Quantcast
Channel: MTAA KWA MTAA BLOG
Viewing all 39030 articles
Browse latest View live

MEYA WA DAR ES SALAAM AZIDUA MASHINDANO YA MASHAIRI

$
0
0
 Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Mashairi ambayo yanaendelea katika ukumbi huo ambayo yameshirikisha washiriki 51 kutoka Dar es Salaam pekee.

Mkurugenzi wa Taasisi ya taaruma za Kiswahili wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Ernesta Mosha akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya ushairi yanayoendelea kufanyika jijini Dar es Salaam leo Septemba 1,2018.
 Jaji wa mashindano ya mashairi, Nassoro Mhamed akizungumza na kuwapa moyo washiriki wa mashindano ya mashairi yanayofanyika jijini Dar es Salaam leo Septemba 1,2018.

Baadhi ya wahudhuriaji katika mashindano ya majaji.
 Wanafunzi wa shule za sekondari walikuja kuangalia mashindano ya mashairi yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki wa mashindano ya mashairi.
Washiriki wa mashindano ya mashairi ambayo yanalengo la kukuza Lugha ya kiswahili nchini Tanzania.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

MEYA wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amezindua mashindano ya mashairi jijini Dar es Salaam leo yenye lengo la kukuza lugha ya kiswahili hapa nchini mashindano hayo yenye kauli mbiu  isemayo " Lugha yetu fahari yetu"

Mashindano hayo mgeni rasmi atakuwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ally Hasan Mwinyi washiriki wa mashindano hayo ni 51 ambapo mshindi wa kwanza atapata shilingi milioni moja, mshindi wa pili atapata shilingi lakitano, mshindi wa tatu atapata shilingi laki tatu na mshini wa nne mpaka kumi watapata shilingi laki moja moja.

Akizungumza katika uzinduzi huo wa mashairi ameomba lugha ya Kiswahili itumike barani Afrika kwa ujumla na Hapa nchini itumike kama Lugha ya kufundishia.

Amesema kuwa mashindano hayo hayataishia jijini Dar es Salaam tuu pia anategemea kuanzisha na mikoa mingine ya Tanzania. "Mashindano haya hayataishi jiji la Dar es Salaam tuu pia tutayaanzisha na mikoa mingine ya Tanzania"

Pia ameomba Lugha ya kiswahili iweze kurasimishwa katika nyanja za kisheria. kiafya pamoja kielemu kwa shule za msingi na sekondari pamoja na chuo kikuu ili mwanafunzi akifundishwa aelewe lugha na kitu anachofundishwa ili ajengewe uwepo wa kuelewa vizuri.

Nae Mkurugenzi wa Taasisi ya taaruma za Kiswahili wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Ernesta Mosha amesema kuwa vitabu vya kufunsihia kidato cha kwanza mpaka cha nne vimeshatayarishwa kwaajili ya kufundishia ila bado havijalasimishwa tuu kutumika vitabu hivyo ni pamoja na Bayilojia, Hisabati, Jeografia na Historia ambavyo vimeandiskwa kwa lugha ya kiswahili fasaha bila kutohoa(translation)

Amesema kuwa tafiti zinaonesha kuwa kikwazo cha Istilahi sio tatizo kabisa kwa sababu mtu anajifunza kuanzia shule ha msingi mpaka chuo kikuu na lugha ya kiingereza iwe kama ya kujifunza ili kuwezesha mawasiliano ya kawaida.

SERIKALI YAJIPANGA KUBHIBITI UCHELEWESHAJI WA KUPAKUA SHEHENA YA MAFUTA BANDARINI

$
0
0

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwele, kushoto akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya bandari na kituo cha kushushia mafuta cha KOJ.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwele, wa pili kushoto akiangalia moja ya nondo zilizoshushwa bandarini kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya bandari na kituo cha kushushia mafuta cha KOJ. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko.  
 Mkandarasi wa mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam (DMGP) kutoka Kampuni ya China Habour Engineering, LV Wei, kushoto akitoa maelezo ya mradi huo ulipofikia kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwele, wa pili kulia na Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya bandari na kituo cha kushushia mafuta cha KOJ.

SERIKALI yajipanga kubhibiti ucheleweshaji wa kupakua shehena ya mafuta bandarini
Dar es Salaam, Tanzania. Septemba 1, 2018. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kwamba Serikali imejipanga kubhibiti ucheleweshaji wa kupakua shehena ya mafuta bandarini ili kubhibiti upandaji bei ya bidhaa hiyo kwenye soko la ndani.

Waziri Kamwelwe ameyasema hayo jijini Dar es Salaam, wakati alipotembelea bandari ya Dar es Salaam katika eneo la Kurasini Oil Jet (KOJ), na kubaini kuwa wakati wa zoezi la upakuaji kunakuwa na tatizo la ucheleweshaji mbalo mwisho wa siku huchangia kuongezeka bei ya mafuta. 

Mh. Kamwele amesema kwamba wamegundua kuwa uwezo mdogo wa pampu za meli za kupakulia mafuta pamoja na uhaba wa matenki ya kuhifadhia mafuta kwa waagizaji wa bidhaa hiyo pamoja na kuvuja kwa mabomba ya mafuta ndio chanzo kikubwa cha kupanda bei.  

“Tumegundua kuwa tatizo lingine linalochangia kuongeza bei ya mafuta kuwa ni ucheleweshaji wa kupakua shehena hiyo ya mafuta kwani baadhi ya meli hazina pampu zenye wezo wa kusukuma bidhaa hiyo kwa nguvu inayotakiwa,” amesema waziri Kamwele.

Mhe Waziri amesema kwamba tatizo lingine alilogundua kuwa linachangia ucheleweshaji wa kupakua bidhaa hiyo sokoni ni waagizaji wa mafuta ambapo wengi wao huagiza shehena kubwa wakati uwezo wa matenki ya kuhifadhia mafuta hayo ni mdogo.

Mbaya zaidi amesema Waziri Kamwele kwamba gharama za ucheleweshaji huo kupelekwa kwa mtumiaji wa mwisho ambaye ni mwananchi. Kufuatia hali hiyo amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa TPA, kufanyia kazi suala hilo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko, amemuahidi Waziri kuwa atalisimamia hilo kikamilifu sababu ni kweli kwamba baadhi ya meli hazina pampu zenye nguvu ya kusukuma mafuta hayo kwa haraka.

Mhandisi Kakoko amesema kwamba kuhusu waagizaji mafuta atawasiliano nao tena kuwakumbusha juu ya hilo na kuwataka wawe wanaagiza mafuta kutokana na uwezo wao au waongeze idadi ya matenki ya kuhifadhia mafuta.

Ametolea mfano meli ambayo ilifunga mnamo tarehe 13/08/2018 na kukamilisha usukumaji wa mafuta kwa siku 11, jambo ambalo limesababisha ucheleweshaji mkubwa wa kupakua shehena hiyo kwa ajili ya soko.

“Makampuni yaliyokuwa yapokee mafuta siku hiyo yalikuwa ni zaidi ya 20 sasa ukichukulia meli kama hiyo ambayo ilikuwa ujazo wa mita karibu 104,000, ilitumia taribani siku 11 hali iliyosababisha wengine wachelewe kupata bidhaa hiyo sokoni,” amesema.

Ameyasihi maakapuni ya mafuta kuwa ni vyema yakaongeza matenki yao ya kuhifadhia mafuta au waagize kulingana na uwezo wao. Vinginevyo basi TPA haitolipa tozo zinazotokana na ucheleweshwaji huo bali kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe.

Meli ya mafuta ikikaa bandari kwa zaidi ya siku tano, TPA hulipa gharama za ukaji wa meli hiyo kwa kiasi cha US$ 25,000 kwa siku hadi meli hiyo itakapoondoka.

