Quantcast
Channel: MTAA KWA MTAA BLOG
Viewing all 39280 articles
Browse latest View live

WANANCHI TUMBE WASHIRIKI KUPANDA MIKOKO KATIKA BONDE LA PONDEANI

$
0
0
WANANCHI wa Tumbe, Kamati za mazingira na jumuiya ya Vijana Wa Tumbe na Viongozi wa Serikali wakipanda miti ya Mikoko katika bonde la Pondeani Tumbe, katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WANANCHI wa Tumbe, Kamati za mazingira na jumuiya ya Vijana Wa Tumbe na Viongozi wa Serikali wakipanda miti ya Mikoko katika bonde la Pondeani Tumbe, katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MITI mbali mbali ya Mikoko ikiwa imepandwa katika bonde la Pondeani Tumbe, katika maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani ambayo huadhimishwa kila Juni 5 ya Kila mwaka.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
AFISA habari kutoka Idara ya Mazingira Pemba, Nassor Ali Salum akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza kazi ya upandaji wa Mikoko huko Tumbe, katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

SPIKA NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI NA KAMATI YA BAJETI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akiongoza kikao cha kamati ya Uongozi na kamati ya Bajeti leo Ofisini kwake Mjini Dodoma kulia kwake ni Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Kushoto kwake ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah na anaefuata ni Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

PICHA: YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Najma Giga akiongoza kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 07, 2017.
 Naibu Waziri Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Angeline Mabula akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 41 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 5, 2017.
 Naibu Waziri Wizara ya Fedha na Mipango Mhe.Dk Ashatu Kijaji akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Dk Medard Kalemani akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
  Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Prof Makame Mbarawa akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
 Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mhe.Anthony Mavunde  katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
  Mbunge wa Kigamboni (CCM) Mhe,Faustine Ndugulile  akiuliza swali katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk Philip Mpango akizungumza jambo na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Gerson Lwenge katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
 Mbunge wa Kasulu Mjini Mhe.Daniel Nsanzugwako akifurahia jambo na Mbunge wa Madaba Mhe.Joseph Mhagama katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma June 7, 2017.
 Mbunge wa Tarime Mjini (CHADEMA) Mhe.Esther Matiko akiuliza swali katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
Mbunge wa Nyamagana(CCM) Mhe.Stanslaus Mabula akiuliza swali katika kikao cha 43 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 7, 2017.
  
Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO,DODOMA.

HASS PETROLEUM GROUP SELLS 40% OF ITS OWNERSHIP TO OMAN TRADING INTERNATIONAL

$
0
0
The Chairman of Hass Petroleum- Mr. Abdinasir Ali Hassan (left) and Mr. Talal Hamid Al-Awfi sign agreements following the sale of Hass Shares to Oman based OTI in Muscat.
Hass Petroleums’ Chairman Mr. Abdinasir Ali Hassan (left) and the Chief Executive of the Oman Trading International (OTI), Mt. Talal Hamid Al-Awfi exchange documents during an event to mark OTI’s acquisition of 40% shareholding in Hass Petroleum.
---
Hass Petroleum Group has sold 40% of its shares to Oman Trading International (OTI) in a move that will see the Kenyan oil marketing company embark on its strategic growth and expansion plans across the Eastern, Central and Horn of Africa.

The Group will invest the additional funding from the transaction to enhance its market visibility through new distribution assets specifically Service Stations across its key markets in the region. It will also boost the marketer’s working capital and increase competitiveness in the Open Tender System. In turn, OTI will provide its supply and trading capabilities to strengthen the Hass service offering, enhance services to consumers and contribute to economic growth across the region.

The Hass founder and management team will continue to operate the business and work closely with OTI to grow and continue long-standing relationships with customers, suppliers and regulators.

This acquisition is in line with the respective companies’ long-term strategies. OTI’s strategic priority of accelerating its growth by entering new emerging markets with high potential will fit well with Hass’s aspiration of being Africa’s leading oil marketing company. As a regular supplier of refined products to the Southern and East African region, this transaction will enable OTI and its new partner Hass to strengthen their businesses across a substantial African footprint.

The completion of the transaction remains subject to approval by the relevant regulatory authorities in the various countries in which Hass operates in.

Abdinasir Ali Hassan Chairman and founder of Hass, commented, "I am delighted to conclude this transaction with OTI. I am convinced that this partnership is a major step in ensuring Hass’ continued competitiveness across the region and I am confident that with OTI we can achieve our mutual long term growth aspirations.”

Talal Hamid Al-Awfi, CEO of OTI, has expressed his satisfaction at the conclusion of the deal “We are delighted to move onto the next phase of growth for OTI, agreeing our first major investment into Africa with Hass. Hass is a unique business with substantial scale and growth potential where we have enjoyed a long standing relationship; most importantly we share a common understanding and vision of the African energy market.”

Standard Advisory London Limited, a member of the Standard Bank Group (“Standard Bank”)acted as exclusive financial advisors to OTI and KPMG Advisory Services Ltd Kenya acted as exclusive financial advisors to Hass.

MAKALA : ASANTE OMOG,TUMEREJEA ALIKOTUTOA RC LIBOLO.

$
0
0
Na Honorius Mpangala.

Mchezo wa soka ni mchezo ambao ili ufanikiwe hauhitaji jitihada za mtu mmoja ila jitihada za timu nzima kuanzia wachezaji,viongozi na benchi la ufundi. Klabu ya Simba imeweza kutembea katika tafsiri hiyo ya mafanikio ya soka yanahitaji ushirikiano wa timu nzima ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Ni kitu ambacho wapenzi na wadau wengi wa soka hawajafahamu dhana ya viraka vilivyopo katika mpira na mwisho vinaunda mpira mwenyewe. Viraka vya mpira ni sehemu ya kuelezea muunganiko unaohitajika katika watu ili kuleta mafanikio ya kitu kizima na pia utofauti wa rangi katika viraka huelezea timu mbili tofauti katika uwanja zinazocheza mchezo wenyewe.

Msimu wa 2016/2017 umekua bora sana kwa klabu ya simba na kufanya klabu imalize ligi nikiwa nafasi ya pili na kufanikiwa kubeba kombe la Azam Sport Federation Cup ( ASFC) msimu huu katika fainali Kali dhidi ya Mbao fc ya Mwanza.

Maandalizi ya klabu ya Simba waliyoyafanya ndiyo matunda ya walichokipata na kitawaletea mafanikio zaidi kama wakiendekea nacho kwa misimu mingine inayokuja.

