mamilioni ya fedha za Uviko

$
0
0

 

Wajumbe wa kamati ya siasa wakikagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa manne katika shule ya sekondari ya wasichana ya Manyunyu iliyoko Matembwe shule hiyo imetengewa shilingi milioni 80.Na Amiri Kilagalila,Njombe

KAMATI ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Njombe imekagua madarasa 13 kati ya madarasa 28 yanayogalimu shilingi milioni 560 yanayojengwa kwa msaada wa fedha za maendeleo UVIKO,mwenyekiti wa Chama hicho wilaya Mzee Edward Mgaya kwa niaba ya kamati amesema wameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Bi,Sharifa Nabalang’anya akishiriki katika kazi pamoja na wananchi wa Mtwango wanaoendelea na ujezni wa madarasa ya shule ya sekondari Sovi.
G:Kamati ya siasa ya ikipokea taarifa ya ujenzi wa maadara matatu katika shule ya sekondari Kidegembye yaliyotengewa shilingi milioni 60 ujezni upo kwenye hatua ya upigaji wa Plasta.
Kamati ya siasa ikikagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa mawili yanayojengwa kwa fedha za Uviko katika shule ya sekondari J.M Makweta iliyopo kata ya Kichiwa yaliyotengewa milioni 40.Madarasa yapo katika hatua ya upigaji wa Plasta.

NI DESEMBA 26, KIDUNDA DHIDI YA KATOMPA UBINGWA WA WBF

$
0
0

 

Na Zainab Nyamka, Michuzi TV
BONDIA Selemani Kidunda ameahidi kuibika na ushindi dhidi ya Bondia Eric Tshimanga Katompa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika pambano la Ubingwa wa dunia wa Mkanda wa WBF litakalofanyika Desemba 26 mwaka huu.

Katika pambano hilo la kulipa kisasi, linatarajiwa kuwa na mapambano 10 ya utangulizi ambapo sita yatakuwa ya kimataifa na manne ya ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Kidunda amesema anataka kuonesha ulimwengu na watanzania kuwa hakuna bondia anayeweza kuja kushinda ndani ya ardhi ya Tanzania.

Kidunda amesema, anataka kuwaonesha ladha watanzania na ushindi upo kikubwa ni sapoti kutoka kwa watanzania wote katika pambano hilo muhimu.

“Nimejiandaa vizuri, ushindi upo na kikubwa ni kusubiri siku ya pambano ifike na hatatoka na ushindi wowote,”

“Nia ya ushindi ipo na na nitampiga Kamtopa kwa namna yoyote, kwa staili yoyote hatatoka kikubwa ni sapoti kutoka kwa watanzania,” amesema

Kwa upande wa muandaaji wa pambano hilo kutoka Peaktime Media, Kapteni Selemani Semunyu amesema amesema pambano kati ya Kidunda na Katompa ni la ubingwa wa WBF, uzito wa Kg 76 na litakuwa la raundi 10.

Amesema, pambano hilo litakuwa la kulipa kisasi baada ya Katompa kumchapa Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ na kuondoka na Ubingwa.

Semunyu amesema, kabla ya pambano hilo kutakuwa na mapambano 10 ya utangulizi na sita yatakuwa ya kimataifa na litafanyika kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza.

“Nawashukuru sana wadhamini wote pia mnadhimu Mkuu wa Jeshi kwa kulisimamia pambano hili kuanzia mwanzo hadi mwisho na kusema ukweli bila yeye pambano hili lilikua na hatihatu ya kufanyika,”

“Ameahidi pia kama namba moja atashindwa kufika siku hiyo basi yeye anaweza kumuwakilisha na kuwa mgeni rasmi siku hiyo,” amesema

Mabondia wengine watakaopambana siku hiyo ni Ismai Galiatano dhidi ya Denis Mwale, Ibrahim Class vs Israel Kamwamba, George Bonalacha vs Hassan Milanzi, Pali Magesta vs Oscar Richard na Viguli Shafii vs Ally Kilongola.

