Quantcast
Channel: MTAA KWA MTAA BLOG
Viewing all 39168 articles
Browse latest View live

DC CHAMWINO AMKARIBISHA OFISA TARAFA ALIYEKUWA MASOMONI CHINA, AMUAHIDI USHIRIKIANO

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
MKUU wa Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma Vumilia Nyamoga amempongeza Ofisa Tarafa wa Itiso Remidius Emmanuel.

Pia amemkaribisha tena  kuendelea na majukumu yake ya kutumikia Taifa ikiwa ni siku chache  tu baada ya kurejea nchini akitokea masomoni nchini China.

"Wilaya ya Chamwino inakutegemea sana na tunatarajia maarifa uliyoyapata yataleta tija zaidi,..Ninakuahidi ushirikiano popote pale utakapohitaji msaada zaidi nitakuunga mkono,"amesema Vumilia

Pia amemtaja Remidius kama Ofisa Tarafa machachali na mchapa kazi na kuwataka Viongozi, watendaji  wa tarafa ya Itiso kumpatia ushirikiano wakati ambo amerejea kwa ajili ya kuwatumikia.

Kwa upande wake Remidius, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa namna ya kipekee kwa shauku ya mapokezi makubwa.

Amesema baada ya  kurejea kutoka masomoni amekuja kukutana na Kufanya mazungumzo na Mkuu wake wa kaziMkuu wa Wilaya.

Amesema amemueleza machache aliyojifunza na kwamba tayari ameanza kazi.

" Ninaahidi kuendelea kutumia uzoefu na maarifa ya kile nilichojifunza nchini China kwa ustawi na maendeleo ya Taifa langu  kupitia Tarafa ya Itiso,"amesema.

Katika hatua nyingine Remidius alimkabidhi Mkuu huyo Kitabu kinachoeleza historia na mifano kutoka baadhi majimbo nchini China  yalivyoweza  kujikwamua na janga la umasikini (The way Forward: Stories of Poverty Reduction in China) 
Amesema kuwa "Kitabu hiki kinaeleza namna ambavyo Taifa la China limeendelea kufanikiwa katika mapambano dhidi ya umaskini, mapambano hayo ndio ambayo hata sisi (Tanzania) tunaendelea nayo.

" Na sasa tunao mwelekeo wa kuufikia Uchumi wa wakati 2025 zote ni juhudi za kuondoa umasikini....naamini hii ni zawadi sahihi kwa mkuu wangu na yeye amefurahia sana, kupitia uzoefu uliomo naamini Chamwino itasonga mbele zaidi,"amesema Remidius

Juni 29 mwaka 2018  Chuo Kikuu cha Kilimo nchini China (China Agricultural University - CAU) kilimtunuku Cheti Maalum akiwa ni mwanafunzi pekee kutoka Afrika  katika chuo hicho kama "Outstanding Graduate "

Ikiwa ni kutambua juhudi zake katika kujituma na mtu mwenye bidii kwa kipindi chote akiwa masomoni.

Remidius  Emmanuel ambaye pia alikuwa ni katibu Mkuu wa Shirikisho la wanafunzi Watanzania nchini China aliweza kutembelea zaidi ya majimbo 15 katika taifa hilo na kujifunza mambo mbalimbali kutoka taifa hilo.

Mapema Julai mwaka 2018  alichaguliwa kushiriki katika kambi maalum ya Vijana nchini China ("Future Leader and  Youth Ambassador, International Social Practice Summer Camp") Julai 16 mpaka Julai 22 Julai,2018.

Ambapo ilihusisha vijana  wapatao 140 (International & Chinese Students) kwa uwakilishi wa vyuo vikuu jijini Beijing, China akiwa mtanzania pekee aliyeshiriki katika kambi hiyo iliyofanyika katika Jimbo la Hebei ( Eneo jipya la Xiongan)

Itakumbukwa  Aprili 1 mwaka  2017, Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jiping (Kupitia Kamati kuu ya Chama cha Kikomunist cha China - CPC ) aliutangaza mji wa Xiongan (katika Jimbo la Hebei) kama eneo jipya " Xiongan New Area".

Mji ambao ifikapo mwaka 2035 utakuwa ndio mji wa kisasa zaidi ya miji ya Shenzhen (Jimbo Guandong) na Pudong (Jimbo la Shanghai) na China kwa ujumla kama Ukanda maalum mpya wa kiuchumi (New Special Economic  Zone).

Wengi wamemtaja kijana huyu kama sehemu ya vijana wachache ambao wanajituma kwelikweli na wenye hulka za uzalendo kwa Taifa.
Ofisa Tarafa wa Itiso, Remidius Emmanuel(kushoto) akifafanua jambo mbele ya Wilaya ya Chamwino, Vumilia Nyamoga kuhusu Kitabu hicho kinachoelezea mapambano ya Umasikini kwa mifano ya baadhi ya maeneo nchini China alipokuwa masomoni nchini humo.

StarTimes yaongeza kasi kupambana na UKIMWI

$
0
0
Kampuni ya StarTimes na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na ugonjwa wa UKIMWI UNAIDS, wamekutana na kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Ushirikiano wao katika kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo. Mkutano huo uliopewa jina la “Thamani ya Taarifa kwa njia za kidigitali katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI” ulihudhuriwa na Makamu Rais wa StarTimes Group Bi. Guo Ziqi, Mke wa Rais wa Malawi Bi. Gertrude Mutharika na Mkurugenzi Mkuu wa UNAIDS Bw. Michel Sidibe.

Katika mkutano huo ambao umefanyika mapema mwanzoni mwa wiki hii jijini Beijing, baadhi ya mambo yaliyoongelewa ni ongezeko la vifo vilivyosababishwa na UKIMWI kwa Vijana hii inatokana na kutofikiwa na taarifa juu ya maambukizi ya VVU/UKIMWI hivyo wanakosa ufahamu juu ya njia sahihi za kujilinda na maambukizi ya ugonjwa huo.
Bw. Michel Sidibe akizungumza katika mkutano huo alisema “Tumejionea mwenendo mzuri katika nchi nyingi lakini changamoto tunayokutana nayo ni kukata tama. Vijana wengi hawana taarifa, hawana ufahamu, hivyo hawajilindi na maambukizi..kwa hiyo taarifa, ufahamu na elimu ni muhimu na ndio maana tunajivunia kufanya kazi na StarTimes katika hili.”
Michel aliongeza, “nataka tu kusema kwamba kupeana taarifa na kueleweshana juu ya UKIMWI ili kuwabadilisha vijana itakuwa ni hatua muhimu sana katika kutokomeza ugonjwa huu”. Pia alisema kwenye nchi nyingi za kiafrika zaidi ya asilimia 70 ya watu wote wana umri wa miaka 35 na hawapati taarifa kuhusu ugonjwa huu. “njia yetu ya kukabiliana nao itabadilisha kila kitu na pengine tutakuwa na kizazi kisicho na maambukizi ya UKIMWI”, aliongeza.
Kwa kupitia teknolojia ya mawasiliano ya intaneti kwenye simu barani Afrika na kwingineko duniani, mawasiliano yatakuwa muhimu zaidi katika mapambano haya.
“Kwa kulitambua hilo, StarTimes tulianzisha huduma ya kupata video za moja kwa moja kwenye simu barani Afrika, StarTimes App ambayo tuliizindua mwezi wa sita, na tayari miezi mitatu baadaye imepakuliwa na watu milioni 8 tunategemea watafikia milioni 15 kufikia mwisho wa mwaka”, aliseama Bi. Guo Ziqi.
Kwa sasa tayari StarTimes wanatoa huduma ya kustream maudhui yanayofahamika kama “Zero Discrimination” ikishirikiana na UNAIDS.
Naye mke wa Rais wa Malawi Bi. Gertrude Mutharika alisema, “Ushirikiano wa StarTimes na UNAIDS katika kupunguza maambukizi ya VVU/UKIMWI umekuja kwa wakati sahihi kabisa ambapo Malawi na Afrika kwa ujumla tupo katika mapambano haya muhimu kwa bara letu”.
Viongozi wa Afrika walikuweko jijini Beijing kuhudhuria kongamano la vyama vya Kisiasa vya Africa na kile cha China FOCAC katika kuimarisha uhusiano wa Afrika na nchi ya China.

