Quantcast
Channel: MTAA KWA MTAA BLOG
Viewing all 39183 articles
Browse latest View live

WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO WASAINI MKATABA WA MKOPO WENYE RIBA ZIRO

$
0
0




Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
WIZARA ya Fedha na mipango kwa niaba ya serikali imesaini mkataba Mkopo wa fedha kati ya serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na benki kuu ya dunia jijini Dar es salaam leo kwaajili ya kusafirisha, kuzalisha na kusambaza nishati ya umeme na maji.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wizara ya fedha na Mipango, Dotto James amesema kuwa mkataba huu wa mkopo huu utahusisha usambazaji wa maji katika maeneo ya vijijini katika mikoa 17 ya Tanzania pamoja na umeme. Pia Katibu Mkuu wizara ya fedha na mipango amewashukuru benki ya dunia kwa kutoa mkopo usio na riba kabisa.

Mkopo huo kutoka Benki ya dunia kiasi cha shilingi trilioni 1.04 ambapo itatumika katika mradi wa umeme na maji kwa mikoa ya kusini ambayo ni  Iringa Kisada,Tunduma, Mbeya hadi mpaka wa Zambia.

Nae Katibu Mkuu wizara ya Maji safi na maji taka, Kitila Mkumbo amesema kuwa fedha hizo zitatumika kikamilifu katika lengo lililopangwa na serikali kwa mikoa 17 katika usambazaji wa maji maeneo ya vijijini.

Kwa upande wa Katibu Mtendaji uwekezaji wizara ya Nishati na Madini, Khalid James amesema kuwa kwa upande wa Nishati ya umeme wataweza kuunganisha gridi ya Taifa kwa mikoa ambayo haijafikiwa na gridi ya taifa.
Katibu Mkuu wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Septemba 7,2018 kabla ya kusaini Mkataba wa mkopo wa fedha kwaajili ya usambazaji wa maji vijijini na uboreshaji, utengenezaji na kuzalisha umeme hapa nchini.
 Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Septemba7, 2018 kabla ya kusaini Mkataba wa Mkopo wenye masharti nafuu pamoja na riba zero ambapo mkopo huo utakuwa kwaajili ya kutekeleza mradi wa maji vijijini pamoja na umeme.
 Katibu Mkuu wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (Kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird (Kushoto) wakisaini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu na wenye riba ziro kwaajili ya uboreshaji na utengenezaji mifumo ya umeme na maji katika maeneo ya vijijini hapa nchi.
  Katibu Mkuu wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (Kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird (Kushoto) wakibadilishana Mkataba wa mkopo jijini Dar es Salaam leo, Septemba 7,2018 wenye masharti nafuu na wenye riba ziro kwaajili ya uboreshaji na utengenezaji mifumo ya umeme na maji katika maeneo ya vijijini hapa nchi.
 Katibu Mkuu wa wizara ya maji safi na maji taka (DAWASO), Kitila Mkumbo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu mpango waliojiwekea katika kuboresha na kusambaza maji hapa nchini katika maeneo ya vijijini. Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird.
Kaimu Mkurugezi mtendaji- Uwekezaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Khalid James kulia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya katibu Mkuu wizara ya fedha na Mipango kusaini mkataba wa Mkopo wa fedha kwaajili ya uboreshaji na usambazaji wa maji pamoja na umeme.

TAKUKURU BAGAMOYO YATOA ELIMU KWA MADIWANI NA WATENDAJI KUHUSU MAADILI NA RUSHWA

$
0
0
 Mtaalamu wa masuala ya Jinsia, Bajeti kwa Mtazamo wa kijinsia na Haki za Binadamu, Ndg. Gemma Akilimali (aliesimama) akitoa mada kwa Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti katika semina iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti wakifuatilia mada iliyowasilishwa na Mtaalamu wa masuala ya Jinsia, Bajeti kwa Mtazamo wa kijinsia na Haki za Binadamu, Ndg. Gemma Akilimali (aliesimama) wakati wa semina iliyohusu Bajeti kwa Mtazamo wa Kijinsia leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. George Simbachawene (kushoto) akizungumza jambo wakati kamati hiyo ikipatiwa semina iliyohusu Bajeti kwa Mtazamo wa Kijinsia, leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Husna Mwilima. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

KAMBI YA TIMU YA YAIFA YA SOKA LA UFUKWENI KUVUNJWA JUMAPILI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya soka ya ufukweni (Beach Soccer) Boniface Pawasa amesema kuwa kwa sasa anavunja kambi rasmi siku ya Jumapili kwa ajili ya wachezaji kurudi nyumbani baada ya wapinzani wao Afrika Kusini kujiondoa kwenye mechi ya kuwania nafasi ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON  Nchini Misri.

Akizungumza leo, Pasawa amesema kuwa kambi waliyokuwa wameweka na wakiendelea na mazoezi kwenye Fukwe za Coco Beach ilikua ni kwa ajili ya kujiandaa na mchezo ho na Afrika Kusini ambapo wamejitoa tayari.

"Lengo letu la kwanza ilikuwa ni mechi dhidi ya Afrika Kusini lakini wamejitoa tayari ambao ulikua  ni mchezo wa kufuzu kwenda Mataifa Afrika (AFCON) na tutawalipa wachezaji wote stahiki zao ili warejee majumbanu," amesema Pawasa.

Amesema, katika maandalizi yajayo kwa ajili ya michuano ya  kuwa wameshatuma maombi kwa  timu ya Taifa ya Oman  kwa Kocha Talib Hilal  kwa ajili ya kuweza kupata kambi ya wiki mbili kabla ya kwenda nchini Misri kuchuana katika michuano hiyo ya AFCON.

"Wenzetu Oman ni wazoefu wameweza kucheza hata mashindano ya dunia kwahiyo kupata nafas ya wiki mbili nchini mwao itakuwa ni nafasi nzuri sana kwetu kwa maandalizi ya AFCON, ukiangalia Oman na Misri sio mbali,"amesema.

Pawasa amesema kuwa mpaka sasa ameshaomba mechi za kirafiki kwa timu ya Malawi na Uganda kwa ajili ya kupata mchezo wa kirafiki kujiandaa na michuano ya AFCON miezi mitatu ijayo.

kIkosi cha timu ya Taifa ya soka la Ufukweni wakiwa katika picha ya pamoja.

micAmeeleza kuwa  mbali na hilo atakuwa na programu ya kuweza kuwapata wachezaji wengi wa mchezo huo mwezi Oktoba mwaka huu na kuwataka wachezaji wa mpira wa miguu kuja kutafuta fursa baada ya kushindwa kuoata nafasi kwenye timu ya taifa ya mpira wa miguu.

Mbali na hilo, Pawasa amewaomba watanzania waweze kujitokeza kuisaidia timu ya taifa ya soka la ufukweni kwani ni timu inayowakilisha nchi na sio klabu, wasiwaachie majukumu yote Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kwani imechukua miaka takribani 30 kuweza kufuzu kwenda Michuano ya AFCON na malengo yakiwa ni kuhakisha wanapata nafasi ya kwenda Kombe la Dunia nchini Paraguay.



Timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni ya Tanzania imefuzu kucheza Fainali za Africa zitakazofanyika nchini Misri. 
 baada ya mpinzani wake Afrika Kusini kuwasilisha barua ya kujiondoa katika mashindano.  


Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) tayari wametuma barua hiyo ya kufuzu kucheza Fainali hizo za Afrika zitakaofanyika Misri mwaka huu kuanzia Desemba 9-Desemba 14,2018 na kushirikisha nchi Nane.

Timu ya  Soka la Ufukweni ilikuwa kambini kujiandaa na mchezo huo uliokuwa uchezwe Jumapili Septemba 9,2018 na kambi hiyo itavunjwa rasmi Jumapili.
Wachezaji wa timu ya taifa ya Soka la Ufukweni wakiwa katika mazoezi Fukwe za Coco Beach.

Viwanja vya ndege vyaaswa kuweka mikakati ya kukabiliana na magonjwa kuambikiza-TCAA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Usafiri wa Anga (TCAA)  imesema kuwa viwanja vya ndege na wadau wengine katika usafiri wa anga wanatakiwa kuwa na mikakati ya kukubiliana na magonjwa ya kuambukiza ili kufanya usafiri wa anga kuwa salama kwa abiria pamoja na mizigo.

Akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa usafiri wa anga uliofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka hiyo  , Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamalaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Redemptus Bugomomola amesema viwanja vya ndege vinatakiwa kuwa na huduma za Afya kwa ajili ya kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza ili kuweza kulinda jamii kutoka sehemu kwenda nyingine.

Bugomola amesema kuwa baada ya kuwepo magonjwa ya kuambukiza kwa watumiaji usafiri wa anga Shirika la Usafiri wa Anga (ICAO) liliunda chombo cha kuratibu masuala kukabiliana na magonjwa ya  kuambukiza katika Viwanja vya Ndege CAPSCA  ambapo nchi za Afrika bado ziko nyuma katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza.

Amesema kuwa TCAA kwa kushirikiana na wadau kunahitajika kuwepo na mikakati ya kila mmoja kutambua umuhimu wa kufanya kazi katika kukabiliana magonjwa ya kuambukiza kutoka ndani au kwenda nje pamoja na wa nje kuangalia wasiweze kuambikiza wanapingia nchini.

Nae Mkuu wa Vituo vya Afya Mipakani wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Remidius Kakula amesema kuwa kupitia ICAO  imeweka viwango vya viwanja vya ndege kuwa mazingira ya kuweza kukabiliana na maginjwa ya kuambikiza.

Amesema kuwa kila kiwanja cha ndege kinatakiwa kuwa na chumba maalumu pale anapobainika kuwepo kwa mgonjwa ili kuweza kupata huduma haraka ndani ya  uwanja ndege ikiwemo na huduma ya Thermo ya kupima kiwango cha joto pamoja na kuwa gari ya wagonjwa kwa kila kiwanja cha ndege..

Amesema katika mkutano huo watajadiliana mbinu mpya ya kukabiliana magojwa ya kuambukiza kwa magonjwa yaliyotishio kama vile Ebola , Homa ya Ini, Mafua ya Nguruwe pamoja na Mafua ya Ndege.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Redemtus Bugomola akizungumza katika mkutano wa wadau wa anga kuhusiana na kukabiliana na magonjwa ya mlipuko katika viwanja vya ndege uliofanyika katika ukumbi wa TCAA, jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti Uchumi Daniel Malanga akizungumza kuhusiana na masuala mbalimbali ya kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza katika viwanja vya ndege.
Baadhi ya wadau wa usafiri wa anga katika mkutano wa kujadilia namna ya kukabiliana na magonjwa kuambukiza

WANAFUNZI WATATU WA IFM WAPATA UFADHILI WA ADA YA MWAKA WA TATU

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Wanafunzi watatu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamepata ufadhili kusoma mwaka wa tatu kwa kulipiwa ada kupitia kampuni ya Bima ya Metropolitan.

Akizungumza wakati wa kupokea hundi ya sh.milioni 4.5 Makamu Mkuu wa Chuo hicho Dkt. Immanuel Muzava amesema kuwa kampuni ya Bima ya Metropolitan kupitia Chama cha Mawakala wa Bima (TIBA) kimefanya jambo la kuigwa katika umuhimu wa kusaidia wanafunzi ambao wana uhitaji wa kuweza kuhitimu masomo yao.

Muzava amesema kuwa sekta ya Bima inakua kwa kasi nchini hivyo lazima kuwepo na watalaam wa kutosha.

Wanafunzi waliopata ufadhili huo Paschalina Msofe,Rhoda Maholy pamoja na Leonard Mahimbo.

Amesema wanafunzi hao walikuwa na changamoto ya kiuchumi ambayo ingewafanya wakwame kuhitimu mwaka wa tatu.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Metropolitan Suresh Kumar amesema kuwa wanajibu wa kufanya hivyo bila kulazimishwa.

Amesema kuwa watu wakipewa elimu kunaongeza tija kwa serikali katika kuwa na watalaam wataosaidia maendeleo ya uchumi.

Aidha amesema waliofadhiliwa sio wakihitimu wakafanye kazi katika kampuni hiyo bali watafanya sehemu yeyote ikiwa nia kutoa huduma ya bima katika maendeleo ya nchi.

Mmoja wa wanafunzi waliofadhiliwa Paschalina Msofe amesema kuwa kazi yao ni kusoma bidii na kutoa matokeo mazuri kwa kile walichosome katika utoaji wa huduma ya bima nchini.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Metropolitan Suresh Kumar akizungumza wakati wa kupokea hundi ya wanafunzi waliofadhiliwa katika chuo hicho.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Metropolitan Suresh Kumar akizungumza kuhusiana na kampuni hiyo kufadhili ada kwa wanafunzi.
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Immanuel Muzava  akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Metropolitan Suresh Kumar kwa ajili ya ada kwa wanafunzi kwa ada ya mwaka wa tatu.
 Mwanafunzi wa IFM Rhoda Maholy akitoa shukurani kwa niaba wanafunzi wenzake kuhusiana msaada kusoma mwaka wa tatu kwa ufadhili.
Wanafunzi wa IFM wakiwa na hundi ya mfano wa ada ya iliyotolewa na Kampuni ya Bima ya Metropolitan.

PROF KITILA MKUMBO AKUTANA NA MENEJIMENTI MPYA YA DAWASA LEO JIJINI DAR.