Moja ya eneo ambalo klabu ya simba ilikua na changamoto na kujikuta wanashindwa kujishika vizuri ilikua katika eneo la benchi la ufundi,naweza kusema Benchi la simba limetibiwa ipasavyo.

Joseph Omog huyu mkameruni ni moja ya makocha wazuri na wenye kuamini katika nidhamu ya mchezaji mmoja na baadae nidhamu ya klabu kwa ujumla. Hakuna asiyefahamu mafanikio aliyoyapaya Omog akiwa na klabu Fc Leopard ya Congo Brazzaville alipoifikisha katika fainali ya kombe la shirikisho katika fainali waliyocheza dhidi ya Sc vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Omog alijitangaza katika mashindano ya afrika kama ilivyo kwa George Lwandamina wa yanga alivyojitangaza kupitia Mashindano ya ligi ya mabingwa. Kabla ya ujio wa Omog klabu ya simba ilikua klabu iliyokua ikicheza soka safi lisilo na faida kwao kutokana na upungufu wa nidhamu ya mchezo kupitia utimamu wa mwili na kuhimili mikiki mikiki ya ligi kwa dakika tisini za mchezo.

Omog ni kocha mkali anayejua kusimamia nidhamu,aliondoa hali ya utoto na kuweka mkazo wa kutafuta matokeo kwa faida ya klabu na sio mtu pekee.
Awali ilionekana kama utani wakati simba waenda kuweka kambi yao katika hostel za seminary pale bingwa Morogoro na kuweka mazingira ya kujidhatiti kwa klabu.

Kulikua na utofauti mkubwa kati ya uongozi wa benchi la ufundi chini ya Omog na ilivyokua kwa Jackson Mayanja ambako tuliona mikwaruzano ya chini chini kati yake na wachezaji,mfano kile kilichotokea kati ya Mayanja na Hassan Isihaka na Hamis Kiiza.

Zoezi la usajili walilolifanya kwa upande wa wachezaji walifanikiwa japo sio kwa asilimia kubwa na hilo ni kutokana na aina yetu ya utafutaji wa wachezaji wa kutoka nje ambapo walitumia majaribio.

Usajili wa Javier Belasa Bukungu ulipondwa sana na vyombo vya habari lakini amekuja kuwa thibtishia yeye ni mtu wa tofauti ndani ya uwanja.

Mafanikio makubwa kwa klabu ya simba ilikua pale walipojidhatiti kuivamia mtibwa sugar na kuwasajili Shiza Kichuya,Mzamiru Yassin na Mohammed Ibrahim ilikua usajili bora ambao umeleta matunda kwasababu katika mechi ya FA Mohammed Ibrahim ndo mfungaji wa bao la kuwapeleka fainali na Kichuya akafunga la kuipa Ubingwa wa FA achilia mbali magoli yake mawili ya mechi dhidi ya yanga ambayo yalimtengenezea jina zaidi na zaidi Kichuya.

Wakati ligi ikiendelea na kuona jinsi gani imekua ngumu simba walifanya makosa ambayo hawakuyajua awali kama wanakosea, Safu ya ushambuliaji Ikiongozwa na Laudit Mavugo ilikua inazidiwa magoli na viungo wakiongozwa mzamiru,Mo na Kichuya huku wakiwaacha Mavugo,Fred Blagnon na Ibrahim Ajib wakiwa na idadi ndogo ya magoli.

Simba walimwamini sana Mavugo kuliko Blagnon kwasababu tu mienendo ya uwanjani kati ya hawa wawili ila kiukweli mienendo ya Blagnon inafaida zaidi kuliko Mavugo hii iko wazi ila kinacho mfanya awe nyuma ya Mavugo ni chenga na visigino.

Nafasi na kazi ya Mavugo na Blagnon imenikumbusha hali hiyo kwa Washambuliajj wa kiitalia Fransisco Totti na Alessandro Del Piero. Kazi inayoshindikana kwa Mavugo kwa kipindi cha dakika themanini kiliwezekana kwa Blagnon kwa dakika kumi tu awepo mchezoni.

Dakika kumi za Blagnon ziliamua mechi dhidi ya mbao fc katika Michezo miwili.

Miongoni mwa Michezo ambayo simba walitereza na kuonekana kushindwa kutegua mitego yao ilikua dhidi ya African Lyon mchezo ambao walipoteza dakika za mwisho za mchezo,Mchezo dhidi ya mbeya city jijini Dar es salaam ilikua mtihani kwa klabu ya simba. Endapo benchi la ufundi likaweza kugundua jinsi anavyocheza Mavugo katika eneo la ushambuliaji na kumtazama Blagnon anavyocheza watakua na majibu ya maamuzi katika kuwatumia.
Michezo ya ugenini ambayo ilikua na wakati mgumu dhidi ya Kagera sugar,prisons na Toto Afrika kutokana tu na kujidhatiti wakikofanya wapinzani wao na kutengeneza woga wa safu ya ushambuliaji ya simba kwa kumpa muda mwingi Mavugo ambaye wapinzani walishamgundua aina yake ya uchezaji.

Usajili wa dirisha Dogo kwa kumsajili Athanas Wa stand utd haukua na tija sana kwasababu mtu pekee alitetakiwa kupunguziwa muda wa kucheza ni Mavugo na kupata nafasi Blagnon.

Eneo la kiungo liko bora sana kwa viungo wa kati na tatizo linakuwa kwa mbadala wa Ajib na Kichuya kwa viungo wa pembeni. Uwezo wa Jamal Mnyatte na Athanas sio watu wazuri sana ambao unaweza kusema unaweza kuwatengenezea mzunguko katika kucheza.Ndo maana Alipoyumba Kichuya ilishindikana kwa mnyatte aliyelata nafasi ya kucheza inapobidi.

Mwinyi kazimoto anaendelea kuwa mtu mwenye msaada sana kwa klabu katika kutuliza munkali wa wachezaji na kutafuta matokeo unaweza kupata majibu kwa mechi akizotokea benchi na kucheza kama ilivyo kwenye mechi ya mbao ligi kuu.

Nafasi ya beki simba ilifanya vyema japo Mwalimu alikua akibadilika sana katika nafasi ya walinzi wa kati. Method Mwanjali,Juuko Murshid,Abdi Banda, Javier Besela Bukungu, James Kotei hawa wote kwa nyakati tofauti wamekua wakicheza nafasi hizo na kufanya mwalimu kushindwa kupata pacha iliyo bora zaidi kwake. Majeruhi ya Mwanjali,majukumu ya timu ya taifa ya Uganda kwa Juuko Murshid ni kati ya sababu zilipelekea kuyumba kwa nafasi ya ulinzi na kufanya Mwalimu kufanya mzunguko kwa walinzi wake.