Kuhusu uvujaji wa mafuta, Waziri Kamwele ametoa maagizo kwa TPA kuwa wasipitishe tena mafuta kwenye mabomba au kwenye pacha za mabomba yanayovuja na kuongeza kuwa pia ni kinyume na utaratibu kupandisha bei ili kufidia hasara inayotokana na uvujaji huo.

Ameongeza kuwa kuendelea kupitisha mafuta kwenye mabomba yanayovuja kumefanya mwananchi ambaye ndio mtumiaji wa mwisho kubebeshwa mzigo usiostahili na kuongeza kwamba Serikali imeligundua hilo na kwa kuanzia itanunua ‘flow meter’ mpya na kuzifunga katika bandari zote. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko, amemuahidi Waziri huyo kuwa hawatoruhusu tena mafuta yaendelee kupita katika mabomba yanayovuja kwani kinachoonekana ni kuwa vifungashio vingine ambavyo vinatumika havikidhi matakwa ya kiubora katika kuhudumia bidhaa ya mafuta. 

“Kuna takribani makapuni 50 ya mafuta yanayopitisha bidhaa zao bandarini, tutawaandikia barua na kuwaelekeza waboreshe mabomba yao, kwa wale ambao watakaidi basi hatutapitisha mafuta yao kupitia miundombinu hiyo,” amesema Mhandisi Kakoko.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kamwelwe alikagua mradi wa uboreshaji wa gati namba 1 hadi 7 katika bandari hiyo na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wake hadi sasa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, ujenzi wa mradi huo unakwenda kwa kasi sababu unasimamiwa kwa ukaribu na watendaji wa TPA chini ya uongozi wake.

Amesema kwamba hadi sasa mradi huo umefikia asilimia 40 ya ujenzi wake ambapo upo mbele kwa asilimia 10 zaidi ya lengo lililopangwa.

Pindi mradi huo utakapokamilika utaifanya bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa zaidi na yenye uwezo mkubwa wa kuhudumia meli kubwa hadi za size ya Panamax ambazo ni moja ya meli kubwa na za kisasa zaidi duniani.

WABUNGE WANAWAKE WAKUSANYA BIL 2.5/-KUJENGA CHOO CHA MFANO KWA MAJIMBO YOTE NCHINI

$
0
0

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Anne Makinda akizungumza wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
  Spika wa Bunge, Job Ndugai akizungumza wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya shughuli ya harambee, Magreth Sitta akizungumza wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa maandalizi ya shuguli ya harambee ya wabunge, Profesa Anna Tibaijuka akizungumza wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Anne Makinda na  Makamu Mwenyekiti wa maandalizi ya shuguli ya harambee ya wabunge, Profesa Anna Tibaijuka wakiwa tayari kusoma fedha wazilizo changisha wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
  
 Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Anne Makinda akipokea hundi kutoka kwa wawakilishi wa benki ya NBC wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Anne Makinda akipokea hundi kutoka kwa wawakilishi wa benki ya CRDB wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

wakati wa harambee ya uchangiaji wa fedha kwaajili ya kujenga choo cha Mfano katika majimbo yote hapa nchini iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

*Spika mstaafu Makinda ashangazwa… atoa neno 
*Dk.Tulia asema ili kufanikisha lengo zinahitaji Bil 3.5/- 
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

CHAMA cha Wabunge Wanawake wa Bunge la Tanzania wamefanikiwa kukusanya Sh.milioni 800 kwenye harambee ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa choo kitakachojengwa katika majimbo yote nchini.

Fedha hizo zimekusanywa jana kwenye harambee iliyofanyika Mliman City jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi kwenye harambee hiyo alikuwa Spika wa Bunge mstaafu Anne Makinda.

Tayari wabunge hao wanawake wamefanikiwa kukusanya jumla ya Sh.bilioni 2.5 kwani kabla ya harambee ya jana tayari walishafanya harambee nyingine ya kukusanya fedha jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa harambee hiyo Spika wa Bunge Job Ndugai amesema wanatambua umuhimu wa kuunga mkono jitihada za wabunge wanawake katika kuhakikisha wanatimiza lengo la ujenzi wa choo.

“Tumekutana hapa kwa lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo.Lengo ni kujenga vyoo nchi nzima kwa maana ya majimbo yote,”amesema Ndugai.

Kwa upande wa mgeni rasmi Spika mstaafu wa Bunge Makinda amesema uamuzi ambao umefanywa na wabunge wanawake na kuungwa mkono na wabunge wanaume katika kufanikisha fedha zinapatikana ni wa kihistoria.

“Tunatambua changamoto ambazo wanafunzi wanazipata na hasa kwa mtoto wa kike kutokana na maumbile yake.Hivyo ujenzi wa choo cha mfano kitasaidia kuwafanya wanafunzi hao kufurahia mazingira yatakayokuwamo kwenye choo hicho.

“Tunafahamu binti wa kike anapovunja ungo akiwa shuleni kuna mabadiliko yanaanza kutokea na anapokuwa kwenye tarehe yake wengine wanatega shuleni kwa kuona hawako salama.Choo kitakachojengwa kitamfanya binti kutokuwa na wasiwasi hata akiwa kwenye tarehe za hedhi,”amefafanua.
Makinda ametoa ombi kwa Watanzania kokote walipo kuchangia ujenzi wa choo hicho kwani lengo na kumuondolea adha mwanafunzi na hasa mwanafunzi wa kike.

Pia amesema kitendo cha wabunge hao kuamua kuchangisha fedha kimemshangaza huku akiwaaambia wamefanya kitu kikubwa na chenye thamani.

Ameongeza mkombozi wa mtoto wa kike ni mazingia rafiki yanayomuwezesha kuwa huru kutimiza ndoto zake.

Wakati huo huo Naibu Spika wa Bunge Dk.Tulia Akson amesema kuwa ili kufanikisha mchakato wa ujenzi wa vyoo hivyo zinahitajika Sh.bilioni 3.5 kwa nchi nzima.

Amesema wabunge wanawake wameona haja ya kuhakikisha wanakusanya fedha kwa ajili ya kujenga choo cha mfano kwa majimbo yote.

Amefafanua choo kimoja kitagharimu Sh.milioni 11 na hivyo ili kujenga kwenye majimbo yote wanahitaji Sh.bilioni 3.5.

Katika kufanikisha ukusanyaji huo wa fedha unafanikiwa taasisi, mashirika, kampuni binafsi, watu mashuhuri wabunge wameonesha mshikamano kwa kuchangia fedha hizo.

Pia ili kufanikisha harambee hiyo bidhaa mbalimbali zilipigwa mnada ambapo fedha zilizopatikana zinakwenda kwenye ujenzi huo.

WABUNGE WAAMSHA SHANGWE UKUMBI WA MLIMANI CITY DAR

$
0
0
*Profesa Jay, Nape wachuana, Mlinga aendesha kigari jukwaani 

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii 
BUNGE limesheheni vipaji katika fani ya Sanaa na burudani!Hivyo ndivyo unavoweza kuelezea baada ya wabunge kutoka majimbo mbalimbali kuonesha umahiri wao katika fani hiyo. 

Wabunge hao wamedhihirisha hili jana usiku kwenye ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam wakati wa harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa choo cha mfano. 

Hivyo kabla ya kuanza kwa shughuli ya harambee hivyo, wabunge waliamua kuteka sekta ya Sanaa na burudani kwa kuonesha umahiri wao. 

Wapo wabunge ambao wameonesha umahiri katika mchezo wa sarakasi huku wengine wakishindana kucheza Singeli.

Pia wabunge wengine walishiriki kuimba nyimbo maalum kwa ajili ya harambee hiyo na wapo walioimba kwaya pamoja na kucheza nyimbo za kabila la Wanyamwezi. 