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KATIBU Mkuu wa  Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo amezindua Menejimenti mpya ya  Mamlaka ya Maji Taka na Maji Safi (DAWASA) na kuwaomba wadau wa maji nchini kushiriki katika utoaji wa maoni kuhusiana na utungaji wa sheria mpya ya maji

Amezungumza hayo katika Ofisi za Dawasa jijini Dar Es Salaam na kuongeza kuwa sheria hii mpya itasaidia Mambo mengi ikiwa ni pamoja na udhibiti wa maji ambayo yamekuwa yakipotea kwa asilimia 44 mpaka sasa

Prof Mkumbo amesema wizara inapendekeza kuanzishwa kwa Taasisi maalumu  ya kushughulikia miradi ya maji mijini na vijijini yaani Rural Water Agency, Taasisi ambayo imekisudia kuimarisha Jumuia za watumiaji wa maji kwa ngazi za vijiji na miji ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa Taasisi mpya ya Dawasa

Kutunga kwa sheria hii mpya ya maji kutaongeza matamanio kwa watumiaji wa maji na kuhakikisha kila Mtanzania anapata maji safi kwa uhakika   

Wakizungumza kwa niaba ya DAWASA Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja amewataka wananchi wa Dar Es Salaam na Pwani kishirikiana na Dawasa katika ufanyaji kazi wake hasa kutoa taarifa punde inapobainika uvujaji wa maji, na kusisitiza kuhusu utungaji wa sheria mpya unapofanyika wananchi watoe maoni ili mchakato uwe na tija kwani sheria hii ina manufaa makubwa kwa wananchi.
Katibu Mkuu wa  Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Menejiment mpya ya Mamlaka ya Maji Taka na Maji Safi (DAWASA) inayoongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja (kulia) leo baada ya kukutana nao ofizi za DAWASA Jijini Dar es Salaam.

PPRA yawapa wahandisi ufafanuzi fursa ya ununuzi kwa njia ya mtandao

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), imeendelea kuwapa wadau wake elimu na ufafanuzi kuhusu fursa na faida za kutumia mfumo wa ununuzi wa njia ya mtandao (TANePS).
Mamlaka hiyo imetumia fursa ya maonesho ya mkutano wa 16 wa mwaka wa Wahandisi yaliyoandaliwa na Bodi ya Wahandisi nchini (ERB), yaliyofanyika Septemba 5 hadi 7 jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, PPRA ilikuwa inapokea maoni na kujibu maswali mbalimbali yaliyohusu mfumo wa ununzi kwa njia ya mtandao (TANePS) pamoja na masuala yanayohusu marekebisho ya sheria ya manunuzi ya umma yaliyofanyika mwaka 2016.
Katika maboresho ya sheria ya ununuzi wa umma, wahandisi walijikita zaidi katika marekebisho ya kanununi Na. 55A, 55B, 55C NA 55D, kama walivyoelezwa na mgeni Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi kuwa kupitia maboresho ya sheria ni vyema wakachangamkia fursa za miradi ya serikali kuliko kulalamika kila wakati kuwa wanakosa miradi hiyo na kupewa kampuni za nje ya nchi.
Akizungumziaa kuhusu mfumo wa ununuzi wa umma (TANePS), Mhandisi Mwanahamisi Ally wa kampuni ya Classic Plan alisema kuwa baada ya kujiunga na TANePS anaona mwanga wa kupungua kwa mianya ya rushwa na urasimu katika michakato ya manunuzi ya umma, hivyo akawaomba PPRA waendelee kutoa elimu zaidi kwa wahandisi na wazabuni kwa ujumla ili wasipitwe na fursa hiyo muhimu.
“Leo nimepata ufafanuzi zaidi zaidi kuhusu maeneo ambayo nilikuwa na maswali  zaidi baada ya kujisajili na kupata mafunzo ya kuutumia mfumo huu wiki kadhaa zilizopita,” alisema.
Aliongeza kuwa baada ya kupata ufafanuzi, alitaka kufahamu ni lini fursa za zabuni zitaanza kutangazwa kwa njia hiyo ili aanze ‘kuchangamkia’ fursa hiyo muhimu isiyo na urasimu na inayohuisha uwazi.
Akitoa ufafanuzi kuhusu swali hilo, Afisa Tehama wa PPRA, Giftness David alisema kuwa kwa sasa baadhi ya taasisi zimeshawasilisha mpango wa manunuzi kwa njia ya TANePS, na kwamba kwa ujumla takribani wazabuni 1000 wamekwisha jiandikisha kwenye mfumo huo, hali inayoashiria utayari zaidi.
Aidha, Mhandisi Tumaini Msaki aliungana na idadi nyingine ya wahandisi kuuliza maswali ya sheria ya manunuzi ya umma, hususan kuhusu marekebisho ya sheria na kanuni ya mwaka 2016.
“Mimi nilitaka kufahamu ni kwa kiasi gani wahandisi wa ndani wanapewa nafasi ya kufanya kazi na Serikali kupitia zabuni mbalimbali ambazo makampuni ya nje yanakuwa yanashindania pia kwa kuwa wenzetu wana nguvu zaidi ya kifedha na mitambo,” alisema Mhandisi.
Aliongeza kuwa alijibiwa na kuoneshwa jinsi ambavyo sheria inatoa nafasi ya upendeleo kwa wazabuni wa ndani wanapokuwa wanashiriki zabuni zinazohusisha makampuni ya nje pia. Alisema kuwa sheria hiyo inatoa hadi upendeleo wa asilimia 10 kwa wazabuni wa ndani katika hali hiyo.
TANePS, ni mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao unaoratibiwa na PPRA kwa kushirikiana na taasisi za Serikali ambao ni wadau wa manunuzi. Mfumo huu ulizinduliwa rasmi Juni mwaka huu na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa. 
 Afisa Tehama wa PPRA, Giftness David, akijibu maswali ya wahandisi kuhusu TANePS katika maonesho ya mkutano wa 16 wa mwaka wa Wahandisi yaliyoandaliwa na Bodi ya Wahandisi nchini (ERB), yaliyofanyika Septemba 5 hadi 7 jijini Dar es Salaam.
Afisa Uhusiano wa PPRA, Nelson Kessy, na Afisa Tehama, Siganike Baruti wakitoa ufafanuzi kwa wazabuni kutoka kampuni ya Bizcyclone katika maonesho ya mkutano wa 16 wa mwaka wa Wahandisi yaliyoandaliwa na Bodi ya Wahandisi nchini (ERB), yaliyofanyika Septemba 5 hadi 7 jijini Dar es Salaam.

KUIONA SIMBA NA AFC LEOPARDS BUKU TANO TU KESHO UWANJA WA TAIFA.

$
0
0
Afisa habari wa Simba Haji Manara. 

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
TIMU ya Simba inashuka dimbani kucheza mchezo wa kirafiki na AFC Leopards ya Kenya kwa ajili ya kujipima nguvu kabla ya Ligi Kuu Tanzania Bara kuendelea tena wiki ijayo utakaochezwa kesho katika dimba la uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia mchezo huo, Afisa habari wa Simba Haji MAnara amesema katika mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa wa klabu ya Simba na AFC Leopards ya Kenya utakaofanyika Jumamosi kiingilio kitakuwa ni Sh. 5,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Manara ametaja viingilio vingine katika mchezo huo utakaoanza Saa 12:00 jioni vitakuwa Sh. 15,000 kwa jukwaa la VIP A na Sh. 10,000 kwa jukwaa la VIP B na mchezo huo utakuwa ni kwa ajili ya kuwapima wachezaji wake kabla ya kuendelea na mtanange wa ligi kuu.

Amesema mchezo huo utazikutanisha timu hizo baada ya miaka miwili toka wakutane mara ya mwisho kwenye tamasha la Simba Day, Agosti 8 mwaka 2016 Uwanja wa Taifa pia na kufanikiwa kuondoka na ushindi wa golo 4-0.