Wengine ni Hamis Kibodi vs Iddy Jumanne, Grace Mwakamela vs Ruth Chisale, Najma Isike vs Leila Zayidu na Daniel Materu vs Haruna Swanga

Rais Samia azindua Kiwanda cha Raddy Fiber Manufacturing Ltd , Mkuranga Pwani

$
0
0

 





Katika Kuelekea Miaka 60 ya Uhuru- Mhe. Rais Samia azindua Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Tanzania Ltd- Pia azungumza na wananchi wa Mbagala (DSM) na Vikindu mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Tanzania Limited kilichopo Mkuranga mkoani Pwani leo tarehe 03 Desemba, 2021. Wengine katika picha kutoka kulia wa kwanza ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Uwekezaji Geoffrey Mwambe pamoja na Mtendaji Mkuu wa Kiwanda hicho Ramadhani Hassani Mlanzi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya kuzindua Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Tanzania Limited kilichopo Mkuranga mkoani Pwani leo tarehe 03 Desemba, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua kazi mbalimbali katika Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Tanzania Limited kilichopo Mkuranga mkoani Pwani leo tarehe 03 Desemba, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Tanzania Limited wakati akipita kukagua hatua mbalimbali za utengenezaji wa nyaya hizo za Mawasiliano Fiber katika kiwanda hicho kilichopo Mkuranga mkoani Pwani leo tarehe 03 Desemba, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasikiliza wataalamu mbalimbali wa Kiwanda hicho cha Nyaya za Mawasiliano katika sehemu ya maabara ya kupima uwezo wa nyaya hizo kabla ya kuziingiza sokoni.



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 03 Desemba, 2021 amezindua Kiwanda cha kutengeneza Nyaya za Mawasiliano cha Raddy Fiber Manufacturing Ltd kilichopo katika Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.


Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho, Mhe. Rais Samia amesema hafla hiyo ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara ambapo ameanza kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika baadhi ya miradi mbalimbali ya maendeleo.


Mhe. Rais Samia amesema uzinduzi wa kiwanda hicho unathibitisha uwezo na fursa nyingi ambazo nchi imejaliwa kuwa nazo na ziweze kutumika ili kukuza uchumi wa nchi, kuleta ajira kwa wananchi hususan vijana na kuzalisha bidhaa ambazo sio lazima kuagizwa kutoka nje.


Aidha, Mhe. Rais Samia amemshukuru na kumpongeza mwekezaji wa kiwanda hicho Bw. Ramadhani Hassani Mlanzi ambaye ni mzawa kwa kuona kuwa Tanzania ni sehemu salama ya kuwekeza na kumhakikishia kuwa Serikali itampa ushirikiano wa kutosha.


Mhe. Rais Samia amewakaribisha wawekezaji wengine kutoka ndani na nje ya nchi kuwekeza Tanzania na kuwahakikishia usalama wa mitaji yao pamoja na uhakika wa kutengeneza faida.


Pia, Mhe. Rais Samia amesema Serikali inatambua mchango wa sekta binafsi nchini katika kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi hivyo inaendelea kuweka mazingira wezeshi na rafiki ya ufanyaji biashara na uwekezaji.


Mhe. Rais Samia ameagiza taasisi zote za Serikali zinazotoa huduma katika sekta ya Uwekezaji kuondoa urasimu ambao umesababisha kupoteza baadhi ya wawekezaji waliokuwa wanataka kuwekeza nchini kwa kuwa wawekezaji wana mchango mkubwa katika kujenga uchumi wa nchi yetu.


Vilevile, Mhe. Rais Samia amesema Serikali itaimarisha jitihada za mageuzi ya kisera na kisheria ikiwemo utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Udhibiti wa Biashara nchini ujulikanao kama The Blueprint for Regulatory Reforms to Improve Business Enviroment.


Mhe. Rais Samia amesema Serikali ina lengo la kuhakikisha kuwa wananchi wote wanafikiwa na huduma za mawasiliano ili kuwawezesha kutumia huduma zitonakazo na TEHAMA katika kukuza uchumi nchini.


Aidha, Mhe. Rais Samia amemtaka Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Raddy Fiber Manufacturing Ltd kuhakikisha kuwa anakamilisha azma yake ya kujenga kiwanda cha kuzalisha simu janja (smart phone) hapa nchini ambacho pia kitachangia utoaji ajira kwa vijana.


Kiwanda cha Raddy Fiber Manufacturing Ltd kina uwezo wa kuzalisha kiasi cha kilomita 24,000 za optic fiber kwa mwaka na kinatarajiwa kutoa ajira zipatazo 670 kitakapokamilika katika awamu zote na hivyo kukifanya kuwa kiwanda cha tatu kwa ukubwa barani Afrika na cha kwanza kwa Afrika Mashariki na Kati.


Awali akiwa njiani kuelekea Mkuranga, Mhe. Rais Samia alipata fursa ya kuwasalimia wananchi wa Mbagala Zakhem na Vikindu mkoani Pwani ambapo amewahakikishia wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga kuwa kwa sasa Serikali inajenga mazingira bora zaidi ambayo yatawawezesha kufanya biashara kwa uhuru na katika msimu wote wa mwaka.