Hata hivyo baada ya burudani hiyo kupamba moto jukwaa likatawaliwa na ushindani mkali kati ya Mbunge wa Mtama Nape Nnauye na Mbunge wa Mikumi Joseph Haule a.k.a Profesa Jay. 

Wakati Nape ameamua kuimba nyimbo za zamani(Zilipendwa) Profesa Jay yeye aliamua kuimba muziki wa kizazi kipya. 

Hata hivyo hakukuwa na mshindi kwani kila mmoja alionesha umahiri mkubwa wa kushika kipaza sauti na kuteka mashabiki ambao wengi wao walikuwa wabunge wenyewe pamoja na wageni waalikwa. 

Haikushia hapo kwani wabunge hao katika kuthibitisha hakuna ambacho hawakijui wapo ambao wao walionesha umahiri wa kulitawala jukwaa kwa kuonesha mitindo ya mavazi. 

Mbunge Geita Vicky Kamata na Mbunge Mathar Mlata wao walithibitisha ubora wa sauti zao walipokuwa wanongoza wabunge wengine kuimba. 

Naibu Spika Dk.Tulia Akson yeye alipanda jukwani kuimba wimbo wa Subalkere Mpenzi akiwa mtoto wake(Gudlucky Mlinga) aliyekuwa anaendesha kigari . 

Baadhi ya wageni waalikwa ambao wamezungumzia namna ambavyo wamebunge hao wameonesha umahiri katika eneo la burani wamesema wanastahili kupongzwa. 

kwani wamethibiwa Viti Maalum Mkoa wa Samua kutoa na kuchezea , kucutoa buruWABUNGE mbalimbali wameonesha.
 
















  














































   




  








TRENI YA KIFAHARI DUNIANI YALETA WATALII 64 DAR KUPITIA RELI YA TAZARA

$
0
0
 Fatma Salum- MAELEZO
TRENI ya kifahari inayojulikana kwa jina la ROVOS ambayo ni miongoni mwa treni tatu bora duniani imewasili jijini Dar es Salaam kwa kutumia reli ya Tazara ikiwa na watalii 64

Watalii hao wamekuja Tanzania kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali yenye vivutio vya utalii hapa nchini ikiwemo mbuga za wanyama na visiwa vya Zanzibar.

Akizungumza katika hafla fupi ya kuwapokea watalii hao iliyofanyika stesheni ya TAZARA Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa TAZARA Tanzania, Fuad Abdallah alieleza kuwa treni hiyo iliondoka mji wa Cape Town nchini Afrika ya Kusini Agosti 18, mwaka huu.

“Watalii mbalimbali huja nchini mara tano kwa mwaka kwa kutumia ROVOS kupitia reli ya TAZARA na nchi yetu hunufaika na ujio huu hasa faida za kiuchumi,” alisema Fuad.

Aidha alibainisha kuwa treni ya ROVOS ni miongoni mwa treni tatu bora duniani, hivyo ujio wa treni hiyo na watalii unatokana na vivutio bora vya utalii na miundombinu mizuri ya reli ya TAZARA.

“Treni hii inatumia reli ya TAZARA kuleta watalii kwa sababu nchi yetu imekidhi vigezo vya utalii na reli yetu imekidhi vigezo vya usalama na mawasiliano ya uhakika,” aliongeza Fuad. 

Alisema kuwa katika safari hiyo ya treni watalii hao pia walipata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Selous iliyopo kusini mwa Tanzania na kuona wanyama mbalimbali wanaopatikana kwenye hifadhi hiyo.

Wakizungumza kwa furaha ya kuwasili Tanzania, watalii hao wa kijerumani walisema kuwa wamefurahia sana safari hiyo na mapokezi mazuri ya watanzania na kuahidi kurudi kwa mara nyingine.

Kwa upande wake mfanyakazi wa treni ya ROVOS, Monica Rieder mwenye asili ya Ujerumani alisema kuwa amewahi kufika Tanzania mara 14 na anavutiwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo yanayofanyika hapa nchini siku hadi siku.

TAZARA ni shirika la reli ya pamoja ya Tanzania na Zambia iliyoanza mwaka 1976 na inamilikiwa kwa asilimia 50 kila upande.


 Meneja Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) Fuad Abdallah (kulia), akizungumza na Waandishi wa Habari katika makao makuu ya shirika hilo Jijini Dar es Salaam kabla ya kuwasili kwa treni ya kitalii ya ROVOS kutoka Afrika ya Kusini.
 Baadhi ya watalii kutoka Ujerumani wakifurahia buradani ya bendi ya Polisi baada ya kushuka kutoka kwenye treni ya ROVOS moja kati ya treni ya kifahari duniani, watalii hao wamekuja nchini kutembelea vivutio mbalimbali.
Meneja Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) Fuad Abdallah (mwenye fulana nyekundu) akifuatilia mahojiano baina ya watalii na Afisa Habari wa Idara ya Habari-MAELEZO, Abraham Nyantori.
  Mtalii Diesknahn akizungumza na Afisa Habari wa Idara ya Habari Fatma Salum (kushoto) mara baada ya kuwasili nchini na treni ya ROVOS wakitokea Afika ya Kusini.
 Mama wa Kijerumani Linde Erdmann (katikati) akifurahia kuwasili Tanzania kwa mara ya kwanza akitokea Afrika ya Kusini kwa kutumia treni ya ROVOS kupitia reli ya TAZARA.
Moja ya mgahawa unaopatikana katika treni ya kifahari ya ROVOS iliyowasili leo hapa nchini ikitokea Afrika ya Kusini kupitia reli ya TAZARA.
Dereva wa treni ya ROVOS Abby (kulia) akizungumza na mmoja wa wafanyakazi wa treni hiyo mara baada ya kuwasili katika stesheni ya Dar es Salaam ikitokea Afrika  ya kusini kupitia reli ya TAZARA.
 Moja ya chumba cha kupumzika abiria katika treni ya kifahari ya ROVOS, treni hiyo ni miongoni mwa treni tatu za kifahari duniani.
  Treni ya ROVOS iliyobeba watalii 64 wa Kijerumani kutoka Afrika ya Kusini, ikiwasili leo stesheni ya TAZARA Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Paschal Dotto- MAELEZO).

MWILI WA MWANAFUNZI ALIYEFARIKI KWA KUPIGWA VIBOKO NA MWALIMU WAKE WAZIKWA WILAYANI MULEBA

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Sinkamba Kandege akitoa heshima za mwisho kwa Mwlili wa Mwanafunzi Marehemu Sperius Eradius aliyefariki dunia Agosti 27, 2018 baada ya kupigwa viboko na Mwalimu wake wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba.

Na ALLAWI KABOYO, MULEBA

Mwlili wa Mwanafunzi Marehemu Sperius Eradius aliyefariki dunia Agosti 27, 2018 baada ya kupigwa viboko na Mwalimu Respicius Mtazangira ambaye alikuwa Mwalimu wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba umeagwa  na kusafirishwa Wilayani Muleba Kata Mubunda Kijiji Kitoko nyumbani kwa baba yake mzazi Eradius Petro na kuzikwa leo Agosti 31, 2018.

Katika mazishi hayo Serikali iliwakilishwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Sinkamba Kandege ambaye alitoa salaam za Serikali katika msiba huo kwa kuwahakikishia familia, ndugu, jamaa wa marehemu pamoja na wananchi waliojumuika kumuaga Sperius Eradius kuwa lazima Serikali isimamie haki mpaka ipatikane kwa waliohusika katika tukio la mauaji ya mwanafunzi huyo.
“Sisi tunawaacha watoto wetu waende shule kama sehemu salaama tukiamini kuwa ndiyo sehemu salama na ya kujifunzia na siyo chuo cha mafunzo ya viboko. Jambo hili haliwezi kuachwa likapita  hivi hivi tuseme inatosha na iwe fundisho kwa wengine.” Alisisitiza Mhe. Naibu Waziri Kandege.