Mbali na hilo, Manara amewataka mashabiki wa Simba na watanzania wote kwa ujumla kuipa sapoti Taifa Stars ambayo inacheza kesho dhidi ya Uganda kuwania tiketi ya kufuzu kuelekea AFCON 2019.

Manara amesema watanzania kwa ujumla wanatakiwa kuwa wamoja kwa ajili tawashangaa mashabiki baadhi wa Simba ambao wataipa sapoti Uganda kutokana na kuondolewa kwa wachezaji wake 6 kwenye kikosi cha Stars kutokana na kuchelewa kufika kambini akieleza kuwa ni sababu ambayo haina maana.


Manara amewaomba mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa kesho ambapo timu yao itakuwa inacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya AFC Leopards ya Kenya majira ya saa 12 jioni.

Sanjari na kujitokeza Uwanjani, mashabiki hao pia ambao watawahi watapata fursa ya kuutazama mchezo wa Uganda dhidi ya Stars ambao utarushwa mbashara kupitia kituo cha ZBC 2.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAHUTUBIA WANANCHI WA TARIME MKOANI MARA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Tarime mjini mara baada ya kuwasili akitokea katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wanakwaya ya Chuo cha Ualimu Tarime mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutano Tarime mjini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Tarime vijijini wakati akitokea katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.
 Kwaya ya Chuo cha Ualimu Tarime ikitoa burudani mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwasili Tarime mjini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wananchi wa Tarime mjini mara bada ya kuwahutubia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mwanafunzi wa Shule ya Sekondary Ingwe iliyopo Nyamongo Wilayani  Tarime Monica Benard kiasi cha Shilingi milioni tano kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya shule hiyo kutokana na vipaumbele vyao.
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Ingwe ya Nyamongo Tarime mkoani Mara Monica Benard akionesha kiasi cha Shilingi milioni tano alizokabidhiwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa ajili ya maendeleo ya shule yao. Pia Rais Dkt. Magufuli aliendesha Harambee ya papo kwa hapo ambapo zilipatikana jumla ya Shilingi milioni 26 kwa ajili ya maendeleo ya Shule hiyo. PICHA NA IKULU

JKCI yaibuka mshindi wa kwanza katika utoaji wa huduma ya upimaji na kutoa elimu ya magonjwa ya moyo katika mkutano wa wahandisi

$
0
0
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeombwa kuwafikia wananchi wengi zaidi wakiwemo wafanyakazi ili waweze kufanyiwa vipimo vya moyo pamoja na kupata elimu ya jinsi ya kuepukana na ugonjwa huo. Ombi hilo limetolewa leo na washiriki wa mkutano wa mwaka wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Diamond Jubilee uliopo jijini Dar es Salaam.

Wahandishi hao pia wamewashauri wafanyakazi kutenga muda wa kupima afya zao na kufanya mazoezi ambayo yatawasaidia kiafya. Mhandisi Alex Kalanje alisema kama Taasisi hiyo itawafikia watu wengi zaidi kwa kwenda katika mikusanyiko mbalimbali kutawasaidia watanzania wakiwemo wafanyakazi ambao kutokana na majukumu yao ya kazi wanakosa muda wa kwenda kupima afya zao kupata huduma ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo.

“Wafanyakazi wengi wanakosa muda wa kwenda Hospitali kupima afya zao, lakini kama kutakuwa na utaratibu wa kuwepo kwa wataalam wa afya katika mikutano mbalimbali kutawasaidia kupata muda wa kupima kirahisi zaidi kuliko wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi”, alisema Mhandisi Kalanje..

Kwa upande wake Mhandisi Dkt. Gemma Modu aliwashauri watanzania kutenga muda wa kupima afya zao kwa kufanya hivyo kutawasaidia kujuwa kama wanamatatizo au la na kama wanayo wataweza kupata matibabu mapema.

Aidha Dkt. Gema pia aliwasihi kinamama kubadilika na kuhamasisha familia zao kwenda kupima na ikifika muda wa kupima waende wao na waume zao pamoja na watoto.

Akizungumza wakati wa kufungwa kwa mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt. Jim James Yonazi aliipongeza Taasisi ya Moyo kwa huduma ya kijamii iliyoitoa ya upimaji na kutoa elimu ya lishe pamoja na mazoezi na kusema kuwa kazi waliyoifanya ni kubwa.

Taasisi hiyo ilishika nafasi ya kwanza ya mtoa huduma za kitaalam kwa kutoa huduma za upimaji wa vihatarishi vya magonjwa ya Moyo, ushauri wa kiafya kuhusiana na Magonjwa ya Moyo, elimu ya lishe bora na mazoezi, kueleza kwa kina huduma zinazotolewa na Taasisi, kutoa dawa bure kwa watu waliokutwa na matatizo ya moyo na kutoa rufaa ya moja kwa moja kwa wagonjwa waliokutwa na matatizo ya moyo yaliyohitajika kupewa rufaa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea cheti cha nafasi ya kwanza ya mtoa huduma za kitaalam kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Elias Kwandikwa kutokana na Taasisi hiyo kushiriki katika kutoa huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo kwenye mkutano wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dorica Burengelo akimpima ugonjwa wa kisukari mhandisi aliyetembelea banda la hiyo kwa ajili ya kupima afya na kupata elimu ya lishe na mazoezi wakati wa mkutano wa 16 wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophylly Mushi akimpima msukumo wa damu (PB) mhandisi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupima afya na kupata elimu ya lishe na mazoezi wakati wa mkutano wa 16 wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hussein Mube akimpa ushauri wa kiafya mhandisi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupima afya na kupata elimu ya lishe bora na mazoezi wakati wa mkutano wa 16 wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa upimaji afya, utoaji wa elimu ya lishe bora na mazoezi wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi mara baada ya kupokea cheti cha kushika nafasi ya kwanza ya mtoa huduma za kitaalam kwenye mkutano wa wahandisi uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.

KAMPUNI YA KITANZANIA YA NALA YASHINDA TUZO YA ECOBANK FINTECH CHALLENGE

$
0
0
SHINDANO la Ecobank Fintech Challenge lenye lengo la  kuonesha na kushirikiana na  miradi yenye mafanikio zaidi ya Fintech Katika bara zima la Afrika limemalizika huku Tanzania kupitia Kampuni ya Nala kupitia mradi wake wa Nala Money(Nala App) chini ya Mkurugenzi na mwanzilishi Benjamin Fernandes wakiibuka na kuwa washindi,

Shindano hilo limelenga  kusaidia kupitia ushirika wa kibiashara ili kukua na kujitanua kwenda kwenye mafanikio ya kikanda na biashara ya kimataifa.

Mradi wa malipo ujulikanao kama Nala hapa Tanzania umetajwa kuwa mshindi wa mwaka wa shindano hilo la Ecobank Fintech Challenge na kufanikiwa kuibuka na zawadi ya dola za kimarekani 10,000.