Nini kifanyike kwa msimu ujao.

Yapo mambo machache ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi ndani ya klabu hiyo. Moja, uongozi kupeana majukumu ya klabu kulingana na nafasi kiutendaji na sio kuingiliana katika majukumu hayo kunakotoa mkanganganyiko kwa benchi la ufundi na wachezaji pia.

Tumeweza kujionaea klabu hiyo viongozi wake kila mmoja akitaka kuonekana sana mbele ya vyombo vya habari na kuzungumzia klabu bila utaratibu mazuri na kufanya kila mmoja kuonekana anajitengenezea mazingira ya kuwepo katika nafasi ya uongozi kwenye uchaguzi ujao.

Mbili,Utulivu wa benchi la ufundi uliopo wasije kuutibua na kumfanya bundi akatua katika paa la jengo lao kwasababu ya kutotekeleza matakwa ya kocha baadaa ya kumaliza ligi.

Tatu,ziko nafasi zinazogitaji marejebisho ili kufanya simba kung'ara zaidi kama nafasi ya mlinzi wa kulia wanajitaji mtu wa kusaidiana na Bukungu kwasababu aliyekuwepo kashindwa kumpa changamoto na nafasi hiyo itakuwa bora sana kama wataweza kumshawishi Salum kimenya wa Tanzania prisons kujiunga nao.

Nafasi nyingine ambayo wanapaswa kuifanyia maamuzi ni kutazama upya nafasi ya kiungo mkabaji toka nje ya nchi kwasababu James Kotei ameweza kufit eneo la ulinzi kwa kucheza na Juuko hivyo kumwondoa katika mfumo Method Mwanjali anayeonekana kuwa na umri mkubwa na kushindwa kumudu kasi ya ligi.

Upande wa mlinzi wa kushoto ni eneo ambalo kwao halina matatizo kwani uwepo wa Abdi Banda na Mohammed Hussein ni tiba tosha na kinachobaki ni kutuliza akili zao na kutambua thamani ya mashindano wanayoshiriki hasa kwa banda mwenye vitendo visivyo vya kiungwana mchezoni.

Kwa upande wa nafasi ta ushambuliaji simba wana kila sababu ya kuwatazama vizuri vijana wao waliopita klabu ya simba mbaraka Yusuph na waziri junior,pia wana kila nafasi ya kuwatazama vizuri wachezaji kama Stamili Mbonde wa mtibwa sugar.

Kwa upande wa mchezaji wa nje ambaye anaweza kuondoka ni Method Mwanjali na nafasi yake kuchukuliwa na Kotei na kufanya nafasi ya kumsajili kiungo mkabaji wa kumpa changamoto Jonas Mkude.

@Mido sankala

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AZINDUA SHUGHULI YA USAMBAZAJI VIFAA KUFUNDISHIA SAYANSI

$
0
0
Waziri  Mkuu  Kassim  Majaliwa  akiangalia Mtoto wa Darasa la saba anayesoma shule ya Uhuru  Mchanganyiko Mariana  Alex  Mwenye  ulemavu  wa macho, anavyoweza kuandika  kwa kutumia  mashine  maalumu  ya kuandika, June 6 2017 Waziri  Mkuu  alikabidhi  vifaa  vya Kujifunzia   katika shule mbalimbali hapa Nchini Shughuli hiyo imefanyika Jijini  Dar es salaam
Waziri  Mkuu  Kassim  Majaliwa  akijaribu  kuandika  kwa kutumia  kifaa maalumu  cha kujifunzia  kuandika  watoto wenye ulemavu  wa Macho 6 June2017, Kulia kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Elimu na Sayansi  Profesa  Joyce Ndalichako, Waziri  Mkuu  alikabidhi  vifaa  vya Kujifunzia   katika shule mbalimbali hapa Nchini Shughuli hiyo imefanyika  Jijini  Dar es salaam
 Waziri Mkuu  Kassim  Majaliwa  akisalimiana na Ofisa wa Banki ya Dunia anayeshughulikia  Elimu  nchini  Tanzania  Bibi  Cornelia  Jesse, katikati ni Ofisa  wa  Ubalozi  Swiden  Nchini Tanzania  anayeshughulikia Elimu Bibi Helena  Reutersward , maofisa hao walishiriki katika Uzinduzi  wa Usambaziji  vifaa  vya  kufundishia  Masomo ya  Sayansi  Shughuli hiyo ilifanyika 6 June 2017   katika  Viwanja  vya  Jeshi  Lugalo  Dar es salaam. Picha na Ofisi  ya  Waziri  Mkuu

NATAMANI KUCHEZA .LIGI YA TANZANIA - MUKHWANA

$
0
0
 Beki wa kati wa timu ya Nakuru All Stars James Sadicky Mukhwana akipambana na kiungo wa Simba Mohamed Ibrahim wakati wa mpambano wao uliofanyika jana katika michuano ya Sportpesa Super Cup.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.


Beki wa kati wa timu ya Nakuru All Stars James Sadicky Mukhwana amesema kuwa anaamini ipo siku atacheza katika mojawapo ya timu za ligi kuu nchini Tanzania.


Beki huyo mwenye mwili uliojazia n a urefu wa futi sita amesema kuwa anaitamani sana ligi ya Tanzania na kama ikitokea timu itakayomuhitaji yupo tayari kuitumikia ili mradi wakubaliane.

Mukhwana ambaye jana katika mchezo wa Nakuru All Stars dhidi ya Simba alionekana mwiba kwa safu ya ushambuliaji wa timu ya Simba na kuweza kuhakikisha hakuna mshambuliaji anayetikisa nyavu za timu yao.

Beki huyo mwenye umri wa miaka 26, amepitia katika timu mbalimbali za nchini ikiwemo kituo cha kukuzia vipaji cha Nakuru Youth Olympic  mwaka 2002 akiwa na umri wa miaka  12 na baadae kupandishwa mpaka timu kubwa ya Nakuru All Stars na kuitumikia kwa miaka miwili.

Baada ya kuachana na Nakuru Mukhwana alijiunga na Complay Fc ya ligi daraja la kwanza mwaka  2013 na kuitumikia timu hiyo kwa  mwaka mmoja na baadae kuhamia Osiria Fc mwaka 2014.