TFS IMESABABISHA MACHO YA WASHIRIKI SHINDANO LA MISS TANZANIA 2018 KUYAONA AMBAYO HAWAJAWAHI KUYAONA .

$
0
0
 Washiriki wa Shindano la Miss Tanzania mwaka 2018 wakishangilia baada ya kufika katika Mapango ya Amboni mkoani Tanga.
 Baadhi ya washiriki wa shindano la Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mkoani Tanga.
 Warembo wa Shindano la Miss Tanzania wakiwa katika kibao cha Mapango ya Amboni mkoani Tanga baada ya kufika hapo kwa ajili ya kushuhudia vivutio vya utalii vilivyopo.

 Baadhi ya washiriki wa Miss Tanzania 2018 wakiwa wamenyoosha mikono juu baada ya kufika katika Shamba la Chai lililopo katika hifadhi ya msitu wa asili wa Amani mkoani Tanga 
Washiriki wa Miss Tanzania 2018 wakiwa katika hifadhi ya msitu wa asili wa Amani mkoani Tanga baada ya kutembelea majiko banifu yanayotumiwa na wananchi wa vijiji vinavyozunguka msitu huo uliopo mkoani Tanga.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Miss Tanzania 2018 wakiwa katika moja ya  mlango wa pango la Amboni mkoani Tanga.

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MOJA ya kauli ambayo nimeisikia zaidi ya mara moja ikitamkwa na washiriki wa Shindano la Miss Tanzania mwaka 2018 ni ile inayoonesha kutoa shukrani zao za dhati kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),

Warembo hao walioumbwa na Molla wao wakaumbika hawakuwa na shaka hata kidogo kupaza sauti zao tena kwa madaha na madoido wakisema Tanzania yetu, Misitu yetu, Fahari yetu, Urembo oyeee na kisha wanamalizia kwa kusema hivi TFS oyeeeeee..Nikwambie mapema nilikuwa nawasikia kwa masikio yangu.Ndio maana nakwambia nimewasikia.Niamini.

Unajua kwanini?Iko hivi TFS ambayo ipo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii na kwamba iliamua kuwapeleka warembo hao kwenye Hifadhi ya Mazingira ya Msitu Asili wa Amani iliyopo mkoani Tanga.

Hifadhi hiyo inapatikana katika Wilaya ya Muheza na ipo umbali wa kilometa 35 kutoka Muheza Mjini.Hivyo ni hifadhi ambayo haiko mbali saaana, lakini kwa vivutio vilivyopo kwenye hifadhi hiyo hata ingekuwa mbali kiasi gani ningekushauri ufike ujioonee mwenyewe. Na hivi TFS wanavyojua kutunza hifadhi zetu hadi raha.Nenda Mtanzania mwenzangu ukaone vilivyomo.

Kwa kukumbusha tu ukubwa wa hifadhi hiyo ni hekta 8380 .Ni eneo kubwa na ukweli ni kwamba TFS wameonesha kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha hifadhi hiyo inatunzwa kama ambavyo wamekuwa wakizitunza hifadhi nyingi za misitu ambayo wamepewa jukumu la kuhakikisha inakuwa salama na haiharibiwi.

Safari ya warembo hao kwenda katika hifadhi hiyo ilianza katika Hoteli ya Serene jijini Dar es Salaam.Kama kumbukumbu zangu ziko sawa safari ilianzaa saa 10 alfajiri.Kwa picha ya haraka haraka ni kwamba warembo hao walianza maandalizi ya safari hiyo usiku wa manane.Haikuwa tatizo kwao kuhusu muda wa kuondoka.Shauku yao ilikuwa ni kwenda msitu wa Amani.

Wakiwa kwenye basi kubwa lenye hadhi ya kubeba warembo ambapo miongoni mwao ndimo atapatikana Miss Tanzania mwaka 2018 ifikapo Septemba 8 mwaka huu safari ilianza kwa mwendo ambao hata trafiki akiiona hana sababu ya kupiga tochi kuangalia spidi.Ilikuwa ni ya kawaida sana na lengo ni kutoa nafasi ya warembo hao kuona na vingine watakavyokutana navyo barabarani.

Naomba nieleze kidogo kabla ya kuendelea zaidi. Sababu ya kuandaliwa kwa safari hiyo ni kwamba mkakati wa TFS ni kuhakikisha warembo hao mbali ya kwenda katika hifadhi hiyo na kisha kutumia jukwaa la Miss Tanzania kama sehemu ya kuzitangaza hifadhi zetu nchini.

Naishukuru TFS kwa kutambua nafasi ya warembo hao katika kuutangaza hifadhi zilizopo nchini pamoja na utalii uliopo kwenye hifadhi hizo na ule ambao upo nje ya hifadhi.

Pia naishukuru TFS kwasababu iliona haja ya kuwa na waandishi ambao nao walikuwa miongoni mwa walioambatana na mamisi hao kushuhudia hifadhi hiyo.TFS inaamini waandishi kwa kutumia kalamu zao wataandika maandishi ambayo yatafikisha ujumbe mmoja tu wenye lengo la kuhamasisha watalii wa ndani na nje ya nchi yetu kutembelea vivutio vilivyopo.

Ahsante Mtendaji Mkuu wa TFS Profesa Dos Santos Silayo kwa kufanikisha safari hiyo. Ahsanteni kitengo cha mawasiliano cha TFS kinachosimamiwa na Madame Glory na msaidizi wake Tulizo Kilaga.Ni maofisa makini na wanajua wajibu wao katika eneo la mawasiliano kwa umma.Unauliza kwanini nashukuru sana? Nimefundishwa kushukuru kwa kila jambo jema.

Baada ya kutoa shukrani hizo ngoja niendelee kuelezea.Safari ikawa inaendelea na basi lilipofika Mto Wami tukasimama kidogo na warembo kushuka na kisha kwenda katika eneo la mto huo.

Wakapiga picha kama kawaida yao na baada ya hapo safari ikaendelea mdogo mdogo. Kwa kuwa dhamira ni kuangalia utalii kabla kuingia Hifadhi ya Msitu wa Amani warembo hao wakapata nafasi ya kwenda hoteli ya Tanga Beach.Wakapumzika kwa muda na kisha kwenda kwanza Mapango ya Amboni.

Naomba niseme jambo unapozungumzia mapango ya Amboni maana yake unazungumzia mapango ambayo yamejaa historia ya aina yake na kuvutia kwa kweli.Usijidanganye kwa kusema Tanga hakuna utalii.Utachekwa.

Kuna maeneo mengi ya utalii mkoani Tanga.Ukitaka kujua waulize warembo hao.Wameona kila aina ya vivutio. Hivyo wakiwa katika mapango ya Amboni wakapata nafasi ya kuelezwa mambo mengi na hasa vivutio vya utalii.Hakika eneo hilo limejaa historia kubwa na yenye mvuto ambayo kimsingi inakwenda sambamba na michoro inayoonekana kwa macho.

Mchoro wa Simba ambao upo kwenye mlango wa mapango hayo uliwafanya warembo hao kuonesha mshango.Ujue ukingalia mchoro ule ambao upo kwenye moja ya wa pango unaona kabisa kichwa cha Simba kinatazama ndani. 

Inaelezwa hivi miaka ya zamani.Tena zamani sana eneo hilo lilikuwa ni la bahari na baadae maji yaliposogea  kwenye kina kirefu cha bahari ndipo yakaacha mapango hayo ambayo ndio imejaa michoro.