Pia Mhe. Naibu Waziri Kandege  aliiomba familia ya marehemu kuwa na subira kwa wakati huu mgumu wa kupoteza mpedwa wao Sperius Eradius na kusema kuwa msiba si wao tu bali ni msiba wa taifa zima. Aidha, aliishukuru Serikali ya Mkoa ilivyoshughulikia tukio hilo tangu lilipotokea Agosti 27, 2018 hadi kuupumzisha mwili wa Mwanafuzi Marehemu Sperius Eradius nyumbani kwa baba yake mzazi Eradius Petro. 

Baba yake mlezi Mchungaji Justus Balilemwa akitoa historia ya Mwanafunzi Marehemu Sperius Eradius alisema kuwa mtoto huyo alizaliwa Mei 2005 na mara baada ya kuzaliwa mama yake aliaga dunia na Sperius Eradius kuchukuliwa na kupelekwa Ntoma katika Kituo cha kulelea watoto yatima na baada ya mwaka mmoja alimchukua mtoto huyo na kuanza kuishi na kumlea kama mtoto wake hadi mauti yalipomkuta Agosti 27, 2018 akiwa na umri wa miaka 13 Shuleni Kibeta Manispaa ya Bukoba.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Sinkamba Kandege akizungumza katika mazishi ya Mwanafunzi Marehemu Sperius Eradius aliyefariki dunia Agosti 27, 2018 baada ya kupigwa viboko na Mwalimu wake wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba.

“Kinachonisikitisha leo hii ni kuwa tulimchukua Sperius Eradius akiwa mzima lakini leo tumerudisha sanduku, haikuwa nia yetu tulitamani sana mtoto huyu atimize ndoto zake kwa kuwa alikuwa mchangamfu sana na alimjua Mungu kwa kuimba na kumtukuza Mungu katika Kwaya mbalimbali mfano kwaya ya Kagoma.” Alimalizia kwa uchungu mkubwa baba mlezi wa Sperius Eradius Mchungaji Justus Balilemwa.

Baba yake mzazi Marehemu Sperius Eradius, Eradius Petro akitoa neno kwa wananchi waliofika kumfariji katika mazishi hayo alisema yeye anamwachia Mungu kwa yaliyotokea bali anaishukuru Serikali kwa kulifuatilia tukio hilo kwa karibu sana. Pia na kutoa ushirikiano nyumbani kwa baba mlezi tangu tukio linatokea hadi kwenye mazishi ya Sperius Eradius.
Serikali ya Mkoa wa Kagera tangu kutokea kwa tukio hilo la mauaji ya Mwanfunzi Sperius Eradius (13) Agosti 27, 2018 imekuwa ikigharamia mahitaji yote katika familia ya baba mlezi na kugharamia jeneza la kumhifadhia marehemu pamoja na usafiri wa kusafirisha mwili wa marehemu, familia, ndugu na jamaa wa Sperius kutoka Kibeta kwenda Mubunda Kijiji Kitoko kwa ajili ya Mazishi. Aidha, Naibu Waziri  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Kandege alitoa Shilingi Milioni mbili kwaniaba ya Serikali.

K-VANT WAJA NA MUONEKANO MPYA NA LADHA YAKE HALISI YA SIKU ZOTE

$
0
0
Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya Mega Beverage Company Limited,ya mkoani Arusha, inayotengeneza pombe kali chapa maarufu ya K-Vant, imezindua chupa mpya za kinywaji cha K-Vant zenye mwonekano tofauti na chupa za awali.Mabadiliko hayo hayakubadilisha ladha halisi ya kinywaji hicho na wateja wake wataendelea kuifuahia ikiwa katika ladha yake halisi ya siku zote.

Lengo kubwa la kubadilisha chupa za pombe ya K-Vant, ni mkakati wa kampuni wa kupanua masoko yake ya ndani na nje ambapo imelenga kuwa katika mwonekano bora zaidi bila kuathiri ladha halisi ya kinywaji hicho ambayo inapendwa na watumiaji wengi wa pombe kali nchini na nje ya mipaka ya Tanzania

Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mh. Antony Mavunde.

Mh.Mavunde,alipongeza hatua ya kampuni kubuni mkakati wa kuongea soko la bidhaa na kuongeza kuwa masoko yakiongezeka ndivyo mapato ya serikali yanaongezeka kupitia kulipa kodi sambamba na kuongeza wigo wa ajira kutokana na kuhitajika nguvu kazi zaidi.

“Serikali ya awamu ya tano inao mkakati wa kuifanya Tanzania nchi ya viwanda,tutazidi kuboresha mazingira zaidi kwa wawekezaji katika sekta hii ili lengo la kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta hii lifanikiwe haraka sambamba na kupunguza changamoto ya tatizo la ajira kwa vijana “,alisema.

Mkurugenzi wa Masoko wa Mega Beverage Company Limited, Marco Maduhu alisema, “Kauli mbiu yetu ya kinywaji cha K-Vant katika mwonekano mpya ni ’Ni Halali Yako’ kampuni imejipanga kuimarisha usambazaji wa bidhaa ya pombe ya K-Vant katika sehemu zote nchini ili watanzania waendelee kufurahia ubora wake kikiwa katika mwonekano wa chupa mpya na katika ladha ileile waliyoizoe kuipata siku zote”.

Alisema uzinduzi wa chupa mpya za K-Vant mbali na kufanyika katika mkoa wa Dar es Salaam pia utafanyika katika mikoa ya Arusha na Mwanza, pia usambazaji wa kinywaji hiki kwenye mwonekano mpya katika ladha yake halisi utaendelea kufanyika katika mikoa yote nchini kuanzia sasa.”Wateja wetu wowote popote mlipo tunawashukuru kwa kuendelea kutuunga mkono nasi tutaendelea kuboresha huduma zetu za usambazaji na kuhakikisha kinywaji bora cha K-Vant kinawafikia popote mlipo kikiwa katika chupa mpya”alisisitiza

Maduhu, alioongeza kusema kuwa, kampuni ya Mega Beverage,itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ambapo kupitia uwekezaji wake itahakikisha inaendelea kuchangia pato la taifa kupitia kulipia kodi mbalimbali, kunufaisha watanzania wengi kupata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja, pia imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za serikali kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye jamii.Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (wa pili kulia) akionyeshwa na Meneja mauzo na Masoko wa Kampuni ya Mega Beverages, Marco Maduhu, Chupa mpya ya K-Vant wakati wa uzinduzi wa muonekano mpya wa chupa ya kinywaji cha K-Vant uliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. (Kushoto) ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Francis Kimaro.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Mega Beverages, wazalishaji wa Kinywaji cha K-Vant ,Francis Kimaro(kushoto) na Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni hiyo ,Marco Maduhu, wakigongeana glasi ya K-VANT
Baadhi ya wadau mbalimbali wa kinywaji cha K-VANT wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Mega Beverages Francis Kimaro
Baadhi ya wadau mbalimbali wa kinywaji cha K-VANT wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Mega Beverages wakati wa uzinduzi huo.

CHANGAMOTO YA KUPUNGUA KWA MAJI MTO MARA KUPATIWA UFUMBUZI

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amewakumbusha watendaji wa Wilaya ya Serengeti wajibu wao wa kipekee wa ulinzi katika hifadhi ya mbuga ya Serengeti kwakuwa Wilaya yao imebeba jina linalojulikana duniani kote ikiwa ni pamoja na eneo maalumu la wanyama aina ya Nyumbu ambao huvuka kwenda upande wa pili na kuwa miongoni mwa vivutio vikubwa vya utalii.

Waziri Makamba ameyasema hayo leo Wilayani Serengeti mara baada ya kufanya ziara ya kikazi Wilayani hapo kujionea uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira na kutembelea eneo la mto Mara eneo ambalo ni muhimu sana ki-ikolojia.