Mukhwana hakuweza kudumu sana katika timu ya Osiria na kujiunga na Bitiko United mwaka 2015  na kucheza kwa miezi sita na kuamua kwenda St joseph na kumalizia miezi sita iliyobaki ambapo zote zinashiriki ligi daraja la kwanza. Mwaka 2016, Mukhwana alijiunga na Nakumat  na 2017  kuhamia Nakuru All stars ambapo anacheza mpaka sasa.


Mukhwana amesema bado anaamini anauwezo wa kucheza mpira na anatamani sana kucheza ligi kuu ya Uingereza huku akisfia uwezo wa mchezaji raia wa Kenya Victor Wanyama anayekipiga katika timu ya Totenham,   David Kalaba wa Zesco na mchezaji wa nje Thiago Silva.

Nakuru wapo nchini kwa ajili ya michuano ya Sportpesa Super Cup inayoendelea ikizikutanisha timu nane ambapo kwa sasa umeingia katika hatua ya nusu fainali mechi zitakazopigwa kesho kati ya Yanga na AFC Leopard huku mchezo wa pili ukiwa kati ya Nakuru All Stars na Gor mahia.

MAKAMU WA RAIS AMALIZA ZIARA MUSOMA MJINI LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia wakazi wa Musoma mjini kwenye kiwanja cha Mukendo ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake mkoani humo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia boksi lililohifadhiwa samaki tayari kwa kusafirisha nje ya nchi wakati alipotembelea kiwanda cha Kuchakata Samaki cha Musoma.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka Serikalini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassana ametoa kauli hiyo wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Musoma katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mukendo mjini Musoma.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa Serikali itapeleka chakula kwa wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa kwa mvua au yalikauka kwa ukame au kwa  maafa mengine na sio kwa wananchi wanaokaa vijiweni mchana kutwa bila kufanya kazi wakisubiri neema ya chakula kutoka kwa Serikali.
Amewahimiza wananchi kote nchini kuendelea kufanya kwa bidii ikiwemo shughuli za kilimo na pindi wanapovuka wajiwekee akiba na waache tabia ya kuuza mazao yote wanayovuka ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula kwenye familia zao.
Makamu wa Rais pia amewataka viongozi wa mkoa wa Mara washirikiane na wananchi katika kuwaelemisha mbinu bora za kilimo ili waweze kupata mazao mengi ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.
Kuhusu tatizo la uvuvi haramu, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameziagiza Kamati za Ulinzi na Usalama kufanya misako ya hali na mali katika kupambana na tatizo hilo ambalo limechangia kupunguza samaki katika maeneo mbalimbali nchini.
Ametoa mfano kwa mkoa wa Mara kuwa ulikuwa na viwanda Vinne vya kuchakata samaki lakini kutokana na shughuli za uvuvi haramu na wa kutumia sumu umepelekea viwanda Vitatu kukosa malighafi hiyo na kusitisha uzalishaji.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema jambo hilo ni baya kwa sababu limeikosesha Serikali mapato na kusababisha wananchi wakose ajira kutoka kwenye viwanda hivyo jitihada za makusudi lazima zifanyike katika kukomesha uvuvi haramu katika maeneo mbalimbali nchini hasa katika Ziwa Victoria.
Aidha, Makamu wa Rais ameeleza kufurahishwa na kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji wa Musoma ambao umetekelezwa na Serikali ya Tanzania na Serikali ya Ufaransa  na kusema kuwa mradi huo utaondoa tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa wilaya ya Musoma.
Amewataka wananchi wa Manispaa ya Musoma kuulinda na kuutunza mradi huo ili uweze kudumu kwa miaka mingi kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa Manispaa hiyo.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mara Dakta Charles Mlingwa amewahimiza wananchi wa mkoa wa Mara kuweka itikadi zao kando na washirikiane katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.
Makamu wa Rais katika ziara yake katika wilaya za Butiama na Musoma amekagua shamba la mbegu bora za muhogo katika eneo la Rwamkoma, Butiama na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Mutex hadi Buhare yenye urefu wa kilomita 9.9 katika Manispaa ya Musoma pamoja na kutembelea kiwanda cha kuchaka samaki cha Musoma.

TUTAINGIA KWA AJILI YA USHINDI DHIDI YA GOR MAHIA- KOCHA NAKURU

$
0
0
Kikosi cha Nakuru All Stars

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
KOCHA Msaidizi wa timu ya Nakuru All Stars Jimmy Angila amesema kuwa mchezo wa hatua ya nusu fainali ya Kombe la Sportpesa Super Cup 2017 dhidi ya Gor Mahia utakuwa ni mgumu sana ila wana imani watatoka na ushindi.

Akizungumza na mtandao huu,  Angila amesema kuwa katika mchezo wao huo hawatakubali kuona wanapoteza kwani kwa wao ni muhimu sana kuingia fainali na cha zaidi hawataingia kwa kuidharau bali watahakikisha wanashinda.

Amesema kuwa, wanaifahamu vizuri timu ya Gor Mahia na zaidi wanatarajia mechi hiyo kuwa ngumu sana kwa kila upande.

"mechi yetu dhidi ya Gor Mahia ni ngumu sana ila tutaingia uwanjani kwa kuhakikisha tunashinda mchezo huo ambao ni muhimu sana kwetu kwani lengo letu ni kuingia fainali,"amesema Angila.

Angila alisisitiza kuwa kikosi chao kipo vizuri na benchi la ufundi ndiyo litapanga kikosi cha kesho na mabadiliko yanaweza kufanywa kulingana na hali za wachezaji.

Daktari wa timu ya Nakuru Vicent Angwenyi amethibitisha kutokuw ana majeruhi katika kikosi chao na zaidi wote wanaweza kucheza katika game mechi ya kesho dhidi ya Gor Mahia.

Timu hizo kutoka Kenya zinakutana katika hatua ya nusu fainali ya  Kombe la Sportpesa Super Cup 2017 na mchezo huo unatarajiwa wa ushindani mkubwa kwani timu hizo mbili zinajuana huku Gor Mahia ikiwa inashiriki ligi kuu ya Kenya na Nakuru ikiwa ligio darala la kwanza.

DIRA YA DUNIA YA BBC KISWAHILI

Benny Kisaka amlilia Marehemu Balozi Cisco Mtiro

$
0
0
 
Na Benny Kisaka

Abdulkarim Omary Mtiro, almaarufu Cisco Mtiro, umelala Brother tangulia.