Ukiwa hapo utaelezwa pia pango la linaloitwa Osare Otanga na pango la Paul Hamisi na kisha utaoneshwa pango dogo kabisa lililopo hapo linajulikana kama pango la jinsia.Ndani ya mapango hayo kwa mujibu wa watoa maelezo wanasema ukiingia ndani kuna njia.

Ukipita njia ya kulia unaenda kutokea Mombasa nchini Kenya na ukipita kushoto unaenda kutokea Stendi ya Mabasi ya Kange huko huko mkoani Tanga. Hata hivyo kwa sasa njia hizo zimezibwa.

Pia kuna michoro ambayo ukiangali inaonesha jengo la Msikiti na Kanisa.Ndani ya mapango hayo kuna michoro ya inayoomunesha Mama Bikira Maria. Pia kuna maandishi ya Koraani.

Wakati maelezo hayo yanatolewa warembo hao walikuwa makini kuhakikisha wanailewa vema. Kilichoawaacha midomo wazi warembo hao ni maelezo kwamba ndani ya mapango kuna eneo la mzimu ambapo watu mbalimbali wanakwenda kufanya maombi na hasa wanaoamini katika kuomba mzimu. Eti ukiwa na shida yako au jambo unalitaka basi ukiomba unafanikiwa.

Kwa kuwa lengo la ziara hiyo ni kujifunza zaidi, hivyo walipata nafasi ya kuuliza maswali kwa waliokuwa wanatoa maelezo kuhusu mapango hayo.Wakajibiwa vizuri.Baada ya kujionea utalii wa ndani katika mapango ya Amboni warembo wakaanza kupiga picha.Nadhan lengo lao lilikuwa ni kuweka kumbukumbu muhimu baada ya kufika hapo.

Hata hivyo kwa kuwa ratiba ilikuwa ni kwenda Hifadhi ya Amani warembo hao wakaanza safari ya kwenda katika hifadhi hiyo.Waliingia hifadhini saa 3:30 usiku.Walipofika moja kwa moja wakaenda kuangalia vinyonga wenye pembe tatu.

Tena unaambiwa kuna aina saba ya vinyonga ndani ya hifadhi hiyo.Ikifika usiku wanaonekana vizuri kuliko mchana.Mbona maajabu mwenzangu! Nashukuru binafsi nimewaona vinyonga na ikitokea nafasi nitakwenda kwa mara nyingine.Wala haichoshi kuwaangalia.

Unajua bwana vinyonga hao tunaelezwa kuwa wanapatikana tu kwenye hifadhi hiyo na si mahali kwingine kokote duniani.Watalii kutoka mataifa mbalimbali duniani wanafunga safari ili kufika hifadhi ya Amani kuona vinyonga.Wewe unasubiri nini?Nenda ukaone.

Utalii ambao warembo hao wameushuhudia ujumbe wao kwa Watanzania  ni kwamba wawe na utamaduni wa kutembelea hifadhi ya Amani yenye utalii wa kila aina.Mbali ya kushuhudia vinyonga hao siku iliyofuata ilipofika saa 12 asubuhi walipata nafasi ya kwenda eneo ambalo ni maalum kwa ajili ya kuangalia jua linavyochomoza.

Ukiwa katika eneo hilo utapata nafasi ya kuona vizuri namna jua linavyochomoza(Sun Rise).Kwa kuwa TFS ilishajipnga kuhakikisha warembo hao wanaona vivutio vya utalii ndani ya hifadhi hiyo iliamua kuwapeleka eneo ambalo lipo juu ya hifadhi na ni maalumu kwa ajili ya kilimo cha Chai.

Safari ya kufika kwenye mashamba hayo nayo ilikuwa ni utalii tosha kabisa.Warembo walipanda kwenye magari ya wazi(Pick Up).Pia kama unavyojua unapanda mlima katika barabara ambayo haina lami zaidi ya udongo wenye tope jingii. Nitoe rai kwa Mtanzania mwenzangu nenda kashuhudie utalii uliopo Amani.

Binafsi nikiri TFS wanajitahidi kutunza misitu ya asili na kubwa zaidi wanatambua umuhimu wa misitu katika maisha binadamu.Ukiwamo wewe na mimi.Hivyo wanaitunza kwa kiwango cha hali ya juu.

Pia ukiwa Amani utapelekwa na eneo ambalo kuna ndege ambao wanapatikana tu ndani ya hifadhi hiyo.Warembo wamepata nafasi ya kuona

Akizungumza na warembo Mhifadhi wa Msitu wa Mazingira Asili wa Aman Mwanaid Kijazi amefafanua kwa kina kuhusu utalii unaopatikana ndani ya hifadhi hiyo ambayo inatunzwa na TFS. 

Akatumia nafasi hiyo kuwaomba warembo hao kuwa mabalozi wa kuutungaza hifadhi hiyo na nyingine zilizopo nchini pamoja na utalii wa kila aina tulio nao nchini kwetu. Pamoja na mambo mengine warembo hao walipata nafasi ya kulala katika eneo hilo la hifadhi .

Kuna nyumba ambazo zilijengwa na Wajerumani miaka ya zamani na ndizo ambazo zinatumika kwa kulala wageni wanaokwenda kulala eneo hilo.Ni nyumba zilizojengwa miaka ya zamani kidogo.

Iinaelezwa baada ya Wajeruman kuingia wilayani Muheza waliamua kwenda Muheza na kutaka kujenga nyuma karibu na makazi ya watu.

Hata hivyo inaelezwa wenyeji walikubaliwa kwa shingo upande.Walipojenga nyumba na kufikia hatua ya kuezeka nyumba upepo mkali ukauzua paa na katika mazingira ya ajabu ajabu.Wajerumani wakaona si sehemu salama kwa kuishi.Ndipo walipoamua kwenda kujenga ndani ya msitu huo na baada ya kuanza kuishi wakaamini eneo hilo ni la Amani.

Hivyo sababu ya kwanini msitu unaitwa Amani ni kwamba imetokana na Wajerumani hao. Inaelezwa ukiondoa msitu huo kujulikana kwa jina la Amani, hakuna kata wala taaarifa inayoitwa hivyo ndani ya eneo hilo.

Kwa upande wa TFS unawahimiza warembo hayo kuchukua jukumu la kuutangaza hifadhi zilizopo nchini pamoja vivutio vya utalii. Meneja Masoko wa TFS Mariam Kobero anasema kazi iliyopo ni kuendelea kuzitangaza hifadhi hizo pamoja na utalii na ndilo jukumu ambalo wamekuwa wakilifanya kila siku.

Inatosha kwa leo.Niliyoyashuhudia mimi ndani ya hifadhi ni mengi.Nikuahidi nitandelea kukuelezea.Kubwa tuombe uzima.