Nala inawasaidia watumiaji wa miamala ya simu kujihusisha na nakala za USSD kupitia njia rahisi kama vile Venmo app, iliyotoa ufumbuzi pamoja na miradi (startups) mingine ipatayo 10 katika sherehe za 30 agosti katika makao makuu ya kimataifa ya Ecobank huko Lome Togo.
Nigeria wallet, imekuwa ya pili na kujishindia dola za kimarekani 7,000 wakati Virtual Identity ya Afrika ya Kusini ilikuwa mshindi wa tatu na kupata dola za kimarekani 5,000. Washiriki wengine ni Lypa ya Kenya, Litee ya Benin, SESO Global ya Afrika ya Kusini, InvestED  ya Sierra Leone, Eversend ya Ufaransa, Seca pay ya Nigeria, Moji pay ya Togo na Awamo ya Uganda.

Ecobank itawaandikisha washindi wote 11 katika ushirika wake wa Fintech. Ushirika huu utadumu kwa kipindi ya miezi 6. Katika kipindi hicho miradi hiyo (startups) itanufaika kutoka kwenye fursa hiyo  kwenda kwenye hatua kubwa Zaidi ya ushirika na ecobank group.
Mkuu wa kitenge cha Masoko na Mawasiliano Ecobank Tanzania, Furaha Samalu(kushoto) akimpongeza Mkurugenzi na mwanzilishi wa Kampuni ya  Nala, Benjamin Fernandes baada ya kuibuka mshindi wa Tuzo ya Ecobank Fintech challenge.

PROFESA KITILA MKUMBO AMEWATAKA WADAU WA MAJI KUSHIRIKI KATIKA UTUNGAJI SHERIA MPYAA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KATIBU Mkuu wa  Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof esa Kitila Mkumbo amewataka  wadau wa maji nchini kushiriki katika utoaji wa maoni kuhusiana na utungaji wa sheria mpya ya maji ili kuweza kudhibiti upotevu wa maji.

Amezungumza hayo katika Ofisi za Dawasa jijini Dar Es Salaam na kuongeza kuwa sheria hii mpya itasaidia Mambo mengi ikiwa ni pamoja na udhibiti wa maji ambayo yamekuwa yakipotea kwa asilimia 44 mpaka sasa

Prof Mkumbo amesema wizara inapendekeza kuanzishwa kwa Taasisi maalumu  ya kushughulikia miradi ya maji mijini na vijijini yaani Rural Water Agency, Taasisi ambayo imekusudia kuimarisha Jumuia za watumiaji wa maji kwa ngazi za vijiji na miji ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa Taasisi mpya ya Dawasa

Kutunga kwa sheria hii mpya ya maji kutaongeza matamanio kwa watumiaji wa maji na kuhakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama kwa uhakika  zaidi.

Akizungumza kwa niaba ya DAWASA Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja amewataka wananchi wa Dar Es Salaam na Pwani kushirikiana na Dawasa katika ufanyaji kazi wake hasa kutoa taarifa punde inapobainika uvujaji wa maji, na kusisitiza kuhusu utungaji wa sheria mpya unapofanyika wananchi watoe maoni ili mchakato uwe na tija kwani sheria hii ina manufaa makubwa kwa wananchi.
Katibu Mkuu wa  Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Menejiment mpya ya Mamlaka ya Maji Taka na Maji Safi (DAWASA) inayoongozwa na Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja (kulia) leo baada ya kukutana nao ofizi za DAWASA Jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SIMIYU.SEPTEMBA 8,2018

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali mojawapo ya wgonjwa aliyepumzishwa katika chumba cha mapumziko katika hospitali mpya ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu mara baada ya kuifungua rasmi hospitali hiyo,Bariadi Mkoa wa Simiyu.Septemba 8,2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi mara baada ya kuifungua rasmi hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.Septemba 8,2018.



  Sehemu ya jengo la wagonjwa wa nje (OPD)la hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu lililofunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Bariadi Mkoa wa Simiyu.Septemba 8,2018.
. PICHA NA IKULU

Mavunde aipongeza Kampuni ya Mafuta Puma

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde na Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti wakiwasaidia kuvuka kwenye kivuko wanafunzi wa shule za msingi za Upanga na Maktaba mara baada ya hafla ya kuwakabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la uchoraji wa picha za usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa Dar es salaam.
Trafiki akisikmamisha magari ili kurughusu Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde na Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti wakiwasaidia kuvuka kwenye kivuko wanafunzi wa shule za msingi za Upanga na Maktaba mara baada ya hafla ya kuwakabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la uchoraji wa picha za usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa Dar es salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde na Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti wakipiga picha ya pamoja na wanafunzi na walimu wa shule za msingi za Upanga na Maktaba mara baada ya hafla ya kuwakabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la uchoraji wa picha za usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa Dar es salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde na Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti wakikabidhi mfano wa cheki yenye tahamani ya shilingi milioni tano kwa mwalimu Mkuu wa wa shule ya msingi Upanga Ailika Yahya mara baada ya shule hiyo kuibuka mshindi katika shindano hilo lililoshirikisha wanafunzi wa shule za msingi za Upanga na Maktaba katika shindano la uchoraji wa picha za usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa Dar es salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde akimkabidhi zawadi za mshindi wa kwanza Mwanafunzi wa shule za msingi ya Maktaba Francisco Salvatory kwa mwakilishi wake Elisha Msafiri katika hafla ya kuwakabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la uchoraji wa picha za usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa Dar es salaam kushoto ni mwalimu mkuu wa shule ya Upanga Ailika Yahya.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde na Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti pamoja na majaji wengine wakichambua picha za wanafunzi walioshinda katika shindano hilo.Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde akizungumza katika hafla hiyo kushoto aliyekaa ni Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Upanga wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Mavunde. Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Maktaba wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Mavunde.




NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Antony Mavunde, ameipongeza Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania, kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kujali usalama wa wanafunzi kwa kutoa mafunzo kwa wanafunzi.

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam wakati akifunga mafunzo ya uchoraji kwa wanafunzi wa shule za msingi za mkoa huo.Amesema tangu mwaka 2013, kampuni hiyo ilipoanzisha kampeni ya usalama barabarani ambayo imekuwa na lengo la kupunguza ajali za usalama barabani na sasa mafanikio yanaonekana.

“Tangu ilipozinduliwa kampeni hii tunaona kuna mafanikio na katika awamu ya kwanza ya mafunzo haya wanafunzi 9,152, wamepewa mafunzo usalama barabarani ikiwamo kushiriki katika michoro hongereni sana Puma.
“….na la kufurahisha zaidi ni hatua ya kuzishirikisha na shule za wanafunzi wenye ulemavu ikiwamo ya shule mojawapo ya Mkoani Ruvuma,” amesema Mavunde.

Awali Meneja Mkuu wa Puma Tanzania, Philippe Corsaletti, alisema mafunzo hayo ni mwendelezo wa kuwaelimisha wanafunzi kuhusu usalama barabarani tangu mwaka 2013 ilipozinduliwa kampeni hiyo.“Tangu ilipoanza kampeni hii tumetoa mafunzo kwa wanafunzi wapatao 68,000 katika shule 63 za mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Geita, Kilimanjaro na Ruvuma,” amesema .