Katika kikao na viongozi wa Wilaya hiyo, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Bw. Wiliam Mwakilema aliainisha kuwa mtiririko wa maji katika Mto Mara kutoka chanzo chake kikuu katika Milima ya Mau nchini Kenya kimepungua kutokana na shughuli za kibinadamu na matumizi mengine yasiyoendelevu jambo linalohatarisha kupungua kwa mtiririko wa maji katika Mto Mara kwa kipindi kirefu, eneo ambalo ni kivutio pekee cha wanyama wanaohama dunia.

Katika kutatua tatizo hilo Waziri Makamba amesema kuwa masuala ya mazingira ni mtambuka hivyo Ofisi yake yenye dhamana na kusimamia hifadhi ya Mazingira nchini itafanya ziara ya kikazi nchini Kenya kwa lengo la kujadiliana na kupata ufumbuzi wa haraka juu ya jambo hilo.

“Sisi na wenzetu wa Kenya tumeingia mkataba mwaka 2013 wa matumizi sahihi ya rasilimali katika Mto Mara na kutunza ikolojia yake, kwa kushirikiana na Mawaziri wenzangu wa Maji na Maliasili na Utalii, tutafanya ziara nchini Kenya ili kwapamoja tupate ufumbuzi wa jambo hili ikiwa ni pamoja na Ziwa Chala, Ziwa Jipe na Ziwa Natroni ambayo yote yako pande mbili yaani Tanzania na Kenya.”

Waziri Makamba amesema Serikali itahakikisha maslahi ya Nchi yanalindwa kwa njia za ki-diplomasia na kuhakikisha Mto Mara unatiririsha maji kipindi chote cha mwaka. Waziri Makamba amehitisha ziara yake Mkoani Mara na amewasili Mkoani Arusha ambapo atakuwa na vikao wa wadau wa hoteli mbalimbali na kambi za uwindaji kwa lengo la kuweka mikakati ya kuhifadhi mazingira maeneo ya mbugani.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akiwa amesimama pemebezoni mwa Mto Mara eneo la ‘Kogatendo’ na kupata maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Serengeti Bw. William Mwakilema juu ya kupungua kwa maji katika Mto huo. Waziri Makamba ameahidi kuipatia ufumbuzi changamoto hiyo mapema iwezekanavyo.
Bw. William Mwakilema (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba mara baada ya kutembelea Mto Mara eneo maalumu ambalo wanyama aina ya nyumbu huvuka kwa makundi na kuwa kivutio kikubwa cha utalii.
Eneo la Kogatendo katika Mto Mara ni miongoni mwa maeneo ambayo wanyama aina ya nyumbu huvuka kwa makundi na kuwa kivutio cha utalii. Waziri mwenye dhamana ya usimamizi wa Mazingira January Makamba ametembelea eneo hilo ili kuhakikisha hatua zinachukuliwa kurejesha ikolojia ya mto huo katika hali ya awali.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA CHINA JIJINI BEIJING

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na baadhi ya Wafanyabiashara wa nchini China, wakati akizungumza nao leo jijini Beijing ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC),unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa China Xi Jinping kesho jumatatu Septemba 3, 2018 ambapo utafanyika kwa siku mbili. Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Joh Pombe Magufuli, katika mkutano huo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya Wajumbe kutoka Tanzania waliopo nchini China kuhudhudhulia Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC),unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa China Xi Jinping kesho jumatatu Septemba 3, 2018.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na baadhi ya Wafanyabiashara wa nchini China,mara baada ya kuzungumza nao leo jijini Beijing ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC),unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa China Xi Jinping kesho jumatatu Septemba 3, 2018 ambapo utafanyika kwa siku mbili. Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Joh Pombe Magufuli, katika mkutano huo.
Balozi wa Tanzani chini China, Mbelwa Kairuki akimtambulisha mmoja wa wafanyabiashara wa China kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Godfrey Mwambe baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuzungumza nao leo jijini Beijing, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC), unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa China, Xi Jinping kesho jumatatu Septemba 3, 2018 ambapo utafanyika kwa siku mbili.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Godfrey Mwambe akibadilishana kadi na baadhi ya Wafanyabiashara wa nchini China.

BARABARA YA MASWA-BARIADI KUONGEZA UKUAJI WA UCHUMI KANDA YA ZIWA

$
0
0
Ujenzi unaondelea wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa Km 49.7 kwa kiwango cha lami unatarajiwa kufungua mkoa wa Simiyu na mikoa jirani ya Mara, Mwanza na Shinyanga hivyo kutarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe mkoani Simiyu wakati akikagua barabara hiyo inayojengwa na mkandarasi wa kampuni ya CHICO na kuridhishwa na hatua zilizofikiwa katika ujenzi huo toka ulipoanza mwezi Oktoba mwaka 2017.

"Nimeridhishwa na hatua zilizofikiwa na nina imani mkandarasi atamaliza mapema mradi huu",amesisitiza Waziri Kamwelwe. Aidha, ameupongeza uongozi wa mkoa huo na Wakala wa Barabara (TANROADS), kwa kusimamia mradi huo usiku na mchana na kuwataka kutoa taarifa muda wowote endapo kutakuwa na changamoto zinazoweza kukwamisha mradi huo.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Simiyu Mhandisi Albert Kent, akimuoesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, nyumba za Mhandisi Mshauri zilizojengwa na mkandarasi wa Kampuni ya CHICO katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, mkoani humo.

Akizungumzia kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Simiyu, Mhandisi Kamwelwe amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa hatua za awali zinaendelea katika kuhakikisha kiwanja hicho kinajengwa ili kufungua mkoa huo katika sekta za usafirishaji na uwekezaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, ameishukuru Serikali kwa kujenga kipande cha barabara hiyo baada ya ile ya Mwigumbi-Maswa kukamilika kwa kiwango cha lami kwa kuwa imekua ni kichocheo cha kuunganisha nchi yetu na nchi za maziwa makuu ambazo ni Uganda, Burundi, Rwanda, Kenya na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka wakikagua kokoto zitakazotumika katika ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.

Naye, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Simiyu Mhandisi Albert Kent amemueleza Waziri huyo kuwa mradi huo mpaka sasa umefikia asilimia 20 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Oktoba mwaka 2019.

Mhandisi Kent ameongeza kuwa kazi zilizofanyika mpaka sasa ni mkandarasi kuanza ujenzi wa madaraja makubwa mawili ya Banhaya na Simiyu na ameshamaliza kujenga madaraja madogo 9 kati ya 12 na makalvati 36 kati ya 58.

Mradi wa Maswa-Bariadi unagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 100 na unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 86. Kukamilika kwa mradi huo kutakamilisha ujenzi wa barabara ya Mwigumbi-Maswa- Bariadi-Lamadi yanye jumla ya urefu wa KM 171.8.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, akioneshwa na Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Simiyu Mhandisi Albert Kent, kazi zinazoendelea katika ujenzi wa daraja la mto Simyu, wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.
Muonekano wa kazi za ujenzi zikiendelea kwenye daraja la mto Simiyu katika barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7, Mkoani Simiyu.

Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Leo limeadhimisha miaka 54 tangu kuanzishwa kwake

$
0
0
Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Leo limeadhimisha miaka 54  tangu kuanzishwa kwake.

Maadhimisho hayo yamefanyika jijini Dar es salaam chini ya Mkuu wa Majeshi Generali Venance Mabeyo akiwa na mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, kwa kufanya usafi katika eneo la kambi ya Jeshi Lugola na  baadaye kufuatiwa na michezo iliyofanyika katika eneo la Uwanja wa Jeshi mwenge vinyago .

Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amelipongeza Jeshi hilo kwa kudumisha usafi na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuiga mfano wa Jeshihilo kutumia mazingira kwa usafi na kupanda miti katika maeneoyao.