YALIYOJIRI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA SEPTEMBA 6, 2018

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Geogre Mkuchika akieleza umuhimu wa muswaada wa Sheria ya Bodi ya Taaluma ya Walimu Tanzania, 2018. (The Tanzania Teachers Professional Board Act, 2018) wakati wa kupitishwa kwa muswaada huo leo Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Mussa  Sima akieleza mikakati ya Serikali kuhakikisha inatunza mazingira ya ziwa manyara ili kuondoa athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akisisitiza jambo wakati akijibu hoja za wabunge leo Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kupitisha muswaada wa Sheria ya Bodi ya Taaluma ya Walimu Tanzania, 2018. (The Tanzania Teachers Professional Board Act, 2018).
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Jumaa Aweso akisisitiza mikakati ya Serikali kuhakikisha kuwa wananchi wote wanafikiwa na huduma ya maji safi na salama kote nchini.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akisisitiza kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi waliokuwa na akaunti katika iliyokuwa  Benki ya FBME  wanalipwa haki zao kwa mujibu wa sheria na Kanuni za utumishi baada ya Benki hiyo kufungwa.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akieleza hatua zilizochukuliwa na Serikali kuondoa mgogoro kati ya wananchi na Manispaa ya Mtwara Mikindani unaotokana na eneo la Mjimwema na Tangira lililopimwa kwa ubia kati ya Manispaa na Taasisi ya UTT-PID mwaka 2003.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati akisisitiza kuhusu umuhimu wa wananchi kupata huduma bora za maji safi na salama wakati wa kipindi cha maswali na majibu leo Bungeni Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Mussa Zungu akisisitiza jambo wakati wa kupitishwa kwa muswaada wa Sheria ya Bodi ya Taaluma ya Walimu Tanzania, 2018.(The Tanzania Teachers Professional Board Act, 2018) leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima, leo Bungeni Jijini Dodoma.
Sehemu ya wageni waliofika Bungeni  kama wanavyoonekana katika picha. (Picha zote na Frank Mvungi)

CHAMA CHA WABUNGE MARAFIKI WA UTURUKI WAKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA UTURUKI NCHINI TANZANIA, BUNGENI JIJINI DODOMA

$
0
0
 Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Fatma Toufiq (kulia) akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (katikati) kwa lengo la kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto ni Mwandishi Mwandamizi wa Taarifa Rasmi za Bunge, Ndg. Patson Sobha
 Wajumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki wakiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Fatma Toufiq (watatu kushoto) wakimsikiliza Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (wa pili kushoto) wakati wa kikao baina yao kilicholenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma.
 Wajumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki wakiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Fatma Toufiq (katikati) wakiwa katika mazungumzo na  Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (wa pili kushoto) wakati wa kikao baina yao kilicholenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu (kulia) akizungumza na Wanachama wa  Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki walioongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Fatma Toufiq (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kililenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi
Mjumbe wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki na Mbunge wa Chilonwa, Mhe. Joel Mwaka akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu na Wanachama wa Chama cha Wabunge Marafiki wa Uturuki (hayupo kwenye picha) katika kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

RAIS MAGUFULI AZINDUA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI KWENYE MABWAWA NA VIZIMBA KATIKA KAMBI YA JESHI 27KJ MAKOKO-MUSOMA MKOANI MARA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashira uzinduzi rasmi wa Mabwawa 9 na Vizimba vya kufugia samaki aina ya Sato katika Kambi ya Jeshi YA 27 KJ Makoko Mkoani Mara.Wengine ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luaga Mpina,Katibu mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt.Frolence Turuka ,Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima,Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo,Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt.Modestus Kimbilimba.Septemba 6,2018.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi mara baada ya kukata utepe kuashira uzinduzi rasmi wa Mabwawa 9 na Vizimba vya kufugia samaki aina ya Sato katika Kambi ya Jeshi YA 27 KJ Makoko Mkoani Mara.Wengine ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luaga Mpina,Katibu mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt.Frolence Turuka , Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima,Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo,Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt.Modestus Kimbilimba.Septemba 6,2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifunua kitambaa kuashira uzinduzi rasmi wa Mabwawa 9 na Vizimba vya kufugia samaki aina ya Sato katika Kambi ya Jeshi YA 27 KJ Makoko Mkoani Mara.Wengine ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luaga Mpina,Katibu mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt.Frolence Turuka ,Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima,Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo,Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt.Modestus Kimbilimba.Septemba 6,2018.
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima mara baada ya kukata kuzindua rasmi mradi wa ufugaji wa Samaki wa kwenye mabwawa katika kambi ya Jeshi 27KJ Makoko Musoma Mkoani Mara.Septemba 6,2018.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua mradi wa ufugaji wa Samaki wa kwenye mabwawa wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa mradi huo katika kambi ya Jeshi 27KJ Makoko Musoma Mkoani Mara.Septemba 6,2018.

 Askari wa Jeshi la kujenga Taifa wakiwawekea samaki chakula katika Mabwawa ya kufugia samaki hao wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kambi ya Jeshi 27KJ Makoko Musoma Mkoani Mara.Septemba 6,2018.
 Askari wa Jeshi la kujenga Taifa wakiwvua samaki katika Mabwawa ya kufugia samaki hao wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kambi ya Jeshi 27KJ Makoko Musoma Mkoani Mara.Septemba 6,2018. (PICHA NA IKULU)

Madereva wasio na vyeti waaswa kuchangamkia fursa za mafunzo VETA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMANDA wa kikosi cha Usalama Barabarani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Fortunatus Musilimu amewataka madereva nchini kuchangamkia fursa za mafunzo ya udereva bora katika vyuo mbalimbali ikiwemo vyuo vya VETA.

Akizungumza wakati wa mahafali ya mafunzo ya muda mfupi katika Chuo cha VETA Dar es Salaam Kamanda Musilimu alisema zoezi la ukaguzi wa vyeti kwa madereva litafanyika kama ilivyopangwa ambapo baada ya miezi mitano iliyotolewa na Jeshi la Polisi kwa madereva kurudi shuleni na kupata vyeti kumalizika, hakutakuwa na mjadala tena bali hatua stahiki zitachukuliwa.

“Nawakumbusha madereva kuwa mwezi mmoja umeisha katika ile miezi mitano iliyotolewa…. Nawasihi tena kutumia vizuri muda uliobaki wakasome…”Alisema

Alisema vyeti vyote vitatakiwa kuwa na sahihi ya Wakuu wa Usalama Barabarani wa Mikoa ili kuhakikisha hakuna udanganyifu katika upatikanaji wa vyeti hivyo.

Kamanda Musilimu aliwaasa vijana waliohitimu mafunzo katika chuo cha VETA kuhakikisha wanatumia vyema ujuzi walioupata kuanzisha shughuli zao za kujiingizia kipato kulingana na fani walizosoma.

Naye Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA Stella Ndimubenya aliwataka vijana kutumia vyema fursa zinazopatikana katika Halmashauri zao kuwa kuna fungu maalum kwa ajili ya kuwawezesha vijana kufanya shughuli za ujasiriamali wakiwa kwenye vikundi.

Awali, Mkuu wa Chuo hicho Douglas Kipokola alisema chuo chake kwa kushirikiana na chuo cha VETA Kihonda wamejipanga vyema kutoa mafunzo ya udereva bora kwa madereva wote wataohitaji kupata mafunzo hayo.

Alisema hivi karibuni chuo hicho kimeanza kutoa mafunzo kwa madereva wa magari makubwa/malori yanayobeba mizigo na kwamba mtaala wake umeshapitishwa ambapo mafunzo hayo yameanza kutolewa tarehe 3 Septemba mwaka huu huku kukiwa na madereva 30 wanaopata mafunzo kwa wamu ya kwanza.

Kipokola alisema katika mahafali hayo,jumla ya wanafunzi 1125 wamehitimu mafunzo ya muda mfupi na katika fani mbalimbali ikiwepo Udereva, Uendeshaji wa hiteli, uhazili, umeme, compyuta, mapishi, Nywele na urembo na ufundi wa magari.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani , Fortunatus Muslimu akizungumza katika mahafali ya Chuo cha Veta Changombe yaliyofanyika Chuoni hapo Jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA Stella Ndimubenya akizungumza katika mahali ya Chuo cha VETA Changombe kuhusiana na VETA katika uimarishaji katika utoaji wa Mafunzo ya Ufundi Stadi.

Mkuu wa Chuo VETA Chang’ombe Douglas Kipokola akitoa historia ya chuo katika uandaji wa nguvu kazi ya taifa yenye ujuzi.
 Sehemu ya wanafunzi wanaohitimu katika Chuo cha Veta Changombe.


 Picha mbalimbali za matukio katika mahafali ya Chuo cha VETA Chang'ombe.