Umelala usingizi. Usingizi ambao hautaamka wakati huu. Hautaamka brother kwa kuwa wanaolala usingizi huu wanamngoja aliyewaumba awaamshe.

Kwa neema yake kuu iko siku utaamka Brother. Mara hii ukiamka hutalala tena.

Naam, hutalala. Maana utakuwa umevuka ng'ambo ya pili ya mto. Huko hakuna uchungu na maumivu makali kama uliyoyapitia nyakati zako za mwisho za uhai wako ukiwa hospitali ya Aga Khan. Pumzika kaka yetu.

Leo June 7, saa 7 mchana tunakuzika kwenye makaburi ya Kisutu mahali ambapo miezi michache iliyopita tulimzika rafiki yako wa karibu Afande Chicco. Pumzika kwa amani, mpaka tutakapoonana tena huko juu Ng'ambo ya pili.

Mwanadiplomasia uliyewahi kuwa balozi mdogo Nigeria na pia Balozi Kamili nchini Malaysia.

Tunakuita brother kwa wakazi wa Temeke tukijua umezaliwa peke yako kwa Mzee Omary na Bi Ummi Seif.

Akiwa amezaliwa mtaa Kipata Kariakoo mwaka 1950, baada ya miaka miwili alihamia Temeke hadi anamaliza elimu ya Chuo Kikuu, alihama pale alipoanza kazi wizara ya mambo ya Nje.

Cisco ni jina la utani lililochepua hadi kuliweka rasmi hata kwenye passport yake ikisomeka Abdul Cisco Mtiro amefariki akiwa na miaka 67.

Leo Temeke itanyanyuka eneo ulilokulia na kusoma elimu yako ya msingi shule ya Temeke, na kumaliza elimu hiyo mwaka 1965.

Itakumbukwa 1997 aligombea Ubunge Temeke akishindana na Mrema, viongozi wote wa ngazi za juu wa CCM walikuja kukupigia debe lakini kura hazikutosha.

Umaarufu wako upo Chang'ombe, Ilala, Wailes, Kurasini Masaki, Magomeni, Mbezi Beach, Kariakoo na hata Kinondoni yote.

Ameishi Mikocheni B hadi umauti umemkuta, lakini muda mwingi amekuwa akikutana na marafiki zake viunga vya Kinondoni kwa John Fedha ama nyuma ya ubalozi wa Ufaransa kijiwe cha Octa.

Ni mmoja wa waanzilishi wa bonanza la kila jpili pale Leaders Club, mshabiki mkubwa wa Yanga, rafiki wa kila tabaka na rika na hakuwa mtu wa kujikweza, umaarufu wake ulitawala kwa kuwa mtu mwenye utani mwingi...

Ni mtoto wa mjini hasa, hakuhitaji aimbwe redioni kutokana na sababu zozote.

Nilikuwepo Kisutu kukuzika bro, ulishiriki msiba wa baba yangu Christopher kisaka, ambaye alikuwa mwalimu wako shuleni Temeke, ulitukaribisha nyumbani kwako kupata chakula cha jioni mara kadhaa tulipofika Kuala Lumpur, Malaysia 2011 nikiwa na Juma Pinto, ulinialika arusi ya mwanao Omary, pia nilishiriki.

Mwanadiplomasia, mkuu wa Itifaki mstaafu kwa Mwalimu Nyerere, Mzee Mkapa na awamu ya nne ya Jakaya Kikwete. Ulikuwa mgeni rasmi miss Temeke 2003. Ulikuwa judge miss Tanzania 2004.

Cisco ana marafiki lukuki kiasi kila mmoja anaweza kumwandika amjuavyo, tena zaidi na vizuri kutipa mimi, ila kwa udogo huu naomba mwenyezi Mungu akupumzishe kwa Amani.

MKURUGENZI MKUU TMF AFUNGUA MAFUNZO YA KARIKACHA NA VIBONZO JIJINI DAR LEO

$
0
0
Mkurungenzi wa Mkuu wa Tanzania Media Foundation (TMF), Bw. Ernest Sungura aliyekaa mbele katikati akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kuchora vibonzo vijana muda mfupi baada ya kuzindua rasmi warsha ya kuwajengea uwezo vijana katika Uchoraji wa Vibonzo, yanayoendelea katika kiota cha wasanii cha NAFASI, Mikocheni jijini Dar es salaam. Mafunzo hayo yanatolewa na asasi ya Nathan Mpangala Foundation (NMF) na kufadhiliwa na Ubalozi wa Uswis nchini. Kushoto kwa mgeni rasmi ni Mwenyekiti wa NMF, B. Nathan Mpangala wakati kulia kwake ni afisa utawala wa Nafasi Art Space. Mafunzo yatamalizika kesho ambapo Balozi wa Uswis nchini tanzania, bi. Florence Tinguely Mattli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Mwezeshaji Nathan Mpangala, akimwelekeza jambo mmoja wa washiriki wa warsha ya karikacha na uchoraji vibonzo yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Penye vibonzo hapakosi tabasamu.
Baadhi ya washiriki wakifanya yao.
Mchoraji, Said Michael maarufu kama ‘Wakudata’ akifanya yake.

Halotel yajivunia kujiunga mfumo wa ulipaji kodi Kielectroniki

$
0
0
Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Halotel, imeipongeza serikali kwa kuweka mfumo wa kukusanya kodi kwa njia rahisi na yenye uwazi na kufafanua kuwa wao wamekuwa kampuni ya kwanza kujiunga na kufurahia utaratibu huo kama ilivyobainishwa na kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kichere, kwani unawezesha kampuni kuwa wazi katika malipo yote ya kodi na tozo wanazozifanya kwa wateja.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo bwana Le Van Dai, amefafanua kuwa wao kama kampuni siku zote wamejiweka mbele katika kuhakikisha wanatimiza matakwa ya serikali kwa kufuata taratibu zote zinazowekwa na mamlaka husika.

“Tulipofahamishwa kuhusu utaratibu huu wa ukusanyaji kodi tulifurahia sana kwa sababu unaweka wazi maendeleo ya biashara na ukusanyaji wa mapato ya serikali, sisi kama wawekezaji tunafurahia kuwa na njia bora za usimamizi wa mapato ya serikali na kampuni husika kwani unatuwezesha sisi pia kujipima kujua biashara kama ni nzuri au sivyo na kuangalia namna bora ya kushauriana na mamlaka husika katika kufanikisha mazingira bora ya kibiashara” Alisema Dai.