Aidha Makonda ameelezeakusikitishwa kwake na kitendo cha mgambo wanaosimamia usafi katika jijini la Dar es salaam kwenda kinyume cha sheria katika kusimamia zoezi hilo kwakupiga wananchi na kusema kuwa hajawatuma kufanya hayo  na ametoa amri wakamatwe .

''Sheria zipo hakuna hata mmoja inayosema adhabu ya kukutwa na uchafu ni kupigwa bali sheria imeongelea faini, nimeagiza tangu jana walihusika na hilo tukio wakamatwe na hatua za sheria zichukuliwe dhidi yao" alisema. 

Kwa upande wake mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo amewataka wanajeshi kudhibiti usalama wa kambi  kwa kutoruhusu raia kukatisha  katika maeneo ya Jeshi  na kuahidi kujenga ukuta katika eneo la jeshi kambi ya Lugalo na  Mwenge na kuhiza usafi kuwa endelevu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda paulo makonda akiwa ameambatana na Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Tanzania jenerali, Venance wakiwasalimi wachezaji wa tumi moja ikiwa ni ya Jeshe na moja siyo ya jeshi katika maazimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
 Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Tanzania jenerali,Venance Mabeyo akizungumza viongozi mbalimbali pamoja na wanajeshi la JWTZ  katika maazimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwake.
 Mbwa wa jeshi akizibiti adui
 Mbwa wa jeshi akizibiti adu alie kua akirukuka ukuta


Michezo ikiendelea katika uwaja jeshi  Mwenge jijini Dar as Salaam.

K-VANT WAJA NA MUONEKANO MPYA NA LADHA YAKE HALISI YA SIKU ZOTE

$
0
0
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (wa pili kulia) akionyeshwa na Meneja mauzo na Masoko wa Kampuni ya Mega Beverages, Marco Maduhu, Chupa mpya ya K-Vant wakati wa uzinduzi wa muonekano mpya wa chupa ya kinywaji cha K-Vant uliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. (Kushoto) ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Francis Kimaro.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Mega Beverages, wazalishaji wa Kinywaji cha K-Vant ,Francis Kimaro(kushoto) na Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni hiyo ,Marco Maduhu, wakigongeana glasi ya K-VANT
Baadhi ya wadau mbalimbali wa kinywaji cha K-VANT wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Mega Beverages Francis Kimaro
Baadhi ya wadau mbalimbali wa kinywaji cha K-VANT wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
Naibu waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Mega Beverages wakati wa uzinduzi huo.

Na Mwandishi Wetu.
KAMPUNI ya Mega Beverage Company Limited,ya mkoani Arusha, inayotengeneza pombe kali chapa maarufu ya K Vant, imezindua chupa mpya za kinywaji cha K-Vant zenye mwonekano tofauti na chupa za awali.Mabadiliko hayo hayakubadilisha ladha halisi ya kinywaji hicho na wateja wake wataendelea kuifuahia ikiwa katika ladha yake halisi ya siku zote.

Lengo kubwa la kubadilisha chupa za pombe ya K-Vant, ni mkakati wa kampuni wa kupanua masoko yake ya ndani na nje ambapo imelenga kuwa katika mwonekano bora zaidi bila kuathiri ladha halisi ya kinywaji hicho ambayo inapendwa na watumiaji wengi wa pombe kali nchini na nje ya mipaka ya Tanzania

Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera,Bunge,Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mh.Antony Mavunde.

Mh.Mavunde,alipongeza hatua ya kampuni kubuni mkakati wa kuongea soko la bidhaa na kuongeza kuwa masoko yakiongezeka ndivyo mapato ya serikali yanaongezeka kupitia kulipa kodi sambamba na kuongeza wigo wa ajira kutokana na kuhitajika nguvu kazi zaidi.

“Serikali ya awamu ya tano inao mkakati wa kuifanya Tanzania nchi ya viwanda,tutazidi kuboresha mazingira zaidi kwa wawekezaji katika sekta hii ili lengo la kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta hii lifanikiwe haraka sambamba na kupunguza changamoto ya tatizo la ajira kwa vijana “,alisema.

Mkurugenzi wa Masoko wa Mega Beverage Company Limited, Marco Maduhu alisema, “Kauli mbiu yetu ya kinywaji cha K-Vant katika mwonekano mpya ni ’Ni Halali Yako’ kampuni imejipanga kuimarisha usambazaji wa bidhaa ya pombe ya K-Vant katika sehemu zote nchini ili watanzania waendelee kufurahia ubora wake kikiwa katika mwonekano wa chupa mpya na katika ladha ileile waliyoizoe kuipata siku zote”.

Alisema uzinduzi wa chupa mpya za K-Vant mbali na kufanyika katika mkoa wa Dar es Salaam pia utafanyika katika mikoa ya Arusha na Mwanza, pia usambazaji wa kinywaji hiki kwenye mwonekano mpya katika ladha yake halisi utaendelea kufanyika katika mikoa yote nchini kuanzia sasa.”Wateja wetu wowote popote mlipo tunawashukuru kwa kuendelea kutuunga mkono nasi tutaendelea kuboresha huduma zetu za usambazaji na kuhakikisha kinywaji bora cha K-Vant kinawafikia popote mlipo kikiwa katika chupa mpya”alisisitiza

Maduhu, alioongeza kusema kuwa, kampuni ya Mega Beverage,itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ambapo kupitia uwekezaji wake itahakikisha inaendelea kuchangia pato la taifa kupitia kulipia kodi mbalimbali, kunufaisha watanzania wengi kupata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja, pia imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za serikali kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye jamii.

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA MADIWANI PAMOJA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO MKOANI GEITA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Madiwani, Viongozi mbalimbali pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita. Wengine katika picha ni Mkuu wa Wilaya ya Chato Eng. Mtemi Msafiri Semeon(kushoto) na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chato Eliud Mwaiteleke(kulia).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mara baada ya kumaliza mkutano huo na Madiwani, Viongozi mbalimbali pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Christian Manunga wapili kutoka (kulia) mstari wa kwanza mbele, Mkuu wa Wilaya ya Chato Eng. Mtemi Msafiri Semeon watatu kutoka (kulia), Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani, wanne kutoka (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chato Eliud Mwaiteleke.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mara baada ya mkutano huo uliofanyika katika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita. Wengine katika picha mstari wa mbele ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Christian Manunga wakwanza kutoka (kulia) mstari wa kwanza mbele, Mkuu wa Wilaya ya Chato Eng. Mtemi Msafiri Semeon wapili kutoka (kulia), Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani wapili kutoka kushoto pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chato Eliud Mwaiteleke.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono Madiwani pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato wakatika akiondoka katika Ofisi za Halmashauri hiyo Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Chato kwa ajili ya mkutano na Madiwani, Viongozi mbalimbali pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita.
Baadhi ya Watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Chato wakifatilia kwa makini wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza masuala mbalimbali katika ukumbi wa Halmashauri hiyo Chato mkoani Geita. 
PICHA NA IKULU

UNLOCK CASTLE LITE YAZIDI KUWAPA RAHA WAKAZI WA JIJI LA DAR

$
0
0
Ile promosheni ya kampuni ya TBL kupitia bia yake ya Castle Lite kwa lengo la kuwapatia burudani inayojulikana kama Unlock Castle Lite inazidi kusambaza furaha kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambapo mwishoni mwa wiki ilikuwa kata mti panda mti ndani ya baa ya 5N iliyopo maeneo ya Sinza. 

 Lengo kubwa la promosheni hiyo ni Kutangaza chapa na kuwashukuru wateja kwa kuendelea kufurahia EXTRA COLD CASTLE LITE!. 