MAMLAKA HALI YA HEWA YATANGAZA UWEZEKANO WA KUNYESHA MVUA JUU YA WASTANI,WATABIRI MAGONJWA YA MLIPUKO

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),imeeleza uwepo wa uwezekano mkubwa wa kunyesha mvua nyingi za wastani hadi juu ya wastani katika msimu wa mvua za vuli kipindi cha Oktoba Dsemba mwaka huu.

Pamoja utabiri huo TMA pia imetoa  athari na ushauri wa mvua hizo ikiwemo kuwepo kwa hali ya unyevunyevu wa udongo na upatikanaji wa chakula cha samaki vinatarajia kuimarika katika maeneo mengi ya ukanda wa nyanda za juu Kaskazini Mashariki na Pwani ya Kaskazini.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA ,Dkt Agnes Kijazi ametangaza utabiri huo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari.

Amefafanua kwamba  mifumo ya hali ya hewa inayotarajiwa  inaonesha kuwepo kwa mkubwa wa mvua za vuli kuwa za wastani katika maeneo mengi ya nchi.

 Ameongeza mvua za vuli kipindi cha Oktoba hadi Desemba ni mahususi kwa maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

“Mvua za Vuli 2018 zinatarajiwa kuanza mapema katikati ya Septemba na mwanzoni mwa Oktoba 2018 katika maeneo mengi yanayopata misimu miwili ya mvua.

"Ambapo kwa mikoa ya Kagera ,Geita na wilaya ya kibondo mvua inatarajia kunyesha wastani hadi chini ya wastani,”amesema Dk.Kijazi

Wakati katika maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki pamoja na maeneo ya mashariki na kusini mwa ziwa Viktoria inatarajia kunyesha mvua za wastani hadi juu ya wastani.

Ameeleza  mvua zinatarajia kuanza mapema kati ya wiki ya pili na ya tatu ya Septemba mwaka huu katika maeneo ya mkoa wa Mara na kusambaa katika mikoa ya Shinyanga ,Simiyu,Mwanza ,Geita na Kagera ifikapo wiki ya tatu ya Oktoba mwaka huu.

 Pia amesema katika ukanda wa Pwani wa kaskazini katika mikoa ya Dar es Salaam ,Tanga,Pwani ,Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na maeneo ya kaskazini mwa mkoa wa Morogoro mvua zinatarajia kuanza mapema wiki ya nne ya Septemba ambapo itanyesha mvua ya wastani hadi juu ya wastani,”alisema Dk. Kijazi

Akielezea zaidi utabiri huo amesema katika maeneo ya Kilimanjaro,Arusha na Manyara mvua inatarajia kunyesha kati ya wiki ya pili ya Oktoba mwaka huu  na inatarajiwa kunyesha wastani hadi juu ya wastani.

Dk.Kijazi amesema mazao yasiyohitaji maji mengi yanaweza kuathiriwa na hali ya unyevunyevyu wa kupitiliza na maji kutuama.

Pia amesema magonjwa ya wanyama na upotevu  wa samaki kutokana na uharibifu wa miundombinu ya kufugia samaki vinaweza kujitokeza kutokana na mvua za juu ya wastani zinazotarajiwa katika maeneo hayo.

Ameongeza upande wa sekta ya afya  kutakuwa na uhaba wa maji salama kwa shughuli za binadamu ikiwemo usafi katika maeneo yanayotarajia kupata mvua za chini ya wastani  huku milipuko ya magonjwa inaweza kujitokeza.

Hivyo amesema menejimenti za maafa zinashauriwa kuandaa mkakati wa kupunguza athari zinazoweza kujitokeza katika msimu wa mvua za vuli .

"Hivyo zinapaswa kuandaa mbinu za kukabiliana na mafuriko pamoja na majanga yatokanayo na mafuriko," amesema.

Pamoja na mambo mengine amewaomba wananchi kuchukua tahadhari iwapo mvua zitanyesha juu ya wastani.

DC SOPHIA MFAUME AHIMIZA WADAU WA MAENDELEO KUWEKEZA WILAYANI NAMTUMBO

$
0
0
Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sofia Mfaume amesema kuna kila sababu ya sekta binafsi na sekta za umma kushirikiana kuhakikisha Wilaya hiyo na Taifa kwa ujumla inapiga hatua kimaendeleo.

Amesema sekta hizo zikishirikiana katika kutatua changamoto zilizopo katika baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Namtumbo wananchi watapiga hatua kubwa kimaendeleo huku akiomba sekta binafsi kuwekeza ndani ya wilaya hiyo.

Mfaume amesema hayo leo wakati wa mkutano kati ya sekta binafsi na sekta za umma wilayani Namtumbo.

Amesema lengo la mkutano huo ni wadau wa maendeleo kupitia sekta hizo kujadili na kuweka mikakati ya kutatua changamoto na kisha kufanya maendeleo.

Amewaambia wadau wa maendeleo ni vema wakatambua Wilaya ya Namtumbo kuna fursa nyingi ambazo zikitumika vizuri kutakuwa na maendeleo.

“Wilaya yetu ya Namtumbo tunayo ardhi ya kutosha na yenye rutuba inayokubali mazao ya kila aina.Wananchi wanaitumia vema ardhi iliyopo katika kujiletea maendeleo.

“Ombi langu kwa wadau wa sekta zote hizi tushirikiane katika kuleta maendeleo na kwetu tutafurahi tukiona viwanda vinajengwa zaidi na hasa vya kuongeza thamani ya mazao ya wakulima,”amesema Mfaume.

Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Namtumbo ambao wamepata nafasi ya kuuzungumzia mkutano huo wamesema unaonesha matumaini makubwa ya kupatikana kwa maendeleo ndani ya wilaya yao na zaidi wanampongeza Mkuu wao wa Wilaya kwani amekuwa chachu ya maendeleo ya wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Mfaume akizungumza wakati wa mkutano kati ya sekta binafsi na sekta za umma uliofanyika wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma leo

TBA WAKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA BUNJU, WANANCHI WAKARIBISHWA KUZINUNUA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh. Elias Kwandikwa amefanya ziara katika mradi wa nyumba zinazojengwa kupitia wakala wa majengo nchini (TBA) katika eneo la Bunju jijini Dar es salaam na kushauri wanananchi kujitokeza kununua nyumba hizo.

Akiongea baada ya kukagua nyumba hizo Kwandikwa amesema kuwa amekagua mradi huo na kuridhishwa na unavyoendelea kwa kuwa hadi sasa nyumba 279 kati ya nyumba 851 ambazo zipo kwenye malengo zimekamilika.

Kwandikwa amesema kuwa wananchi na wafanyakazi wajitokeze kununua nyumba hizo na kama serikali wanasimamia ili waweze kupata kilicho bora.

Aidha ameeleza kuwa heka 650 zilizopo Dodoma zitaanza kufanyiwa mradi huo mapema ili kuweza kuongeza makazi ya kutosha jijini humu katika wakati huu ambapo idara nyingi zimehamia Dodoma.

Pia amewataka wakala wa majengo nchini kutoa matangazo ili wananchi wajue kuna nyumba nzuri na bora zilizokamilika ili waweze kununua.

Na amewataka wafanyakazi wa wakala hiyo kufanya kazi kwa weledi na amewashauri waharakishe mradi wa ujenzi wa nyumba Dodoma.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TBA  Idara ya miliki Baltazari Kimangano ameeleza kuwa kuna nyumba za viwango vyote  na hadi sasa nyumba 105 zimekamilika  na wateja bado wanauhitaji na kwa wafanyakazi wanaweza kulipia miaka 7 kwa nyumba hizo.