NAIBU WAZIRI MWANAIDI AIAGIZA TAASISI YA USTAWI WA JAMII KUFANYA UTAFITI HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII

$
0
0

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis akitoa vyeti vya kufanya vizuri wanahitimu katika mahafali ya 45 ya taasisi ya ustawi wa jamii yaliyofanyika leo Desemba 3, 2021 jijini Dar es Salaam.

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis amemuagiza Kamishna wa Ustawi wa Jamii kushirikiana na Menejimenti ya Taasisi hiyo kuainisha maeneo ya ushirikiano na kupanga mikakati ya pamoja ili kuwatumia wahitimu katika utoaji wa huduma za jamii, tafiti na ushauri wa kitaalamu.

Hayo yamesemwa na Mwanaidi Ally Khamis wakati wa Mahafali ya 45 ya taasisi ya ustawi wa jamii yaliyofanyika chuoni hap oleo Desemba 3, 2021 Amesema kuwa serikali inaiangalia taasisis hiyo kwa jicho la kipekee.

Amesema hatua hiyo ni kubwa katika kuimarisha uwezo wa Taasisi ambayo itawezesha kutoa wanafunzi waliobobea katika fani mbalimbali.

Amesema kuwa Katika hotuba ya Bajeti kwa mwaka 2021/2022, Wizara ya afya kupitia Idara ya Ustawi wa Jamii iliainisha maeneo mbalimbali ya utekelezaji ikiwemo kuwezesha mafunzo ya ufundi stadi, ujasiriamali na stadi za maisha kwa watoto wanaokinzana na sheria katika mahabusu za watoto na shule ya maadilisho.

Kuwezesha kuwaunganisha na familia zao watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani katika mikoa 26 nchini, Kuwezesha upatikanaji wa mahitaji ya msingi kwa wazee pamoja na upatikanaji wa huduma za Ustawi wa Jamii kwa wazee katika makazi ya wazee nchini, Kuwezesha utungaji wa Sheria ya Taaluma ya Ustawi, Kufanya mapitio ya mwongozo wa huduma za malezi ya kambo na kuasili pamoja na Kufanya ufuatiliaji wa ubora wa huduma za Ustawi wa Jamii.

"Pia nimefurahishwa na jinsi mlivyoweka mkazo kwenye mafunzo ya vitendo ili kumpa mwanafunzi uzoefu na ujuzi wa ziada katika fani anayosomea. Hatua hii itapunguza ama kuondoa kabisa pengo lililopo kati ya mahitaji ya soko la ajira na uwezo wa wahitimu wetu. Alisema Naibu Waziri Mwanaidi.

Aidha Naibu Waziri Mwanaidi amewataka wahitimu hao kusimamia misingi na maadili ya taaluma mbalimbali walizojifunza kwenye Taasisi hiyo, pamoja na kuweka uzalendo na upendo kwa nchi yao.

Pia ameipongeza Menejimenti ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii kwa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia hasa kusomesha wahadhiri kwenye ngazi ya Shahada ya Uzamivu (PHD).

Awali Mkuu wa Taasisi hiyo, Dkt. Joyce Nyoni amesema kwa mwaka wa masomo 2020/2021 katika mahafali hayo wahitimu 1,271 sawa na asilimia 68 ni wanawake na 596 ni wanaume, sawa na asilimia 32.

Hata hivyo amesema Taasisi inajivunia mafanikio iliyoyapata ikiwa ni pamoja na kuongeza udahili kutoka wanafunzi 3,159 kwa mwaka wa masomo 2020/21 hadi 5,122 kwa mwaka wa masomo 2021/22.

"Pia imeendelea kuwasomesha walimu pamoja na wafanyakazi katika ngazi mbalimbali ili kukidhi mahitaji yetu na kuendana na kasi ya ongezeko la wanafunzi. Taasisi pia imeendelea kuboresha mitaala yake ili iendane na mahitaji ya soko na kujenga wahitimu wanaolenga katika kujiajiri," amesema Dkt. Nyoni.

Awali Mkuu wa Taasisi hiyo, Dkt. Joyce Nyoni amesema kwa mwaka wa masomo 2020/2021 katika mahafali hayo wahitimu 1,271 sawa na asilimia 68 ni wanawake na 596 ni wanaume, sawa na asilimia 32.

Hata hivyo amesema Taasisi inajivunia mafanikio iliyoyapata ikiwa ni pamoja na kuongeza udahili kutoka wanafunzi 3,159 kwa mwaka wa masomo 2020/21 hadi 5,122 kwa mwaka wa masomo 2021/22.