Aidha, Mkurugenzi huyo pia aliwaeleza waandishi wa habari kuwa wanaendelea kufurahia mafanikio ambayo kampuni hiyo imekuwa ikiyapata tangu kuanzishwa kwake.

“Katika taarifa ya robo ya kwanza ya mwaka huu 2017 iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeonesha namna ambavyo kampuni yetu imeendelea kufanya vyema katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita,”

"Kimsingi, idadi ya wateja wa kampuni za simu ilipungua kutoka 40,173,783 kwa Desemba mwaka jana na kufika39,856,212 kwa Machi mwaka huu. Hii ina maana kuwa kuna baadhi ya mitandao ya simu ilipoteza wateja ila Halotel tumeweza kuongeza wateja wapya wapatao 73,872. Hii ni ishara kuwa Watanzania wanaridhika na huduma zetu. Tunawaahidi kuwa hatutawaangusha," alisema,”

Alisema Dai na kuongeza kuwa “hii ni dalili nzuri kwetu kibiashara. Tunawashukuru Watanzania kwa kuendelea kutuamini na kuendelea kujiunga na sisi, tunawaahidi kuendelea kuboresha huduma zetu na kuufanya Halotel uendelee kuwa Mtandao chaguo namba moja kwao.” Alihitimisha Mkurugenzi huyo.

Pamoja na mambo mengine Mkurugenzi huyo amesema kampuni hiyo bado inatoa kipaumbele kwa kutoa huduma bora kwa jamii ya Watanzania ikiwepo pamoja na kuwezesha miundombinu ya mawasiliano kwa taasisi mbalimbali za serikali pamoja na taasisi za kijamii, zikiwemo shule, hospitali, ofisi za posta na halmashauri mbalimbali. Hivi karibuni kampuni hiyo ilitangaza uwekezaji wa Zaidi ya bilioni 200 katika kuboresha ubora wa mtandao huo, ikilenga kuongeza kasi ya intaneti na ubora wa huduma za sauti.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halotel, Le Van Dai, Akizungumza na waandishi wa habari wakati kampuni hiyo ilipokuwa ikitoa pongezi kwa serikali kwa kuanzisha mfumo wa wawazi wa ulipaji kodi kwa njia ya kielektroniki, Kampuni hiyo ni miongoni mwa makampuni matatu ya simu ya kwanza kujiunga na mfumo huo ambao amefafanua kuwa unaweka uwazi katika biashara. Pamoja nae katika picha ni Meneja Uhusiano wa Kampuniu hiyo Stela Pius na Meneja Mawasiliano Hindu Kanyamala (Kushoto).
Meneja Mawasiliano wa Halotel, Hindu Kanyamala akifafanua jambo kwa waandishi wa habari, Wakati kampuni hiyo ilipofanya mkutano wa kuipongeza serikali kwa kuanzisha mfumo wa ulipaji kodi kwa njia ya kielectroniki. Katikati ni Mkurugenzi Mtenzaji wa Kampuni hiyo Le Van Dai na Meneja Uhusiano Stella Pius.

Ndesamburo Amuibua Dr Slaa

$
0
0
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa amesema kuwa amesikitishwa sana na kifo cha Mzee Philemon Ndesamburo na kueleza jinsi walivyokijenga chama pamoja.

Dk. Slaa amesema kuwa licha ya Ndesamburo kuwa na utajiri mkubwa, lakini hakuuona kuwa ni kitu bali ni nyenzo ya kuwakomboa wananchi katika sekta mbalimbali.

Dk. Slaa ameitoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tangu aliyekuwa Mbunge wa Moshi Mjini kwa miaka 15, Mzee Philemon Ndesamburo alipozikwa nyumbani kwake KDC Moshi baada ya kufariki wiki iliyopita alivyopata matatizo ghafla akiwa ofisini kwake.

Dk. Slaa ambaye sasa anaishi Toroto nchini Canada baada ya kujiuzulu  wadhifa wake na kuachana na siasa tangu mwaka juzi, alisema kuwa ameshtushwa sana na kifo cha ghafla cha kiongozi huyo tegemeo. Alieleza kuwa licha ya wao kubaki na majonzi, lakini anaamini kazi ya Mungu haina makosa wala haihojiwa.

"Ni kweli nimefanya kazi na Ndesamburo, tumejenga CHADEMA kwa pamoja hasa kipindi cha mwaka 2003 hadi 2005 ambapo tulizunguka nchi nzima," alisema Dk. Slaa na kuongeza kuwa licha ya mazingira magumu waliyokutana naye kwenye harakati za kukitangaza chama hicho, Mzee Ndesamburo hakulalamika alipotakiwa kulala chini, lakini aliona hizo ni changamoto za kutafuta ukombozi.

Aidha, Dk. Slaa alisema kuwa Mzee Ndesamburo alikuwa msikivu na mwenye kuelewa na kuwa tayari kuwasaidia wengi kwa hali na mali kwani mara kadhaa alitoa mali zake kuwasaidia wagombea wa CHADEMA na hata yeye mwenyewe kwenda kuwapigia kampeni bila kujali umbali aliotakiwa kwenda.

Akizungumzia kifo chake, Dk. Slaa alisema kuwa kifo hicho ni cha kusikitisha kwa sababu alifariki ghafla, hakupata nafasi ya kuagana na ndugu jamaa na marafiki. 

"Wakati mwingine afadhai mtu akiugua mnajiandaa kisaikolojia, ila akifariki ghafla tu, huwa ni kazi ngumu kuipokea ile hali.Kazi kubwa iliyobaki kwa watanzania sasa ni kutekeleza yale yote ambayo Mzee Ndesamburo amewaachia huku tukimuombea Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi."

Dk. Slaa aliondoka nchini mwaka 2015 baada ya kujiuzulu wadhifa wake kufuatia chama chake kumpokea na kumpa nafasi ya kugombea urais, aliyekuwa kada nguli wa CCM, Edward Lowassa.


Bajeti Kuu ya Serikali Kusomwa Leo

$
0
0
Nchi  za Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania zinawasilisha bajeti zao kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango anatarajiwa kuwasilisha bajeti hiyo bungeni leo mjini Dodoma  kuanzia saa 10 kamili jioni.

Kabla ya kufanya hivyo, asubuhi Dk Mpango atawasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi ya nchi, ambayo itajikita katika kueleza mipango ya maendeleo kwa mwaka ujao. 

Kwa mujibu wa ratiba ya Bunge la Tanzania katika Mkutano wake wa Saba wa Bunge la Bajeti, wabunge watatumia kesho kusoma na kutafakari hotuba hiyo.