Pia amesema kuwa wateja wanaweza kupata mikopo kupitia benki za CRDB, NBC, BOA na wanamazungumzo na benki ya Zanzibar ambazo zitatoa mkopo kwa riba nafuu kwa wateja wao ili kuweza kupata nyumba hizo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Mh. Elias Kwandikwa (katikati)akiwa na viongozi wa wakala wa majengo nchini (TBA) wakati alipofanya ziara ya kukagua nyumba za umma zilizojengwa na TBA zilizokamilika huko Bunju.
 Mkurugenzi wa Idara ya umiliki wa  mamlaka ya majengo nchini Bartazari Kimangano (kushoto) akimuongoza naibu waziri kukagua baadhi ya nyumba hizo.
Baadhi ya nyumba  zijulikanazo kama Villa ambazo zimekamilika na zipo tayari kwa makazi.

KURASA ZA MBELE ZA MAGAZETI YA LEO

NDUGULILE ATOA SIKU 14 KUKAMILISHWA KWA MASHINE YA X RAY HOSPITALI YA RUFAA DODOMA

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kitabu cha taarifa mbalimbali za hospitali wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma, kulia kwake ni katibu wa afya wa hospitali hiyo Mwanaisha Hassan.

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameutaka uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma kuhakikisha mashine ya kutolea huduma za X-ray  inafanya kazi ndani ya siku 14. 

Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza yenye lengo la kuangalia na kujiridhisha na hali ya utoaji huduma za afya  katika Hospitali hiyo leo jijini Dodoma. 

"Ifikapo Septemba 21 nataka kuona mashine ya kutolea huduma za X-ray na vifaa vingne viwe tayari kutoa huduma kwa wananchi wa Dodoma na maeneo yanayoizunguka kwani Hospitali hii ni tegemezi kwa wakazi wa mkoa huu la sivyo hatua stahiki zitachukuliwa bila ya kumuonea mtu haya" alisisitiza Dkt. Ndugulile

Aidha,Dkt. Ndugulile ametoa siku 30 kwa uongozi wa hospitali hiyo kukarabati jengo la bima ya afya baada ya kukagua na kutoridhishwa na muonekano wake kwani linaleta kero kwa wateja wanaokwenda kupata huduma Hospitalini hapo. 

Mbali na hayo Dkt.  Ndugulile ameonekana kukerwa na uzembe  wa watendaji wa Hospitali  hiyo na kusababisha kuwakemea vikali na kuhaidi maagizo aliyoyatoa yasipotekelezwa kwa wakati hatua za kinidhamu zitakuchululiwa kwa vitendo.

Wakati huo huo dkt.Ndugulile ameuagiza uongozi wa hospitali hiyo kuwarudishia fedha wagonjwa walizotumia kununua dawa pamoja na sindano kwenye maduka yaliopo nje ya hospitali hiyo ilihali wana vifaa hivyo  takribani ya kutosha miezi sita kwenye stoo yao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akikagua maboksi ya sindano katika stoo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wagonjwa waliokua wanasubiri huduma katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akitoa maelekezo kwa viongozi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali hiyo.

WAFANYABIASHARA MNARANI WAKINZANA NA HALMASHAURI YA MJI WA KIBAHA KATIKA KODI

$
0
0
 NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA.

MADUKA ya baadhi ya wafanyabiashara wa soko la Mnarani, Loliondo, halmashauri ya Mji wa Kibaha, Pwani, yamefungwa kwa siku tatu baada ya kushindwa kulipia kodi kwa zaidi ya mwaka sasa. Kufuatia kufungwa kwa maduka hayo, wameiomba ofisi ya mkuu wa mkoa huo iingilie kati suala hilo kwani wanatakiwa kulipa sh.8,000 kwa mita za mraba kiasi ambacho ni kikubwa kwao.

Mfanyabiashara aliyefungiwa duka lake ,Henry Makundi alisema wamehamishiwa kutoka Maili Moja stendi na kupewa maeneo Loliondo ili wajenge maduka na fedha zao watafidia kwenye kodi.  Alieleza, walikuwa wanataka kuwe na mafungu matatu ya malipo moja ya tatu mkurugenzi na moja ya tatu mfanyabiashara na moja ya tatu iwe ya mfanyabiashara kama wawekezaji moja ya tatu iwe kama faida.

Makundi alielezea ,halmashauri inataka asilimia 50 na mfanyabiashara 50 ili kurudisha gharama jambo ambalo hawakubaliani nalo.

Nae mwenyekiti wa soko hilo ,Ramadhan Maulid alishangaa kuona maduka yanafungwa. Alisema kwamba,kulikuwa na makubaliano walipe mita za mraba 4,000 huku akiwepo mkurugenzi na mbunge wa mji huo hivyo wanashangaa kuambiwa walipie sh 8,000.

Maulid alifafanua, kutokana na hali hiyo wanaendelea na mazungumzo na katibu tawala wa mkoa ili kuangalia namna ya kulishughulikia suala hilo .
Akijibu hoja za wafanyabiashara hao mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Jeniffer Omolo alisema ,walikubaliana kuwa wafanyabiashara wajenge maduka kwa gharama ya sh .milioni tano na halmashauri walitoa ardhi lakini hawajalipa kodi zaidi ya mwaka sasa.

Kwa mujibu wake ,wamegundua wengi wanaofanya biashara ni wapangaji na sio waliojenga maduka ambayo wanapangisha kuanzia sh.300,000 hadi sh.400,000 kwa mwezi.

Jennifer alibainisha ,kwa mwaka wanapata kati ya sh.milioni 3.6 - milioni 4.8 kwa miaka miwili anakuwa amerejesha gharama zake za ujenzi .

Mkurugenzi huyo aliwataka ,wale ambao gharama zimezidi ya waliyokubaliana waende ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo.

Jennifer alielekeza ,wafanyabiashara ambao hawajalipa kodi kulipa kwani kutolipa kodi ni kinyume cha sheria , ili waepukane na usumbufu.

KATIBU MKUU UVCCM AWATAMBULISHA WAKUU WA IDARA WAPYA KWA WATUMISHI WA MAKAO MAKUU UVCCM LEO

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) pamoja na wakuu wa Idara wapya wa Umoja wa Vijana walipowalisi katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya Makao Makuu UVCCM Upanga Dar Es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl.Raymond Mwangwala (MNEC) akizungumza na watumishi wa Makao makuu wakati akiwatambulisha wakuu wa Idara wapya wa Umoja wa Vijana walioteuliwa na Kuthibitishwa na baraza kuu la UVCCM Taifa lililoketi jijini Dodoma wiki iliyopita
 Wakuu wa Idara za Makao makuu UVCCM wakifuatilia mazungumzo ya Katibu Mkuu UVCCM Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) alipokuwa akiwatambulisha kwa watumishi wa UVCCM makao makuu.
 watumishi wa UVCCM makao makuu wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya Katibu Mkuu wa UVCCM Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) alipokuwa akiwatambulisha wakuu wa idara za UVCCM  makao makuu kwao
 Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni na Siasa Ndg Peter Kasela akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndg.Hassan Bomboko  akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndg Kamana Juma Simba  akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM.
Katibu wa Idara ya Uchumi na Uwezeshaji Ndg.Nelson Lusekelo akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) akiwakabidhi Mpangokazi wa Utekelezaji wa UVCCM Mwaka 2018/2019
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) akiwaongoza wakuu wa Idara za Makao makuu ya Umoja wa Vijana wakati akiwatembeza maeneo mbali mbali ya Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es Salaam
(Picha na FahadiSiraji wa UVCCM).