"Pia imeendelea kuwasomesha walimu pamoja na wafanyakazi katika ngazi mbalimbali ili kukidhi mahitaji yetu na kuendana na kasi ya ongezeko la wanafunzi. Taasisi pia imeendelea kuboresha mitaala yake ili iendane na mahitaji ya soko na kujenga wahitimu wanaolenga katika kujiajiri," amesema Dkt. Nyoni.

 

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis akizungumza na wazazi pamoja na wahitimu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam leo Desemba 3,2021 katika mahafali ya 45 ya taasisi hiyo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis katikati kulia ni  Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya- Idara ya Maendeleo ya Jamii, Patrick Golwike  na kulia ni Mkuu wa Taasisi hiyo, Dkt. Joyce Nyoni 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis akitoa vyeti vya kufanya vizuri wanahitimu katika mahafali ya 45 ya taasisi ya ustawi wa jamii yaliyofanyika leo Desemba 3, 2021 jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Ali Khamis akitoa vyeti vya kufanya vizuri wanahitimu katika mahafali ya 45 ya taasisi ya ustawi wa jamii yaliyofanyika leo Desemba 3, 2021 jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wahitimu wakiwa katika mahafali ya 45 ya taasisi ya ustawi wa jamii leo Desemba 3, 2021 jijini Dar es Salaam.

Wahitimu wakiingia katika mahafali ya 45 ya taasisis ya Ustawi wa Jamii leo Desemba 3, 2021 jijini Dar es Salaam.

WAZIRI SIMBACHAWENE AKAGUA MAENDELEO YA AWALI UJENZI WA JENGO JIPYA LA WIZARA AWAMU YA PILI

$
0
0

WAZIRI SIMBACHAWENE AKAGUA MAENDELEO YA AWALI UJENZI WA JENGO JIPYA LA WIZARA AWAMU YA PILI, MJI WA SERIKALI, JIJINI DODOMA, KUKAMILIKA OKTOBA 2023.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Ujenzi na Uhandisi wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Haikamen Mlekio (kushoto) ambaye ni Mkandarasi wa ujenzi wa jengo jipya la ghorofa sita la Wizara yake, awamu ya pili katika Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya awali ya ujenzi huo, leo Desemba 3, 2021. Watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. Jengo hilo linatarajiwa kukamilika Oktoba 14, 2023. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Muonekano wa jengo jipya la ghorofa sita la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi litakapokamilika katika Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, Oktoba 14, 2023. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akiangalia ramani ya ujenzi wa jengo jipya la ghorofa sita la Wizara yake, awamu ya pili katika Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya awali ya ujenzi huo, leo Desemba 3, 2021. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. Jengo hilo linatarajiwa kukamilika Oktoba 14, 2023. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza jambo na Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima (kushoto), baada ya kumaliza kukagua maendeleo ya awali ya ujenzi wa jengo jipya la ghorofa sita la Wizara yake, awamu ya pili katika Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, leo Desemba 3, 2021. Katikati ni Msajili wa Jumuiya wa Wizara hiyo, Emmanuel Kihampa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akimpa maelekezo Mshauri Elekezi, Peter Salyeem (kushoto) wa ujenzi wa jengo jipya la ghorofa sita la Wizara yake, awamu ya pili katika Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya awali ya ujenzi huo, leo Desemba 3, 2021. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. Jengo hilo linatarajiwa kukamilika Oktoba 14, 2023. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


JUKWAA LA KWANZA LA BIASHARA NA UWEKEZAJI LAFANYIKA ITALIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Roma
Jukwaa la kwanza la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Italia limefanyika Jijini Roma kwa mafanikio makubwa, Italia na kuwakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji zaidi ya 250 kutoka nchi zote mbili hasa katika kipindi hiki cha Uviko 19.

Pamoja na mambo mengine, jukwaa hilo limewawezesha wafanyabiashara na wawekezaji kujadili fursa, uwezekano wa ubia, changamoto zinazokabili mazingira ya biashara na njia ya kuboresha mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Italia ambapo limendaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Italia kwa kushirikiana na Kituo cha Taifa cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mamlaka ya Taifa ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA). 
Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya ambapo Prof. Manya amewaeleza wawekezaji na wfanyabiashara kutoka Italia kuwa Tanzania kwa sasa imejikita kuwekeza katika miundombinu wezeshi ya uwekezaji, na kwamba hilo ndilo jambo ambalo Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Rais  Samia ameliweka suala la uwekezaji kama kipaumbele katika kuhakikisha kuwa wawekezaji kutoka nje na ndani ya nchi wanawekeza fedha na mitaji yao ili kukuza biashara na ajira kwa watanzania na kuwezesha uchumi wa Tanzania kusonga mbele.