Tofauti na promosheni zilizozoeleka, promosheni hii imesheheni kila aina ya burudani ambapo inaweza kuwakutanisha ndugu, jamaa na marafiki pamoja na kupiga picha mbalimbali huku wakifurahia kinywaji bia ya Castle Lite wakiwemo wafanyakazi wa TBL ambao kwa sasa wameamua kutokana ofisini na kujumuika na wateja wao. 

 Unlock Castle Lite, ambayo inafanyika katika siku za Alhamisi na Ijumaa baada ya saa za kazi pia inawashirikisha wafanyakazi wa kampuni ya TBL ambao wanajumika pamoja na wateja na kuwapatia zawadi mbalimbali za promosheni. Tayari wakazi wa Kawe, Boko na Tegeta, Sinza,wamefikiwa na Unlock Castle Lite.
 Burudani za furaha ya Castle Lite zikiendelea
  Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakiwa na wateja waliojumuika pamoja katika burudani za furaha ya Castle Lite.
Furaha ya Castle Lite ilipamba kila mahali katika kiwanja cha maraha cha 5N kilichopo jijini Dar es Salaam.

UBA Grows Gross Earnings By 16%, Delivers 17% Return on Average Equity

$
0
0
GMD -CEO of UBA Plc -Kennedy Uzoka 

LAGOS, NIGERIA – August 29, 2018 – Africa’s leading financial institution, United Bank for Africa Plc has announced its audited 2018 half year financial results, showing strong growth across key performance metrics as well as a significant contribution from its African subsidiaries.

Despite declining yield environment in two core markets, Nigeria and Ghana, the pan Africa financial institution delivered double digit growth in gross earnings, as it recorded a 16 percent year-on-year rise in top-line to N258 billion, compared to N223 billion recorded in the corresponding period of 2017. This performance, according to analysts, underscores the capacity of the Group to deliver strong performance through economic cycles, even in a challenging business environment.
UBA building

According to the report filed to the Nigerian Stock Exchange on Wednesday, UBA, reported strong growth in operating income at N168.5 billion, compared to N161.8 billion in the first half of 2017, an increase of 4.1 percent. Notwithstanding the inflation-induced cost pressure in the period, UBA finished the first half of the year strongly, with a Profit Before Tax of N58.1 billion. The Profit After Tax also improved to N43.8 billion, a 3.4 percent growth compared to N42.3 billion achieved in the corresponding period of 2017. The first half of the year profit, translated to pre-tax and post-tax return on average equity of 23% and 17% respectively.

UBA’s foreign operations continue to grow in importance, contributing 40% of the Group’s profit, which according to analysts attests to the benefit of UBA’s pan-African strategy and reinforces the Bank’s objective of achieving 50 percent earnings contribution from offshore subsidiaries.

In the first six months of the year, the Bank’s Total Assets grew 4.9% to N4.27 trillion and Customer Deposits rose by 6.1 per cent to N2.90 trillion, compared to N2.73 trillion as at December 2017. This growth trajectory underlines UBA’s market share gain, as it increasingly wins customers through its re-engineered customer service and innovative digital offerings. The Group’s Shareholders’ Funds remained strong atN496.3 billion, even as implementation of IFRS 9 impacted the total equity of the bank and its peers.

In line with its culture of paying both interim and final cash dividend, the Board of Directors of UBA Plc declared an interim dividend of N0.20 per share for every ordinary share of N0.50 each held on the qualification date – Wednesday, September 05, 2018.

Commenting on the results, the Group Managing Director/CEO, United Bank for Africa Plc (UBA), Mr. Kennedy Uzoka said: "Our performance in the first half the year reflects the resilience of our business model and strategies. Despite declining yields in two core markets, Nigeria and Ghana, we delivered double digit growth in gross earnings. Our performance demonstrates the success of our digital banking initiatives and broader Customer-First strategies”

“We are integrating banking to our customers’ lifestyle, simplifying processes for routine transactions and driving financial inclusion by making banking services accessible and affordable. We are creating opportunities for wealth creation and economic progress, as we empower our customers through innovative platforms and solutions that support their personal and business growth. Our commitment to delivering excellent service is paying-off, as we increasingly win a bigger share of customers’ wallet across our chosen markets. We won the highly coveted “Africa’s Best Digital Bank” Award by Euromoney, demonstrating our pioneering initiatives are being recognised with Leo, our digital banker having been name checked by Mark Zuckerberg ” Uzoka said.
 
“Our enhanced asset-liability management strategies improved asset yield and grew interest income by 21% despite prevailing yield environment. Our re-engineered sales structure provided the impetus for renewed retail deposit growth. I am particularly pleased by the 24% year-to-date growth in retail savings and current account deposits, underpining the increasing penetration of our digital offerings and the Group’s overarching goal of democratizing banking across Africa. We improved net interest margin to 7.4%in line with our 2018 target, notwithstanding strong competition for wholesale deposits and the impact of rising global interest rates on our foreign currency funding,” he concluded

Also speaking on UBA’s financial performance and position, the Group CFO, Ugo Nwaghodoh said; “We finished the first half of the year in a stronger position and we are optimistic on the future of our business. Amidst economic recovery and uncertainties in Nigeria, our largest market, we grew net interest income and operating income by 9.6% and 4.1% respectively. We doubled revenue from trade services and grew e-banking income by 24%, a testament to our market share gain, which is driven by innovative offerings. Our foreign operations contributed 40% of Group’s profit, underlining the benefit of our Pan-African strategy.

“We sustained our asset quality, with cost of risk at 0.8%. Whilst the loan book declined by 6.5% due to prepayments from some customers in Nigeria and Ghana, we grew the overall balance sheet by 5% in the first half of the year. The Group’s capital adequacy ratio of 23%, Bank’s liquidity ratio of 48% and loan-to-deposit ratio of 57% all reinforce our capacity to grow, with ample headroom for risk asset creation,” Nwaghodoh said.

In recognition of UBA’s dominance in Africa’s digital banking space, UBA emerged the Best Institution in Digital Banking across Africa, courtesy of Euromoney. Earlier in the year, UBA launched Leo, an e-chat service using artificial intelligence to help customers execute transactions on Facebook, the first of its kind in Africa. The Bank is set to replicate the success of Leo on WhatsApp on September 1st, bringing convenience to its growing youthful customer base across Africa.
 
UBA is one of Africa’s leading banks with operations in 20 African countries. It also has presence in the global financial centres; London, New York and Paris. UBA provides banking services to more than 15 million customers globally, through diverse channels.

Vodacom yatoa gari la Tisa la M-Pesa jijini Tanga katika sherehe ya kufana

$
0
0
  Mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Vodacom Tanzania, Brigita Stephen (kushoto) akikabidhi kadi ya gari kwa mkazi wa Tanga Adolf Mlay, huku mkewe Amina Urssa akishuhudia, hafla hiyo ya kusherehekea miaka 10 ya M-Pesa ilifanyika katika viwanja vya Commercial jijini Tanga, ili kushinda Mteja anatakiwa kufanya miamala mingi Zaidi na kutumia M-Pesa ili kujikusanyia points na kuongeza wigo wa kushinda.
  Mshindi wa gari ya tisa ya M-Pesa kutoka Tanga Adolf Mlay (wa pili kushoto) na wake wakionesha kadi ya gari wakati wa hafla ya kukabidhiwa gari katika viwanja vya Commercial jijini Tanga
Mshindi wa gari ya tisa ya M-Pesa kutoka Tanga Adolf Mlayakiingia kwenye gari lake mara baada ya kukabidhiwa na kampuni ya simu ya Vodacomkatika viwanja vya Commercial jijini Tanga
Mshindi wa gari ya tisa ya M-Pesa kutoka Tanga Adolf Mlay (wa pili kushoto) akiwa na familia yake wakati wa hafla ya kukabidhiwa gari katika viwanja vya Commercial jijini Tanga

GULAMALI AENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NA ELIMU MANONGA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MBUNGE wa Manonga Mh. Seif Khamis Gulamali ameendelea na  ziara yake jimboni humo katika kukagua na kuangalia namna miradi ya  maendeleo  inavyoendelea kutekelezwa  kunufaisha wana Manonga.