Alisema madhumuni ya kuwahusisha wanafunzi wa shule za msingi imetokana na kuamini kwamba mafunzo ya salama barabarani yanatakiwa kutolewa kwa watto wadogo ili waweze kukua wakiwa na uelewa kuhusu usalama barabarani.
“Tumeamua kuweka mkazo katika mafunzo haya kwa wanafunzi tukielewa kuwa wanakabiliwa na hatari nyingi za barabarani. Na kuyafanya mafunzo haya kuwa kipaumbele chetu cha kwanza,” amesema Philippe.

Meneja huyo alisema kuwa kwa mwaka huu wamefundisha wanafunzi 9,152 wa shule za msingi 16 za Mkoa wa Dar es Salaam na Ruvuma pamoja na kuendesha mafunzo hayo kwa shule za walemavu na kuwa kampuni ya kwanza ya mafuta kuendesha mafunzo hayo.

Katika mashindano hayo mshindi wa kwanza aliibuka mwanafunzi Francisco Salvatory wa Shule ya Msingi Upanga ambaye alinyakua kitita cha Sh 500,000 wa pili ni Magreth Andrew wa Shule ya Msingi Maktaba, ambaye alivyakua kitita cha Sh 300,000 na wa tatu ni pia alikuwa mwanafunzi wa shule ya Msingi Upanga ambaye alizwadiwa Sh 150,000 .

NAMA International Conference & Exhibition kuzikutanisha asasi za kiraia

$
0
0
TAASISI ya Kimataifa ya Mikutano na Maonesho, NAMA International Conference and Exhibition - NICX inatarajia kufanya kongamano kubwa ambalo linalenga kuziunganisha asasi za kiraia kufanya kazi kwa ushirikiano zaidi kuongeza tija katika shughuli zao. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari, Mratibu wa NICX kwa mwaka 2018, Bw. Shaban Mlongakweli amesema matarajio katika kongamano la mwaka huu ni pamoja na kuwatambulisha wataalamu kwenye nyanja za asasi za kiraia, elimu na maendeleo ya vijana.
Alisema kongamano la mwaka huu ambalo linatarajia kukusanya zaidi ya vijana 250 kutoka katika taasisi zaidi ya 100 litaitambulisha NAMA kama mbia wa maendeleo ambaye anafadhili na kuwaandaa wataalamu kutumika kwa ufanisi.

"NAMA Foundation ya Malaysia inaamini ufanisi wa asasi za kiraia unatokana na rasilimali zilizopo pamoja na elimu bora. Hivyo kuna wataalamu walioandaliwa kwenye nyanja mbalimbali za kiuongozi wa asasi kwenye maendeleo ya elimu na maendeleo ya vijana...pia NAMA tunaunga mkono juhudi za asasi za kiraia kwa kudhamini miradi mbalimbali za asasi hizo," alisema Bw. Mlongakweli.

Aidha aliongeza kuwa NAMA ina wataalamu wa ushauri, wabobezi wa elimu, wataalamu wa malezi kwa vijana pamoja na wataalamu wa kujitolea hivyo kuzitaka asasi za kiraia kujitokeza kwa wingi na kujadiliana kwa kina namna ya kuwatumia wataalam hao kwa maendeleo na pia kupanga namna bora ya ushirikiano utakaoleta tija kwa asasi hizo na taifa kwa ujumla.

Alibainisha kuwa kongamano hilo litakalofanyika Septemba 15, 2018, Serena Hotel ya jijini Dar es Salaam kwa siku moja kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni. Taasisi ya NAMA inafanya kazi kupitia washirika na kwa nchini Tanzania inajumuisha washirika An-Nahl Trust, Pamoja Foundation, TAMSYA, TAMPRO na UKUEM.

MKUU WA WILAYA YA TEMEKE AUNGANA NA BENKI YA KCB KUFANYA USAFI MBAGALA ZAKHEM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva akishirikiana na wafanyakazi wa Benki wa KCB pamoja na   wafanyabiashara wa eneo la Mbagala Zakhiem wamefanya  usafi kwa pamoja katika eneo hilo ikiwa ni kuweka mazingira safi na salama.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaniva ameiomba Benki ya KCB  kutoa huduma nzuri na bora kwa wakazi wa Mbagala, na ikiwezekana kuwapa punguzo la riba na masharti nafuu katika mikopo ili kuweza kupata wateja wengi zaidi.


Ameyasema hayo mapema wakati akifungua zoezi la usafi katika wilaya hiyo lililofanywa na benki ya KCB maeneo ya Mbagala Zakhiem, na kuwaomba watoe mikopo ya riba nafuu katika eneo hilo kwa kuwa lina wafanyabiashara wengi na wadogo wakiwa wanahitaji kupewa nguvu ili waweze kufikia malengo yao.


Lyaniva ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, aliipongeza Benki ya KCB kwa juhudi na kufanikisha kuwaleta wadau mbali mbali pamoja na wananchi wa Mbagala kushiriki katika kufanya usafi. “Mlichokifanikisha leo si kidogo na ninawapongeza lakini pia iwe chachu ya kutaka kufanya zaidi katika jamii yenu, ni mfano mzuri wa kuigwa hata na makampui mengine.” aliongeza DC Lyaniva.

Aliendelea kusema kuwa anafurahia kuona wawekezaji wengi wanaendelea kuwekeza katika wilaya ya Temeke kwani anategemea ubora wa huduma kwa wananchi wake, lakini pia watamsaidia katika shughuli nyingi za kijamii ikiwemo kujenga Madarasa, Zahanati na hata huduma za usafi katika maeneo hayo kwani ndio malengo ya serikali ya awamu ya tano.

Mkuu wa wilaya huyo aliendelea kusisitiza kuwa zoezi la usafi liwe ni endelevu kwani yeye anafanya usafi kila jumaa mosi na sio mpaka iwe jumaa mosi ya mwisho wa mwezi, lakini pia alisema anashukuru kupata wasaidizi kwani alikuwa akipata usumbufu mkubwa hasa katika eneo hilo la Zakiem.


Afisa Mazingira wa Wilaya ya Temeke, Ally Hatibu aliwashukuru wakazi wa Mbagala kwa kuitikia wito wa Benki ya KCB. Alisema ni ishara njema inayoonyesha kwamba wakazi wa hao wanalipa kipaumbele swala la kutunza mazingira.”Ninawasihi kuendeleza kuukuza ushirikiano huu na kufanya shughuli endelevu za kutunza mazingira.” alisema.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa KCB Benki Christina Manyeye alisema kuwa wameamua kufanya zoezi hilo ili kuonyesha ushirikiano kati yao na wafanyabiashara pamoja na wakazi wa maeneo hayo, japo kuwa ukiliangalia zoezi hilo kwa haraka haraka utaliona kama ni dogo lakini kwao lina maana kubwa sana.

Aliendelea kusema kuwa KCB Benki inaendelea kuwawezesha wafanya biashara wadogo wadogo katika maeneo mbalimbali nje na ndani ya nchi, kama leo ilivyotoa zawadi za vitendea kazi kwa wafanyabiashara wa eneo hilo kama miamvuli ya biashara na zawadi nyinginezo.