“Tanzania inathamini uwekezaji na sasa inapiga hatua kwa kuweka miundombinu wezeshi pia Tanzania kama nchi tunamshukuru Mungu kwamba lengo la njozi yetu na maono yetu ya Tanzania Development Vision (2020-2025) imeweza kufikia malengo yake miaka mitano kabla muda uliokuwa umepangwa. Ambapo lengo kubwa lilikuwa ni kuifanya Tanzania kwenda katika viwango vikubwa vya kiuchumi na mwaka 2020 Tanzania ilitangazwa na Benki ya Dunia kuingia katika Uchumi wa kati,” amesema Prof. Manya.

Kadhalika, Prof. Manya ameongeza kuwa katika miaka mitano inayokuja Tanzania inapoelekea kumaliza njozi yake, inatamani kuendelea kukuza uchumi na ikiwezekana ihame katika uchumi wa kati na kuhamia uchumi wa juu……na ndiyo maana imejikita kuwekeza katika miundombinu ya reli ya kati itakayotumika kusafirisha mizigo kwa umeme, ujenzi wa bwawa kubwa linaloweza kuzalisha umeme wa kutosha pamoja na barabara za kusafiri kutoka mashariki kwenda magharibi na kaskazini kwenda kusini.

Ameongeza kuwa Tanzania inajivunia kuwa na hali ya amani na utulivu na katika nchi za ukanda wa maziwa makuu Tanzania inajivunia kuwa na siasa safi yenye utulivu na amani ndani yake.
“Mfano tumeona mwekezaji aliyewekeza katika kilimo cha Pareto ameshuhudia kwa kusema kuwa Tanzania ni nchi ya amani na utlivu na kuwasihi Waitaliano kuja kuwekeza Tanzania,” ameongeza Prof. Manya.

Kupitia jukwaa hili, tunaamini kuwa litachagiza chachu ya uwekezaji zaidi nchini Tanzania na kukuza biashara kati ya Tanzania na Italia.

Mwitikio ni mkubwa na wameonesha utayari wa kuja kuwekeza zaidi Tanzania pamoja na kukuza biashara miongoni mwetu na tumewahahakikishia kuwa Tanzania ni sehemu salama na yenye mazingira mazuri ya Uwekezaji na wameahidi kuwekeza zaidi Tanzania.
Nae Balozi wa Tanzania Nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabiti Kombo amesema kuwa kufanyika kwa Jukwaa la biashara na uwekezaji lengo lake kubwa ni kuwavutia wafanyabiashara na wewekezaji wa sekta mbalimbali kutoka Italia kuwekeza zaidi Tanzania ili kukuza uchumi wa pande zote mbili.

“Mwitikio ni mkubwa sana na tumeitikiwa na Serikali ya Italia vizuri sana pamoja na jumuiya za Italia za kibishara na pia kwa upande wa Tanzania pia mwitikio ni mkubwa pia,” amesema Balozi Kombo.

Mwenyekiti wa Chama Wawekezaji wa Hoteli Zanzibar, Bw. Paulo Rosso amewasihi wawekezaji kutoka Italia kuwekeza kwa wingi Tanzania kwa kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji ni tulivu na salama.
“Tanzania ni sehemu salama kuwekeza, ni nchi ya amani, tulivu kwa uwekezaji, karibuni sana kuwekeza Tanzania,” amesema Bw. Rosso.

Katika Jukwaa hilo, Kampuni mbalimbali za Kiitaliano zimeonesha nia ya kuwekeza Tanzania ambazo ni pamoja na Kampuni ya utengenezaji Magari Ferari ambayo imeonesha utayari wa kuwekeza katika Gereji nchini Tanzania na Shirikisho la Uwekezaji katika Uchumi wa Buluu kutoka Italia pia limeonesha nia ya kuwekeza Tanzania.


MAFANIKIO YA MIAKA SITINI YA UHURU KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

$
0
0

 


Kuhusu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji;

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Sera ya umwagiliaji ya Taifa ya Mwaka 2010, ilitoa Mwongozo wa kuwepo kwa mambo mahususi kwenye uendelezwaji wa sekta ya Umwagiliaji pamoja na mambo mengine ni kuwa na chombo cha kuboresha na kusimamia sekta ya umwagiliaji nchini.

Kilimo cha umwagiliaji kilianzia mkoani Arusha enzi za ukoloni, na baada ya Uhuru serikali iliendeleza mikakati mbalimbali ndipo mipango mahuhusi ilianzishwa  chini ya wizara husika kama Wizara ya maji na kilimo. Ameeleza Bwana Daudi Kaali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

Akiongea Ofisini kwake Mwanasheria wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Bw. Godwin Mutahangarwa,alisema katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Umwagiiaji, ambayo ilitoa muelekeo wa sekta ya umwagiliaji nchini, serikali ilipeleka mapendekezo bungeni ya kuwa na sheria inayoitwa Sheria ya Taifa ya Uanzishwaji wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji. National Irrigation Act ya mwaka 2013.