Kuanzia Jumatatu ijayo Juni 12 hadi Juni 20, mwaka huu, wabunge watajadili Taarifa ya Hali ya Uchumi na Bajeti ya Serikali kwa siku saba kabla ya jioni ya Juni 20, mjadala kuhitimishwa kwa upigaji kura ya wazi.


Serikali kuendelea kudhibiti matumizi ya fedha za umma yasiyo ya lazima

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina imeahidi kuendelea kusimamia na kufuatilia sheria na miongozo yote iliyotolewa ili kuhakikisha lengo la kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima kwenye Mashirika na Taasisi za Umma ikiwemo safari za nje na posho za wajumbe wa Bodi za mashirika na Taasisi zote za Umma linafanikiwa.

Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Vwawa (CCM), Mhe. Japhet Hasunga ambaye alitaka kujua hatua ambazo Serikali inatarajia kuchukua kudhibiti matumizi ya fedha za Umma katika Taasisi zake.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Serikali imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa matumizi ya fedha za Umma yasiyo ya lazima yanadhibitiwa kikamilifu kupitia Sheria mbalimbali zilizotungwa na Bunge ikiwemo Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 ambayo imebainishwa hatua mbalimbali za kibajeti zenye lengo la kuongeza usimamizi na udhibiti wa matumizi ya fedha za Umma katika Mashirika na Taasisi za Umma.

“Sheria hiyo imebainisha utolewaji wa Mwongozo wa Mipango na Bajeti wa Serikali unaojumuisha Mashirika na Taasisi zote za Serikali ambao unatoa miongozo mbalimbali ya kuzingatiwa katika matumizi ya Umma kwa mwaka husika,” alifafanua Dkt. Kijaji

Alisema kuwa kupitia Sheria hiyo, Ofisi ya Msajili wa Hazina imepewa mamlaka ya kupitia bajeti za Mashirika na Taasisi zilizo chini yake kwa kuzingatia miongozo na mipango ya Serikali inayotarajiwa kutekelezwa.

Mhe. Kijaji alibainisha kuwa katika Sheria hiyo Ofisi ya Msajili wa Hazina imepewa jukumu la kupitia na kuridhia kanuni za fedha za Mashirika na Taasisi zote za Umma ili kuimarisha usimamizi na udhibiti wa matumizi ya fedha za Umma.

“Sheria nyingine iliyopitishwa na Bunge ni marekebisho ya Sheria ya Fedha ya Mwaka 2015 ambayo iliweka ukomo kwa Taasisi na Mashirika ya Umma kutumia asilimia 60 tu ya mapato yake kwa matumizi ya kawaida yasiyojumuisha mishahara,” aliongeza Dkt. Kijaji.

Aidha, Dkt. Kijaji alisema kuwa katika kuhakikisha Ofisi ya Msajili wa Hazina inatekeleza majukumu yake kisheria, imetoa miongozo mbalimbali yenye lengo la kudhibiti matumizi ya Mashirika na Taasisi za Umma ili kupunguza matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima.

“Miongoni mwa miongozo hiyo ni barua iliyotolewa na Msajili wa Hazina tarehe 10 Novemba, 2015 ya kudhibiti safari za nje ya nchi zisizo za lazima kwa watumishi wa Mashirika na Taasisi za Umma ambazo awali zilionekana kutumia sehemu kubwa ya fedha za Umma,” alisema Dkt. Kijaji.

Aliongeza kuwa waraka wa Msajili wa Hazina Na. 12 wa mwaka 2015 kuhusu Posho za Vikao vya Bodi ya Wakurugenzi wa Mashirika na Taasisi za Umma pia ni miongoni mwa miongozo ya kuzuia matumizi yasiyo ya lazima kwani waraka huo umefuta posho za vikao vya Bodi na kuondoa utaratibu wa Bodi kuwa na vikao zaidi ya vinne kwa mwaka.

Dkt. Kijaji alisema kuwa Waraka wa Msajili wa Hazina Na. 1 wa mwaka 2016 kuhusu posho za kujikimu kwa Wajumbe wa Bodi za Wakurugenzi wa Mashirika na Taasisi za Umma ulikuwa na lengo la kuendeleza jitihada za Serikali kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za Umma.

Alisema kuwa Waraka huo uliweka ukomo wa posho hizo kwa Wajumbe wa Bodi kwa safari za ndani na nje ya nchi, huku akisisitiza kuwa bado Serikali itaendelea kuhakikisha matumizi ya fedha za Umma yasiyo ya lazima yanadhibitiwa kikamilifu.

WAZIRI MPANGO AWASILISHA TAARIFA YA HALI YA UCHUMI KATIKA MWAKA 2016 BUNGENI MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasili katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma kwa ajili ya kuwasilisha Bungeni Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2016.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Bungeni Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2016, Mjini Dodoma, ambapo katika mwaka huo, pato la Taifa lilikua kwa asilimia 7.0, likichangiwa na kukua kwa sekta ya ufuaji umeme, kuimarika kwa huduma za usafirishaji na uhifadhi wa mizigo, sekta ya habari na mawasiliano, ujenzi na uchimbaji wa madini na mawe.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango)

BULEMBO AFUNGA KAZI WILAYA YA MISENYI NA BUKOBA MJINI MKOANI KAGERA

$
0
0
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Alhaj Abdallah Bulembo akiwasili ukumbini kuendesha kikao cha Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Misenyi, Mabalozi, viongozi wa Jumuia za CCM na watendaji wa Serikali katika Wilaya hiyo mkoani Kagera, leo
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwaili ukumbini
                         Wajumbe wakiwa ukumbini tayari kumsikiliza Alhaj Bulembo
Katibu wa Jumuia ya Wazazi Tanzana, Wilaya ya Misenyi Rehema Mtawala akimkabidhi zawadi maalum Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo kabla ya kikao kuanza
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo akionyesha zawadi hiyo maalum baada ya kukabidhiwa. Zawadi hiyo ina maneno ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Mbunge.
 Mwenyekiti wa CCM wa CCM Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, Haji Seruhu akifungua kikao hicho
 Katibu wa CCM Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera Mwajuma Mboha, akieleza maneno ya utangulizi katika kikao hicho