Hafla hiyo pia ilitoa fursa pekee kwa mama ntilie wanaofanya shughuli zao katika maeneo yanayozunguka Tawi la Benki ya KCB Mbagala, kwa kutoa huduma ya chakula kwa washiriki zaidi ya 100 katika hafla hiyo. “Kutoa fursa hii kwa akina mama hawa ilikuwa na jambo la kusudi na tuliwafuata bayana na kuwaomba kushiriki. Tutaendeleza ushirikiano wa aina hii kwa wajasiriamali wote wanaolizunguka tawi letu hasa wakina mama.’’ Alisema Bi. Christine Manyeye, Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano ya Umma wa Benki ya KCB Tanzania.

Kwa upande wake, Bi. Jamila Dilunga ambaye alikuwa muwakilishi wa mama ntilie waliohudumia hafla hiyo, aliishukuru Benki ya KCB kwa fursa waliotoa kwa wakina mama wa Mbagala. Alisisitiza kwamba hakuna sababu ya Mbagala Zakhem kuwa chafu wakati washapata mdau kama Benki ya KCB anayejali mazingira na usafi wa eneo la biashara yake. Aidha, aliiomba Benki ya KCB kufanya swala la kuhamasisha usafi katika eneo hilo kuwa endelevu.


Na mwisho alipenda kutoa shukrani za dhati wadau waliofanikisha zoezi hilo kwenda mbele wakiwemo, Clouds Media Group, kampuni ya usafi ya West Pro, Creative Company, Pamoja na kampuni ya Proper Media.Benki ya KCB Tanzania, Jumamosi ya tarehe 8 Septemba imefanya shughuli za usafi ikishirikiana na wakazi wa Mbagala katika eneo la Mbagala Zakhem ambapo benki hiyo imefungua tawi lake la 14 nchini hivi karibuni.

Clouds Media Group, Green WastePro Limited, kampuni ya kazoa na kuchakata taka pamoja na The Creative Company, kampuni kutengeneza matangazo ndiyo walikuwa washirika wakuu wa Benki ya KCB Tanzania katika hafla hiyo iliyopokelewa kipekee na wakazi wa Mbagala ambao pia walishiriki. Hafla hiyo pia ilipewa uzito kwa kuwepo kwa ofisi za uongozi za Wilaya ya Temeke ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Afisa Mazingira na Watendaji wa Kata na mitaa.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva  akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya KCB Zuhura Muro(kulia)  wakifanya usafi na pamoja kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama Mbagala Zakhiem Jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa  Benki ya KCB, wafanyabiashara wadogo wadogo, kampuni ya Green Waste wakiendelea na usafi Mbagala Zakhiem kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama.
Meneja Masoko wa KCB Benki Christina Manyeye akitoa zawadi kwa wafanyabiashara walioshirikiana nao katka zoezi la usafi wa mazingira Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam

Ujumbe kutoka kwa Bi. Audrey Azoulay kuhusu Siku ya Kimkataifa ya Kisomo

$
0
0
“Mara baada ya kujifunza kusoma, utakuwa huru siku zote", aliandika Frederick Douglass katika karne ya kumi na tisa, MtumwaMarekani mweusi aliyekuwa huru, bingwa wa sababu za ukomeshaji na mwandishi wa vitabu kadhaa. Wito huu wa ukombozi kupitia kusoma, na zaidi kwa ujumla kwa ujuzi wa msingi - Kisomo na kuhesabu vina wigo wa jumla.

Kisomo ni hatua ya kwanza kuelekea katika uhuru, kua huru kutoka katika vikwazo vya kijamii na kiuchumi. Ni muhimu kwa ajili ya maendeleo kwa kila mmoja na kwa pamoja. Inapunguza umaskini na kuleta usawa, hujenga uthamani, na husaidia kuondoa matatizo ya lishe na afya ya umma.

Tangu nyakati za Frederick Douglass, na hasa katika miongo ya hivi karibuni, maendeleo makubwa yamefanywa katika mikoa yote ya dunia na mamilioni ya wanaume na wanawake wameondolewa kutokana na ujinga na utegemezi kwa njia ya harakati ya msingi ya kusoma na kujifunza na demokrasia ya upatikanaji wa elimu. Hata hivyo, matarajio ya ulimwengu ambayo kila mtu awe na ujuzi wa msingi bado ni bora.

Hivi leo, duniani kote, watoto na vijana zaidi ya milioni 260 hawajasajiliwa shule; watoto sita kati ya kumi na vijana - karibu milioni 617 - hawana ujuzi mdogo katika kusoma na kuhesabu; Vijana milioni 750 na watu wazima bado hawawezi kusoma na kuandika - na kati yao, theluthi mbili ni wanawake. Vikwazo hivi vibaya vya uharibifu husababisha kutengwa kwa jamii na kuendeleza ongezeko la usawa wa kijamii na usawa wa kijinsia.

Changamoto mpya sasa imeongezeka: ulimwengu unaozunguka, ambapo kasi ya ugunduzi wa kiteknolojia inaendelea kuharakisha. Ili kupata nafasi katika jamii, kupata kazi, na kukabiliana na changamoto za kijamii, kiuchumi na mazingira, ujuzi wa jadi na ujuzi wa kuhesabu haitoshi tena; ujuzi mpya, ikiwa ni pamoja na teknolojia ya habari na mawasiliano, unazidi kuwa muhimu.

Kuandaa vijana na watu wazima kwa ajili ya kazi ambazo hazijaanzishwa, ni changamoto. Upatikanaji wa Elimu isiyo na Mwisho, kutumia fursa za aina tofauti za mafunzo, na kufaidika na fursa kubwa za uhamaji imekua muhimu.

Kauli mbiu ya Siku hii ya Kimataifa ya mwaka huu ni "Kisomo na kuendeleza stadi za kazi" yenye kulenga njia hii ya kuendeleza elimu. UNESCO inashiriki kikamilifu katika ufafanuzi wa sera za Kisomona kuhamasisha elimu ya ubunifu. Pia inasaidia aina mbalimbali za ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi kwani ufahamu kamili wa sababu ya elimu inaweza kuwezesha majibu sahihi kwa mahitaji ya dunia ambayo huonekana kuwa yenye mabadiliko kila siku.

Katika Siku hii ya Kimataifa, ninatoa wito kwa wadau wote katika ulimwengu wa elimu, na zaidi, kwa kua ni sababu inayotuhusisha sisi sote, kuhamasisha ili uwezekano wa jamii ya kimataifa ya kujifunza ikawe ya uhalisia zaidi.

QUEEN ELIZABETH ASHINDA TAJI LA MISS TANZANIA 2018

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Kinyang'anyiro cha kumpata mrembo wa Miss Tanzania 2018 limefanyika jana usiku na Mrembo kutoka Kinondoni Queen Elizabeth amefanikiwa kuondoka na taji hilo katika shindano lililofanyika jana usiku kwenye Ukumbi mpya wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Saalaam.

Katika shindano hili, Mshindi wa pili ni Nelly Kazikazi na mshindi wa tatu ni Sandra Giovinazzo.
Baada ya kuibuka na ushind wa taji la Miss Tanzania 2018, Queen Elizabeth ameweka wazi mwanzo mwisho kile kilichopelekea kushinda taji hili la U-Miss kwa walikuwa wanashindana na warembo wengi halafu wazuri.