Imeelezwa kuwa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeanza kutekeleza majukumu yake mwaka 2015, ikiwa ni pamoja na uendelezwaji utekelezwaji na kutoa utaalam na kuratibu na kuthibiti shughuli zote za umwagilaji nchini.

Tume imekuwa ikitekeleza sheria na miongozo na kanuni pamoja na kutoa elimu ya sheria hiyo kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali anabainisha kuwa  Tume  ina mpango wa kuanza kutoa elimu kwa wananchi ya namna bora ya kuvuna maji ya mvua kwa ajili kilimo cha umwagiliaji na matumizi mengine.

Anaongeza kuwa kwa kusema kuwa lengo ni kuwawezesha  wakulima watumie teknolojia ambazo zitawezesha matumizi madogo ya maji ikilinganishwa na sasa ambapo bado wakulima wengi wanatumia mbinu za kizamani.

MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.

Kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi Mkurugenzi huyo anaeleza kuwa kuna mikakati kabambe, imewekwa ya  kuanza kutoa elimu na kuhamasisha wananchi namna ya kuvuna na kutunza maji wakati wa msika ili yaweze kutumika wakati wa kiangazi kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji.

 “Kuna teknolojia za kisasa ambazo zinatuwezesha kufanya kilimo cha umwagiliaji pale tu ambapo mmea unahitaji maji, pamoja na umwagiliaji wa kutumia matone ili maji machache yanayopatikana yatumike kuzalisha chakula hapa nchini,”anaeleza  Kaali.

Baadhi ya Mafanikio katika sekta ya kilimo cha Umwagiliaji katika kipindi cha miaka 60 ya Uhuru.

Kufikia miaka ya 2000 imelezwa kuwa, Serikali imekuwa ikiendelea kuwekeza katika miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji na eneo linalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji kwa sasa ni zaidi ya hekta laki sita, (600,000) na kwa kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inaendelea kupanua eneo la umwagiliaji kufikia hekta 1,200,000 ifikapo mwaka 2025.

Aidha Serikali, imeendelea kuingiza progam mbalimbali katika sekta ya Umwagiliaji kama vile utengenezaji wa mitambo na maboresho ya Miundombinu ya umwagiliaji, kwa kutumia vyanzo vyake vya fedha vya ndani.

Wakulima nchini walikuwa wakilima kwa kutumia njia za asili,Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea kujenga na kuboresha Miundombinu ya kilimo hicho na wakulima wameweza kujiunga katika skimu kupitia vyama vya umwagilia vinavyosajiliwa na Tume ya taifa ya Umwagiliaji hali ambayo inawapa fursa ya wao kulima katika skimu hizo nchini.

Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetambulisha Ada na Tozo kwa wakulima wa kilimo cha umwagiliaji ili kuendeleza ukarabati wa skimu za umwagiliaji na kuzipatia matunzo, na wakulima wameendelea kupata mafunzo mbalimbali ya kilimo cha umwagiliaji kupitia Technolojia mbalimbali za kisasa zinazotumia maji kidogo,ili kuruhusu maji yaende katika shughuli nyingine za maendeleo na ujenzi wa Taifa,kutoka na mabadiliko ya tabianchi yanayosababisha hali ya ukame na ukosefu wa mvua za uhakika.

Ili kuweza kuhimili na kukabiliana na janga hili,Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imekuwa na mikakati ya kuwa na vyanzo vya uhakika vya maji kama vile teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua kwa kuchimba mabwawa yatakayo tumika katika kilimo cha umwagiliaji wakati wa kipindi cha kiangazi.

Bwana Daudi Kaali, Ameeleza kuwa matumizi ya teknolojia ya sensa yaani vifaa vinavyotumika katika kilimo cha umwagiliaji ambapo mkulima atatumia maji kidogo kwa wakati sahihi, teknolojia ambayo imefanyiwa majaribio katika skimu za kilimo cha umwagiliaji mkoani Iringa, imenufaisha wakulima.

Katika ipindi hiki cha miaka 60 ya Uhuru, Idara ya Usanifu na Utafiti; imeweza kuwa kwenye nafasi kubwa ya kusanifu miradi mbalimbali kwa kutumia wataalam wake wa ndani, tofauti na huko nyuma ambapo Tume ya taifa ya umwagiliaji ilikuwa ikitumia wakandarasi washauri kufanya kazi hizo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara hiyo, Mhandisi Gregory Chigwiye, amesema Idara kwa kutumia wataalam wake wa ndani inaanda na kusanifu miradi kumi, na kuweza kuokoa kiasi cha fedha cha shilingi bilioni moja za kitanzania kama ingetumia mtaalam mshauri kutoka nje.