MAHAKIMU WAANDAMIZI WAPONGEZA ELIMU WALIYOIPATA KUHUSU SHERIA YA FIDIA KWA MFANYAKAZI

$
0
0
 Waheshimiwa Mashakimu Wakzi wa Mikoa na Wilaya kutoka Mikoa mitano ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara, wakiwa kwenye mahakama ya mfano ili kujipima kuona uelewa wao kuhusu Sheria ya Bunge ya Fidia kwa Wafanyakazi kifungu namba 5  [Sura ya 263 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2015] naada ya kushiriki mafunzo ya siku mbili yaliyoandaliwa na kuratibiwa kwa pamoja na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na kufanyika mkoani Morogoro kuanzia Septemba 5-6, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Morogoro


MAHAKIMU wakazi wafawidhi wa Mahakama za Mikoa na Wilaya kutoka mikoa mitano ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara, wamefurahishwa na mafunzo ya kuwajengea uelewa wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi yaliyoandaliwa kwa ushirikiano baina ya Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyoanzishwa kwa Sheria ya Bunge, kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura ya 263 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2015] ambapo jukumu lake kubwa ni kutoa fidia kwa wafanyakazi walioumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi wanazozifanya.
Kutokana na jukumu hilo la Mfuko, Chuo cha Uongozi wa Mahama Lushoto ambacho ndicho chenye dhamana ya kutoa mafunzo kwa watumishi waandamizi wa mahakama, kiliandaa mafunzo hayo ili kuwawezesha viongozi hao wa mahakama wa ngazi za mikoa na wilaya kuelewa vema Sheria hiyo ili iwe rahisi kwa wao kutoa maamuzi sahihi endapo mashauri yahusuyo fidia kwa wafanyakazi na shughhuli za Mfuko yatafika mbele yao. Amesema Mkuu wa Huduma za Sheria wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Abraham Siyovelwa.
Wakizungumza katika mahojiano baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Elizabeth Nyembele, alisema
“Nimefurahia sana kupata mafunzo haya, mimi nina nafasi mbili, kwanza kabisa kama mfanyakazi,  lakini pia kama mdau mkubwa wa Sheria ya Mfuko huu kama hakimu, nimefaidika sana na elimu hii kwani nimeelewa vitu vingi ambavyo hapo awali sikuwa nikivijua.”
Alisema, elimu aliyoipata kama mtumishi wa mahakama, ameelewa haki zake za msingi kuhusiana na Mfuko huo wa Fidia ameridhika na kufurahia kuwa anafanya kazi katika mazingira ya uhakika na akiamini pia hata wategemezi wake lolote likimtokea kutegemea na Mungu amepanga nini, basi wategemezi wake wanaweza kunufaika licha ya yeye mwenyewe.
“Uelewa nilioupata baada ya mafunzo haya ni mkubwa sana hususan kwenye makosa ya jinai yameelezwa bayana, na nimeelewa jinsi nitakavyosimamia sheria hii endapo nitakutana na kesi yoyote itakayoletwa mbele yangu, kwa sababu ninailewe sheria hii kwa kina.” Alisema
Alishauri pia Mfuko uendelee kutoa elimu hususan kwa wafanyakazi, kwani wengi hawajui manufaa ya huu Mfuko.
Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Lindi, Mhe. James Mutakyahwa Karayemaha amesema, mafunzo aliyoyapata yamemfanya apate uelewa mpana kuhusu sio tu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi na namna gani anapaswa kuisimamia wakati atakapokutana na mashauri yahusuyo Fidia kwa wafanyakazi, lakini pia amepata uelewa wa faida anazoweza kupata yeye binafsi kama mtumishi wa umma.
“Nimejua kuwa mwajiri kwa mujibu wa Sheria hii, anao wajibu wa kujisajili na kuwasilisha michango ya kila mwezi kwa Mfuko na asipofanya hivyo anatenda kosa la jinai na adhabu yake ni kifungo,  faini au vyote viwili.” Alisema
Alisema pia amejua kuwa kama mfanyakazi hapaswi kushwishiwa kwa namna yoyote ile na mwajiri wake, kutoa taarifa mbili tofauti za viwango vya mishahara, ambapo taarifa za malipo ya mtumishi zikionyesha kiwango cha juu cha mshahara na taarifa zinazopelekwa WCF zikionyesha kiwango cha chini cha mshahara.
“Taarifa hizi zisizosahihi kama hizi ni janga kwa mfanyakazi kwani endapo atapatwa na tatizo lolote la kuumia akiwa, kuugua au hata kifo akiwa kazini, inapofika wakati wa kufidiwa, malipo hayo yatazingatia taarifa za malipo ya mshahara zilizokuwa zikiwasilishwa  kwenye Mfuko.” Alisema.
Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara, Mhe.Godfrey Mwambapa, alisema kimsingi yeye ameongeza weledi kuhusu sheria inayoendesha na musimamia shughuli za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
“Mfuko huu nunatuhusu watu wote tulio kwenye ajira na kwakweli unatusaidia hasa kuwa salama sehemu ya kazi endapo utapatwa na matatizo sehemu ya kazi Mfuko huu utakuja na kunifanya niishi kama vile nikiwa kazini na kuniondolea magumu yote ya kimaisha.” Alsiema.
Alisema, yeye kama hakimu ameweza kuelewa sheria inayosimamia Mfuko na hata kama shauri lihusulo masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi litamfikia mbele yake yuko katika nafasi nzuri ya kusimamia sheria hii kwani ameielewa vilivyo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, mafunzo hayo ni muendelezo wa mipango ya Mfuko kutoa elimu kwa wadau wote ambapo tayari Mfuko umetoa elimu kw amadaktari kote nchini, Waajiri kote nchini, lakini pia elimu kwa wafanyakazi kwenye maeneo yao ya kazi kupitia ziara za maafisa wa WCF kwenye taasisi mbalimbali hapa nchini.

 Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Chuom cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, (IJA), Mhe. jaji Dkt.Paul Kihwelo, akitoa nasaha zake kwa washiriki wa mafunzo hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya JIA na WCF. Aliyesimama kushoto ni mratibu wa mafunzo, Mhadhiri Msaidizi wa Chuo hicho, Mhe. Lameck Samson.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Temeke jijini Dar es Salaam, Mhe. Susan P. Kihawe (kuli) akifurahia jambo wakati akizungumza na mwenzake, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Ilala, Mhe. Martha Mpaze.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Elizabeth Nyembele, akizungumza.

 Waheshimiwa mahakimu wakiwa kwenye majadiliano ya vikundi.
 Mhe.S.Mwalusamba (kushoto) na Mhe.Godfrey Mwambapa wakifuatilia kwa makini.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kinondoni, Mhe. Gofrey Isaya, akizungumza
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Pwani, Mhe.Joyce J. Mkhoi, akitoa maoni yake kwenye semina hiyo.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, Mhe. Batista Kashushe, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
 Mhadhiri Msaidizi Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, Mhe. Lameck Samson akifafanua jambo.
 Hakimu Mkazi wa Mfawidhi Mahakama ya Kilombero/Ifakara Mkoani Morogoro, Mhe. L.Khamsini akisikiklzia kwa makini wakati Mkuu wa Huduma za Sheria wa WCF, Bw. Abraham Siyovelwa (hayupo pichani) alipokuwa akitoa mada.
 Majadiliano ya vikundi
 Majadiliano ya vikundi
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Masha Mshomba, (wapili kushoto), akimkabidhi cheti cha ushiriki, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani, Mhe. Devota Kisoka, mwishoni mwa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo mahakimu wakazi wa mikoa na wilaya yaliyofikia kilele mkoani Morogoro Septemba 6, 2018. Wengine pichani ni Mkuu wa Huduma za Sheria WCF, Bw. Abraham Siyovelwa. na kulia ni Mhadhiri Msaidizi, Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) Mhe. Lameck Samson.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Masha Mshomba, (kulia) na Mkuu wa Huduma za Sheria, wa Mfuko huo, Bw. Abraham Siyovelwa, wakipiga makofi ikiwa ni ishara ya kuwapongeza mahakimu hao baada ya kumaliza mafunzo.
 Majadiliano ya vikundi.
Afisa Uhusiano na Mawasiliano mwandamizi wa WCF, Bw. Sebera Fulgence, (kushoto), na Afisa Sheria wa Mfuko huo, Bw. Deo Victor wakijadiliana jambo mwishoni mwa mafunzo hayo.