“Nafurahia kushinda taji hili la Miss Tanzania 2018, najisikia vizuri sana napenda kuwashukuru majaji kwa kuweza kuona nafaa kuiwakilisha nchi nasema asante Tanzania, ukiwa kama mrembo lazima ujiandae kama unavyoona warembo ni wazuri sio kwamba ni wazuri kumuonekano tu hata kichwani pia wako vizuri” Queen alisema

Katika shinda no hilo Queen Elizabeth amewashinda warembo wengine 19 waliokuwa wakiliwinda taji hilo kubwa kabisa nchini katika tasnia ya urembo.


Shindano la Miss Tanzania 2018 liliweza kuhudhuriwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe akiwa moja ya zao la Miss Tanzania 2006 na kuibuka namba mbili Jokate Mwegelo pamoja mbunge wa Segerea Bona Kaluwa.


Waziri Mwakyembe amesema kuwa, mashindano ya mwaka huu yamekuwa na tija kubwa sana kutokana na waandaaji wa mwaka huu chini ya Basila Mwanukuzi  kujipanga na kushirikiana na serikali kuanzia hatua ya mwanzo mpaka kufikia tamati.

Warembo watano waliofanikiwa kuingia tano bora wamepewa ubalozi wa mwaka mmoja na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na  Wakala wa Misitu Nchini (TFS).

 Miss Tanzania 2016 Diana Edward akikabidhi taji kwa mshindi wa Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth baada ya kutangazwa akiwabwaga walimbwende wengine 19. 
Miss Tanzania 2016 Diana Edward akikabidhi taji kwa mshindi wa Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth baada ya kutangazwa akiwabwaga walimbwende wengine 19

 Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth akiwa na washindi wa pili na wa tatu baada ya kuvalishwa rasmi taji la Miss Tanzania usiku wa jana kwenue Ukumbi wa Kimataifa wa Mwl Julius Nyerere Jijini Dar.
 

 

 Majaji wa Miss Tanzania 2018 wakifuatilia kwa makini shindano hilo jana usiku.
 







Walimbwende wa Miss Tanzania 2018 wakipita jukwaani katika mashindano yaliyofanyika usiku wa Jana kwenye ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Mwl Julius Kambarage Nyerere.


 .


PROF KITILA MKUMBO AZINDUA MENEJIMENTI YA DAWASA MPYA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo amezindua menejimenti mpya ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam(DAWASA) itakayokuwa inaongozwa na Afisa Mtendaji Mhandisi Cyprian Luhemeja. 

Akizindua menejimenti hiyo, Profesa Mkumbo amesema kuwa Dawasa mpya inatakiwa kuhakikisha kufika mwaka 2030 wananchi wanapata maji ya kuhakikisha kutokana na ongezeko la watu ambapo Dar es Salaam ni moja ya miji inayokuwa kwa kasi duniani na ifikapo 2030 ongezeko la watu litafikia takribani Milioni 1. 

Akizungumza katika sherehe za kuunganishwa kwa DAWASA na DASAWCO  Profesa Kitila Mkumbo amesema kuunganishwa huko kutaokoa Sh Bilioni 2.9 kila mwaka zilizokuwa zikipotea katika uendeshaji wa Dawasa na Dawasco na kusema


 fedha hizo zitakwenda kusaidia upatikanaji wa huduma ya maji katika Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani. 

“Serikali iliamua kuunganisha Dawasa na Dawasco ili kupunguza matumizi na fedha hizi zitaimarisha miundombinu na kuboresha huduma za maji katika eneo la huduma,” alisema Profesa Mkumbo. 

Profesa Mkumbo amewaonya wafanyakazi wa Dawasa mpya kuacha tabia ya ya dharau, nyodo,kukumbatia matatizo, na kuomba rushwa kwa wateja. 


“Baadhi yenu mmekuwa na nyodo, kikola,rushwa na kuridhika na mafanikio kidogo tabia hizi zikome kuanzia sasa,” alisema Profesa Mkumbo. 

Ametaka Dawasa mpya kujiendesha kama kampuni binafsi inayolipwa na wananchi wa Dar es Salaam na si Idara ya serikali ili kuongeza makusanyo ya fedha. 


“Niwaombe mpunguze upotevu wa maji ambao kwa sasa asilimia 47 ya maji yanayozalishwa na Dawasa yanapotea,” alisema Profesa Mkumbo. 

Aidha alisema serikali imeamua kuwapa Dawasa jengo la ghorofa lililopo Ubungo njiapanda ya kwenda Chuo Kikuu ili walimalizie na kuhamia humo. 

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Cyprian Luhemeja ameahidi kuteteleza baakukamilisha miradi mitatu na kutoa muendelezo wa miradi mingine ndani ya siku 100. 

“Zawadi yetu kwa Rais Dk John Magufuli hadi kufikia Disemba 9, mwaka huu tutakamilisha mradi wa maji wa Chalinze, usambazaji wa maji upande wa Goba tegeta na maeneo mengine yaliyokaribu,” alisema Luhemeja. 

amsemandani ya siku 100 hizo watafunga mita za malipo ya kabla nyingi na kuwahakikishia wanaanza ujenzi wa matenki ya Pugu na kusanifu upya mradi wa visima vya Mpera.  


“Ndani y siku hizo pia tutaongeza mapato kutoka Sh Bilioni tisa hadi kufikia Sh Bilioni 12 na pia tutahakikisha tunapunguza upotevu wa maji,” alisema Luhemeja. 









Mwenyekiti wa Bodi wa Dawasa Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange amesema kuwa watashirikiana na menejimenti mya ya Dawasa na watahakikisha kuweza kufikia malengo yaliyowekwa ya maji kuwafikia wakazi wote wa Jiji la Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo akizungumza na Menejimenti mpya ya Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasa) sambamba na wafanyakazi wa Dawasco na Dawasa wakati wa uzinduzi wa Menejimenti hiyo na kumtambulisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja (kushoto).

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange akizungumza na Menejimenti mpya ya Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasa) sambamba na wafanyakazi wa Dawasco na Dawasa wakati wa uzinduzi wa Menejimenti hiyo na kutambulishwa kwa  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja 
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (Dawasa) Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza na wafanyakazi wa Dawasa na Dawasco baada ya kutambulishwa rasmi kuwa mtendaji mkuu wa Mamlaka hiyo.
 Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo(katikati)  akiwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (Dawasa) Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa pili kushoto),Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili kulia) na menejimenti nzima ya Dawasa.

Wafanyakazi wa Dawasco na Dawasa wakiwa katika uzinduzi wa menejimenti moya ya Dawasa wakifuatilia kwa umakini.

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA ITILIMA NA KISESA MKOANI SIMIYU

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu akiwa njiani kuelekea Wilaya ya Meatu mkoani humo. Picha na Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kisesa mkoani Simiyu wakati akiwa njiani kuelekea Meatu mkoani humo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa mwankoli(hawaonekani pichani) katika jimbo la Kisesa mkoani Simiyu. Picha na IKULU
Viewing all 39183 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>