Mhandisi Chigwiye alisema kuwa, upembuzi yakinifu umekuwa na faida nyingi katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji kwani, kabla ya kuanzisha miradi katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji, upembuzi yanikinifu unasaidia kufahamu kama mradi unaoenda kutekelezwa unatekelezeka na utakuwa na manufaa kwa jamii.

“Tafiti hizi pia zinaweza kusaidia kufahamu kama kunaweza kuwa athari zozote katika mazingira na kuangalia namna ya kuhimili na kukabiliana na hali hiyo.” Alisisitiza.

Mhandisi Naomi Mcharo ni kaimu Mkuu wa Kitengo cha uthibiti Ubora kitengo kinachohusika na uangaliaji wa ubora wa miundombinu inayojengwa pamoja na kazi zinazofanyika katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.

Mhandisi Mcharo alifafanua kuwa, katika miaka 60 ya uhuru Idara imekuwa na jukumu la kuhakiki na kuangalia ubora ya miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji kuanzia kwenye mipango ya pamoja ya ujenzi.

Kwa Upande wa TEHAMA ,katika kipindi hiki cha miaka 60 ya Uhuu, Serikali imefanya mambo mengi makubwa kama vile kuanzisha taasisi za serikali kama vile Serikali Mtandao EGa, Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA) hizi zote ni Juhudi za Serikali za kuhakikisha kwamba Teknolojia ya habari na Mawasiliano (TEHAMA) inakuwa  nyenzo muhimu kwa maendeleo ya mtanzania.

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imenufaika na kuwepo kwa mfumo wa mtandao Serikalini wenye kasi, usalama na uhakika ili kuweza kufanya shughuli za ofisi kiufanisi zaidi.

Serikali pia imefanikisha  kuwepo kwa mkongo wa Taifa,kuwepo kwa barua pepe katika Ofisi za umwagiliaji nchi nzima kwa njia salama iliyorahisishwa.

MIRADI KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI NDANI YA MIAKA 60 YA UHURU

Mhandisi Ntonda Kimasa ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya ujenzi na uendelezwaji wa Miundombinu ya Umwagiliaji Amesema Serikali Kupitia Tume ya Taifa ya umwagiliaji imewekeza katika Miradi Mikubwa ya kilimo cha umwagiliaji kama ile ya SSIDP, iliyokarabati na kujenga miradi mikubwa ya kitaifa kama DAKAWA na Lower Moshi, miradi ya ASDP, ERPP na TANCAID awamu ya kwanza na ya pili.

Kwa kipindi hiki cha miaka 60 ya Uhuru uzalishaji katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji kwa upande wa mazao ya chakula hususan zao la mpunga umeongezeka kutoa tani 2 kwa heka kwa  hadi tani 8 hivisasa.

Pamoja na mafanikio yote haya, Tume ya Taifa ya umwagiliaji ina endelea kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwa kutumia wataalam wa ndani ili kuboresha utaalam katika shughuli za ujenzi kama vile wa mabwawa na miundombinu mingine.Hataivyo tume ya Taifa ya Umwagiliaji inawashirikisha wakandarasi wenye zoefu wa kujenga miradi mikubwa ya Umwagiliaji ili kuharakisha Maendeleo ya sekta ya Umwagiliaji.

KILIMO CHA UMWAGILIAJI KWA SASA KINACHANGIA 24% YA CHAKULA NCHINI NA MALENGO KATIKA JAMBO HILI NI KUCHANGIA 50% IFIKAPO MWAKA 2025.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali akizungumza na waandishi wa Habari hawapo pichani, Ofisini kwake jijini Dodoma mapema leo, kuhusu Mafanikio katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji ndani ya kipindi cha miaka sitini ya uhuru.

TGNP YAPONGEZWA KWA JITIHADA ZA KUPINGA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

$
0
0

 




JAMII imetakiwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali, wadau na asasi za kiraia katika kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na mabinti ili kujenga jamii yenye usawa ifikapo mwaka 2022. 

Hayo yameelezwa leo na Diwani wa kata ya Saranga Edward Laizer wakati wa mwendelezo wa siku 16 za Uanaharakati wa kupinga ukatili wa kijinsia uliokutanisha Mtandao wa Vituo vya Taarifa na Maarifa vya Kata za Wilaya ya Ubungo hafla iliyofanyika katika viwanja vya TGNP jijini Dar es Salaam.