Afisa Sheria WCF, Bw. Deo Victor (aliyesimama kulia) akisimamia majadiliano ya vikundi kuhusu kile kilichofundihswa. 

RAIS MAGUFULI AKAGUA UJENZI WA DARAJA LA MTO MARA, AHUTUBIA WANANCHI WA NYAMONGO MKOANI MARA

$
0
0


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Nyamongo mkoani Mara wakati akitokea Mugumu Serengeti.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kukagua daraja hilo la mto mara lenye urefu wa mita 94 linalounganisha katika ya Wilaya ya Serengeti na Tarime mkoani Mara.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyansura Serengeti mara baada ya kukagua mradi wa daraja la mto mara lenye urefu wa mita 94 linalounganisha katika ya Wilaya ya Serengeti na Tarime mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Nyambura Nyamarasa ambaye alikuwa na kero ya kulishiwa na shamba lake na mfugaji mmoja huko Mugumu Serengeti mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa shilingi milioni moja Nyambura Nyamarasa ambaye alikuwa na kero ya kulishiwa na shamba lake na mfugaji mmoja huko Mugumu Serengeti mkoani Mara.

Sehemu ya Daraja la mto mara mita 94 ambalo ujenzi wake unaendelea na litaunganisha kati ya katika ya Wilaya ya Serengeti na Tarime mkoani Mara. PICHA NA IKULU

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UTURUKI NCHINI

$
0
0
  Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu kabla ya kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi huo,  pia kujifunza shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu  wakati wa kikao baina yao kilicholenga kuboresha uhusiano kati ya Bunge na Ubalozi, nakujifunza shughuli Mbali mbali zinazofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu baada ya mazungumzo yaliyofanyika  leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

DC ahimiza jamii za wafugaji kusomesha watoto wa kike hadi chuo kikuu

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Simanjiro
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula amezitaka jamii za wafugaji kuanza kuchukua hatua dhidi ya Mila potofu zinazoendelea kumkandamiza Uhuru wa mtoto wa kike na kumfanya ashindwe kusoma kwa maslahi ya wazazi wake

Aidha ameitaka jamii hiyo ya kabila la kimasai kubadilika na kuanza kusomesha watoto wa kike hadi vyuo vikuu ili kuwapatia elimu itakayosaidia kuielimisha jamii hiyo ili kuachana na mila potofu zikiwemo ndoa za utotoni na ukeketaji .

Kauli hiyo ameitoa mapema jana katika kijiji cha Namalulu,wilayani Simanjiro,Mkoa wa Manyara wakati  alipohudhulia   sherehe za Kimika za kusimikwa kwa viongozi wakuu wa kabila la Kimasai alimaarufu Laigwanani.,Ambapo  Mzee Meshack Toreto na Lucas Kisongira walisimikwa kuwa viongozi wakuu wa Kimila katika jamii hiyo.

"Jamii za kifugaji lazima zianze sasa kumwandaa mtoto wa kike kwa ajili ya kumpatia Elimu bora ili aje kuikomboa jamii hiyo ambayo baadhi yao bado wanaendekeza mila potofu zilizopitwa na wakati''Amesema chaula

Mhandisi Chaula alisema serikali inaunga mkono mila na destuli za makabila mbalimbali na aliahidi kushirikiana na viongozi wa kimila  na kuwataka kufuata taratibu na sheria za nchi ikiwemo kuhamasisha maendeleo na kujiepusha na tamaduni zinazokinzana na sheria za nchi.

Ameipongeza jamii huyo ya kimasai kwa  hatua hiyo ya kuendelea kudumisha mila na tamaduni zao jambo linaloendelea kulipa sifa taifa katika nyanja za kimataifa kwani kwa hapa nchini ni kabila pekee linalotambulika kimataifa katika utamaduni wao unaoleta tija kimataifa.

Awali katibu wa viongozi wa kimila Ilaigwanak, Mchungaji Yohana ole Tiamongoi amesema kupitia viongozi hao wa kimila wamefanikiwa kuziondoa mila mbalimbali potofu katika jamii yao kupitia maadhimio mbalimbali kwenye vikao vyao.

Katika sherehe hizo za kusimikwa viongozi hao wa kimila katibu huyo amewataka wafugaji wa jamii hiyo kuanza kuwekeza kwa mtoto wa kike kwa kumpatia Elimu hadi  chuo kikuu.

Mmoja wa Laigwanani aliyesimikwa ,Meshack Toreto alisema kuwa kazi yao kubwa ni kutatua changamoto mbalimbali kwenye jamii yao ikiwemo migogoro ya Ardhi ili kuisaidia serikali kupunguza msongamano wa mashauri mahakamani yanayotokana na migogoro ya jamii hiyo.

"Sisi hatupingi watu wetu kwenda kwenye vyombo vya kisheria ila tunataka zaidi mambo yetu kuyamalize wenyewe na hii itasaidia hata serikali kupunguza mzigo wa wa kuendesha kesi mahakamani''Amesema Toreto

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula (kushoto) akimkabidhi rungu maalumu mmoja ya wazee wakubwa, Meshack Toreto aliyesimikwa kuwa Laigwanani wa kabila la wamasai katika kijiji cha Namalulu, wilayani Simanjiro jana.

VYUO VIKUU VIWE NA BODI ILI KULINDA MASLAHI YA WANAFUNZI NA WAHADHIRI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MBUNGE wa Manonga Mh. Seif Gulamali amependekeza kuwepo kwa bodi maalumu itakayowaongoza wahadhiri wa vyuo vikuu kiutendaji na kinidhamu.

Akichangia katika mjadala wa kupitisha muswada wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi  kuhusiana na uanzishwaji wa bodi ya kitaalamu ya walimu nchini ambayo itakuwa na majukumu ya kuinua viwango vya utaalamu wa Ualimu kwa lengo la kuhakikisha walimu wanakuwa na viwango stahiki kitaaluma na kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya ualimu.

Gulamali ameunga mkono muswada huo na kuongeza kuwa isiwe kwa walimu pekee bali ilenge kwa wahadhiri pia ambao  wana wana umoja wao kama UDOMASA kwa wahadhiri wa Chuo kikuu cha Dodoma na UDASA kwa chuo kikuu cha Dar es saalam.

Ameeleza kuwa vyuo vyenye umoja huo lazima kuwe na bodi moja ambayo itawaongoza na majukumu ya bodi iwe ni pamoja na kusajili wataalamu hao kwa ngazi za shahada, uzamili na uzamivu na kujua idadi yao ili kuweza kuwa na takwimu sahihi za idadi ya wataalamu hao.

Pia ameshauri kuwa bodi hiyo iwe na kazi ya kutambua uwezo wao kitaalama sambamba na kusimamia nidhamu hasa malalamiko ya wanafunzi hasa wakike juu ya wahadhiri kwa manyanyaso ya kijinsia.

Aidha amesema kuwa bodi hizo zitakuwa na maslahi kwa pande zote mbili  wawezeshaji na wawezeshwaji katika elimu ili kuweza kuzalisha wataalamu wengi na bora zaidi.

Muswada huo uliopita Bungeni utawalenga walimu katika ngazi zote waliohitimu katika vyuo vinavyotambulika kwa ngazi ya Shahada, stashahada na astashahada na utashirikisha taasisi na wizara mbalimbali zikiwemo Utumishi wa Umma, Chama cha Walimu, Maafisa elimu, Wizara ya mambo ya ndani na Ofisi ya Waziri Mkuu.

ISBAH ENTERTAINMENT YAANDAA SHOW YA KIBABE JIJINI DAR

Viewing all 39168 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>