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akifurahia jambo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Misenyi Haji Seruhu, wakati wanapita taarifa iliyosomwa na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo
 Wajumbe wakihamasika kwenye kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wajumbe wakati wa kikao hicho
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akitulia kumsikiliza kwa makini mshairi Mansur Athan wakati akighani shairi mwishoni mwa kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akipokea zawadi ya Mbuzi aliyopewa na Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Misenyi wakati wa kikao hicho leo.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera Yahya Kateme (kushoto) akibadilishana mawazo na Vijana wa wa CCM nje ya ukumbi baada ya kikao
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Ajhaj Abdallah Bulembo akiendelea kuwasikiliza nje ya ukumbi badhi ya wadau waliotaka ufafanuzi wa baadhi ya mambo baada ya kikao hicho
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM akiwafafanulia jambo nje ya ukumbi baadhi ya wadau
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj abdallah Bulembo akiendelea kuwasikiliza wadau hata baada ya kupanda gari lake tayari kwa kuondoka

Baada ya wadau kuridhika wakamuaga kwa furaha na kumtakia safari njema kwenda Wilaya ya Bukoba mjini
 Safari ya Alhaj Bulembo kutoka Misenyi kwenda Wilaya ya Bukoba mjini ilipitia kwenye daraja hili la Mto Kagera, eneo la Kyaka.
 Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera Yahya Kateme akizungumza na vijana waendesha bodaboda aliowakuta Bukoba Mjini, baada ya msafara wa Alhaj Abdallah Bulembo kuwasili
 Mwenyekiti huyo wa UVCCM akapiga picha ya pamoja na vijana wa green Guard wa Bukoba mjini
 Baada ya kuwasili tu Bukoba Mjini, Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo alieanda ofisini kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu na kuwa na mazungumzo naye kwa muda. Pichani, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo hayo. Wengine kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Lahel Ndegeleki na Mwenyekiti wa CCM mkoa huo Costansia Buhiye
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akimweleza jambo Mkuu huyo wa mkoa kabla ya kuondoka
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiwasalimia vijana wa green Guard nje ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akimwelekeza jambo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba mjini Yusuf Ngaiza wakati wa kikao cha Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya hiyo, Mabalozi, viongozi wa Jumuiya na Watendaji wa serikali, leo
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini mkoani Kagera Yusuf Ngaiza akifungua kikao hicho
                                                       Wajumbe wakiwa ukumbini katika kikao hicho
Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wajumbe wakati wa kikao hicho Bukoba mjini mkoani Kagera, leo. PICHA; BASHIR NKOROMO

AZAM TV WAINGIA MKATABA WA KUONYESHA MSIMU MPYA WA NDONDO CUP

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando akikabidhiana mkataba wa makubaliano ya urushwaji wa matangazo wa michuano ya Ndondo Cup na Mratibu Shafii Dauda ukishuhudiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam Almas Kisongo.                        

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

ILE michuano ya Ndondo Cup inatarajiwa kuanza kwa hatua ya makundi huku kituo cha kurushia matangazo ya Luninga ya Azam Tv wakidhamini kwa mara nyingine tena.

Utiaji wa saini wa mkataba wa kuonyesha michuano hiyo umetiwa leo baina ya Mratibu na Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media wakishuhudiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam Almas Kasongo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando amesema kuwa wanaipongeza Clouds Media kama w
aandaaji na waratibu wa michuano hiyo ya Ndondo Cup kwani imeweza kuwa na hamasa kubwa kwa vijana ambao wanapenda mpira na pia wanatumia kama fursa ya ajira.

Mhando amesema, wanaonyesha michuano hiyo kwa mara ya nne ikiwa mara ya kwanza walianza kwa kuonyesha hatua ya nusu fainali ila kuanzia msimu wa 2016 wameanzia hatua ya makundi.

Akizungumza kabla ya uwekaji wa saini wa mkataba huo, Mratibu wa michuano ya Ndondo Cup Shafii Dauda amesema kuwa huu ni mwaka wa nne toka kuanza kwa michuano hiyo na kampuni ya Azam Media wameweza kuionyesha na mwaka huu wameingia tena mkataba.

Dauda amesema, anawashukuru sana Azam Media kwa hatua hii kubwa ya kuonyesha tena michuano hiyo na wanaamini kuwa itazidi kuhamasisha kujiajiri kwa kucheza mpira wa miguu kwani kwa sasa inaonekana Afrika Mashariki na Kati.

Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguh Mkos wa Dar es salaam, Almas Kasongo amewapongeza Clouds Media na Azam media kwa hatu kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wadau na wapenzi wa Mpira wanaendelea kupata burudani.

Droo ya hatua ya Makundi itafanyika kesho katika fukwe za Escape One majira ya saa 8 mchana na kuweza kuzifahamu timu 32 zitakazoumana kumpata bingwa mpya wa michuano ya Ndondo Cup.
Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando wakiweka saini mkataba wa makubaliano ya urushwaji wa matangazo wa michuano ya Ndondo Cup na Mratibu Shafii Dauda ukishuhudiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam Almas Kisongo.                        

Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Tido Mhando akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mkataba wa makubaliano ya urushwaji wa matangazo wa michuano ya Ndondo Cup kushoto ni  Mratibu Shafii Dauda na kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam Almas Kisongo



MSUVA AAHIDI USHINDI DHIDI YA LESOTHO JUMAMOSI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Winga wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Simon Msuva amesema kuwa wanaamini watapata ushindi katika mchezo wao wa kufuzu kombe la Mataifa Afrika mwaka 2019 yatakayofanyika nchini Cameroon.

Taifa Stars inamenyana na timu ya taifa ya Lesotho mechi itakayopigwa siku ya Jumamosi majira ya saa 2 usiku kwenye Uwanja wa Chamazi.

Timu hiyo iliyoweka kambi ya wiki moja nchini Misri imerejea jana majira ya saa 6 mchana kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo.

Akizungumza na globu hii, Msuva amesema kuwa wao kama wachezaji wamefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya mchezo huo siku ya Jumamosi na cha zaidi nawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi.

Msuva amesema kuwa, mechi hiyi ni muhimu sana ili kuweza kuweka matumaini ya kuingia fainali za Mataifa Afrika na watakachokifanya ni kuhakikisha wanapata ushindi.

"Tumejipanga kuhakikisha tunashinda katika mchezo wetu dhidi ya Lesotho ili malengo yetu yaweze kutimia na kuingia fainali za mataifa Afrika," amesema Msuva.

Winga huyo amesema kambi ya nchini Misri imeweza kuwajenga kiushindani na hata ukiangalia mazingira ya kule na hali ya hewa hakuna tofauti.

Stars inakabiliwa na mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya Lesotho utakaofanyika siku ya Jumamosi katika dimba la Uwanja wa Chamazi.
Viewing all 39280 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>