"Ili kufanikisha zoezi hili lazima mapambano yaanzie katika ngazi ya familia kwa kuhakikisha hakuna mwanajamii anayethubutu kuonesha vitendo hivyo kwa wanawake na mabinti....Lazima tujenge jamii yenye usawa kuanzia ngazi ya familia." Amesema.

Laizer amesema kuwa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP,) umeleta mabadiliko makubwa tangu kuanzishwa kwake hasa katika ngazi ya familia, jamii na katika ngazi ya kutoa maamuzi.

"TGNP imeleta mabadiliko  mengi kubwa zaidi ni katika kutoa elimu kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi juu ya njia ya kuripoti matukio yoyote ya unyanyasaji wa kijinsia hasa unyanyasaji wa kingono, Serikali kupitia Halmashauri, Wilaya, Kata na Mitaa tupo nao pamoja katika hili na kila mmoja kwa nafasi yake ashiriki vita hii." Ameeleza.

Aidha Laizer ameshauri mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ipewe nguvu zaidi ya kuangazia masuala ya usawa katika umiliki wa mali pamoja na kutambulika na kuipa heshima jinsia ya kike.



Kwa upande wake Diwani wa viti maalum  Wilaya ya Ubungo Liberata Samson ameipongeza TGNP kwa kushirikiana na Mtandao wa Vituo vya Taarifa na Maarifa katika kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

"Vituo hivi ndiyo jamii na vinashuhudia vitendo hivyo, hatua ya TGNP kushirikiana na vituo hivi wanajamiii na waathirika wa matukio haya wanapata ahueni na pahala pa kusemea,....jamii ishiriki katika vita hii na kwa siku hizi 16 za kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ulete mabadiliko chanya kuanzia ngazi ya familia zetu." Amesema.

Awali akitoa taarifa vituo hivyo Mwenyekiti wa  Mtandao wa Vituo vya Taarifa na Maarifa Wilaya ya Ubungo Neema Mwinyi amesema ndani ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia vituo vyote vilivyopo katika mikoa 15 nchini vitajadili mafanikio, changamoto na mwendelezo wa mpango mkakati wa kukomesha vitendo hivyo.

Amesema, Serikali imeweka sera na mikakati ya kupinga vitendo vyote vya ukatili na nguvu zaidi ni kwa jamii kushiriki kwa ukaribu katika kukemea na kuripoti vitendo hivyo.

"Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu katika makundi mbalimbali, kutambulika katika Serikali za Mitaa, Polisi na katika madawati wa jinsia ambapo tumekuwa tukitoa elimu juu ya kupinga vitendo hivyo na jamii imekuwa na mwamko jambo ambalo linaleta matumaini ya kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ubakaji, ulawiti na vitendo vingine vya udhalilishaji." Amesema.

Amesema licha ya kuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutoripotiwa kwa vitendo vya rushwa ya ngono vituo hivyo vimedhamiria kuendelea kutoa elimu, kuwa na mshauri katika kila Kata na Mtaa pamoja na kushirikiana kwa ukaribu na Serikali na wadau katika kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Hafla hiyo iliyowakutanisha wadau wa Mtandao wa Vituo vya Taarifa na Maarifa Wilaya ya Ubungo, Madiwani, wenyeviti wa Mitaa na wanafunzi ni mwendelezo wa siku 16 za uanaharakati wa kupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia kwa kauli mbiu ya 'Ewe Mwananchi Umejipangaje Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Komesha Sasa.'




TCAA YAIBUKA MSHINDI WA PILI MAMLAKA ZA UDHIBITI TUZO ZA NBAA

$
0
0
Mgeni rasmi Mhasibu Mkuu wa Serikali, Leonard Mkude  akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti Uchumi Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Daniel Malanga tuzo ya mshindi wa pili kwa upande wa Mamlaka za Serikali katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka 2020 (Best Presented Financial Statements for the Year 2020 Awards) kwa Taasisi, Makampuni pamoja na Mashirika zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA) kwenye hafla iliyofanyika katika Hotel ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Washindi wa pili wa tuzo zilizotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu wakati wa utoaji wa tuzo za umahiri katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka 2020 (Best Presented Financial Statements for the Year 2020 Awards) kwa Taasisi, Makampuni pamoja na Mashirika zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) kwenye hafla iliyofanyika katika Hotel ya APC Bunju jijini Dar es Salaam..
Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuibuka mshindi wa pili kwa upande wa Mamlaka za Serikali katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka 2020 (Best Presented Financial Statements for the Year 2020 Awards) kwa Taasisi, Makampuni pamoja na Mashirika zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA)
Viewing all 39120 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>