Katika ziara ziara yake Gulamali alitembelea kituo cha afya Simbo sambamba na kukagua ujenzi wa madarasa matatu katika shule ya sekondari Mwisi ambako ameridhishwa namna miradi hiyo inavyotekelezwa na kuwataka wasimamizi kwenda na kasi na kufanya kazi zilizo bora zaidi.

Aidha Mbunge huyo alipata wasaa wa kukutana na kamati ya Zahanati ya  Nkinga, viongozi wa CCM na wadau wengine na kuona namna ukarabati wa miundombinu katika Zahanati ya Nkinga unavyoendelea. 

Gulamali  ameahidi kutoa kiasi cha shilingi 430,000 kwa ajili ya kuvuta maji ya Uhakika kwenye Zahanati ya Nkinga ili kupunguza adha kwa wananchi wa wauguzi katika mchakato mzima wa kutoa na kupokea huduma.

Pia ameahidi kuongeza vitanda viwili vya kujifungulia katika wodi ya wazazi na kueleza kuwa suala la afya hasa ya mama na mtoto lazima ipewe kipaupele.

Gulamali alihitimisha ziara yake kwa  kufanya kikao na wachezaji pamoja na viongozi wa timu  ya Manonga Queens ambayo iliibuka kidedea kwa kuichapa  Singida Worrier kwa goli mbili, na  amekabidhi mipira miwili na  kuahidi jezi na vifaa vya michezo ambavyo ameshaagiza kwa ajili ya timu hiyo itakayowakilisha mkoa mzima wa Tabora kwenye michuano ya soka daraja la kwanza Tanzania bara kwa timu za wanawake.
Mbunge wa Manonga Seif Gulamali (katikati) akizungumza na kamati ya Zahanati ya Nkinga mara baada ya kuwasili.

SERIKALI KUPAMBANA NA MIMEA VAMIZI NGORONGORO

$
0
0
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akiwa katika kikao na wadau na wamiliki wa hoteli zilizopo katika kingo za kreta katika bonde la Ngorongoro. Pamoja na mambo mengine Waziri Makamba amewata kuwekeza katika teknolojia ya kisasa ya kutibu maji taka ili yaweze kutumika tena na kuwataka kufahamu kwa matumizi ya maji kutoka ndani ya kreta hitimisho lake linakaribia, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akipata maelezo ya kitaalamu kutoka kwa Dkt. Linus Munishi mtafiti kutoka Taasisi ya Nelson Mandela. Taasisi hiyo imetenga eneo maalumu la majaribio ya kuua mimea vamizi bila kuathiri mazingira, utafiti unao onekana kufanikiwa.
Pichani ni mmea vamizi ambao unaathiri sana malisho ya wanyama katika bonde la Ngorongoro kreta. Serikali inachuka hatua za haraka kudhibiti mmea huo unaosambaa kwa kasi.

Serikali imeazimia kurudisha ikolojia ya hifadhi ya Ngorongoro katika mazingira yake ya asili na kusisitiza kuwa shughuli zote za kuharibu na kuchafua  ikolojia hiyo vitadhibitiwa kwa nguvu na uwezo wote.
Akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba amesema kuwa lengo la ziara yake ni kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwa Mamlaka hiyo mwezi Machi 2017.
Katika ziara yake mapema mwaka jana pamoja na mambo mengine Waziri Makamba aliagiza Mamlaka hiyo kuchukua hatua za haraka na kuwaelekeza wamiliki wa hoteli na loji hususan zilizoko katika kingo za kreta katika bonde la Ngorongoro kutafuta vyanzo mbadala vya maji na kuondokana na kutegemea chanzo cha chemichemi za Lerai.
Aidha, Waziri Makamba aliagiza kuchukuliwa kwa hatua za haraka ili kudhibiti mimea inayohatarisha uoto wa asili katika Mamlaka ya Ngorongoro kwa kuunda jopo la wataalamu kutoka Tume ya Sayansi na Tecknolojia,  Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira, Hifadhi za Taifa za Tanzania, Wizara ya Kilimo na Mifugo na Mamlaka ya Ngorongoro ili kufanya utafiti wa kina na wakisayansi wa kubaini mbinu mpya ya kupambana na mimea hiyo vamizi inayotawala mimea inayotumiwa na wanyama kama malisho.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa maagizo hayo Kaimu Mhifadhi wa Ngorongoro Dkt. Maurus Msuha amesema kuwa Mamlaka ya Ngorongoro iliwaandikia barua wamiliki wote wa hoteli na loji  na kufanya tafiti kupitia kwa wataalamu elekezi wawili tofauti ambao kwa pamoja walishauri kuandaliwa kwa mkakati wa usimamizi na matumizi ya maji ndani ya Mamlaka ya Ngorongoro utakaokuwa suluhisho la matatizo la maji bila kuathiri mifumo ya ikolojia katika Hifadhi.

Aidha, katika kukabiliana na changamoto ya mimea vamizi ndani ya hifadhi, Bw. Msuha amesema kuwa Mamlaka imeanda ramani ya kuainisha aina, kiasi na maeneo ilipo mimea vamizi ndani ya hifadhi ili kuweza kuweka mikakati na mbinu sahihi za kukabiliana nayo ikiwa ni pamoja na kuendelea na kazi ya kutumia njia rafiki ya kimazingira ya kungo’a, kufyeka na kuchoma njia iliyoonyesha mafanikio makubwa hususan katika kudhibiti mmea tishio (Darura stramonium) ndani ya kreta na maeneo mengine.

Bw. Msuha amefafanua kuwa Ofisi yake inashirikiana na wataalamu wa Taasisi ya Sayansi na Teknoljia ya Nelson Mandela ya Mkoani Arusha na wameanziasha utafiti utakaodumu kwa kipindi cha miaka miwili, utafiti wa kuua magugu katika hifadhi kwa kutumia mifumo ya ki-biolojia. Matokeo ya awali yanaonyesha mafanikio kwa asilimia 70 katika kupambana na mimea vamizi.

Mara baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri Makamba amesema kuwa suala la mimea vamizi ni janga la kitaifa ambalo kwa sasa linawekewa mikakati ya kitaifa ili kuweza kukabiliana nalo. “Mimea hii vamizi imetapakaa maeneo mengi nchi hivyo jitihada za pamoja zinahitajika, Sisi Ofisi ya Makamu wa Rais tumeitisha Mkutano Mkubwa Arusha tarehe 04/09/2018 utaojumuisha wataalamu na wadau kutoka taasisi mbalimbali ili kwa pamoja tuzungumze chanzo cha tatizo hili, ukubwa wake, madhara na hatua za kuchukua” Makamba alisisitiza.

Pia, Waziri Makamba ametoa muda wa miezi mitatu kwa Mamlaka ya Ngorongoro kuanza kutekeleza kwa vitendo Mpango wa usimamizi na matumizi ya maji ndani ya Mamlaka na kutoa rai kwa wamiliki wa Hoteli na loji hususan zilizoko katika kingo za kreta katika bonde la Ngorongoro kuanza kuwekeza katika teknolojia ya kisasa ya kutibu maji taka ili yaweze kutumika tena na kuwataka kufahamu kwa matumizi ya maji kutoka ndani ya kreta hitimisho lake linakaribia.

Waziri Makamba yuko Mkoani Arusha kupitia utekelezaji wa maagizo yake aliyoyatoa mwaka jana pamoja na kuzungumza na wadau waliowekeza katika hoteli na kambi za uwindaji.

BARABARA YA MASWA-BARIADI KUONGEZA UKUAJI WA UCHUMI KANDA YA ZIWA

$
0
0
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa  Simiyu, Anthony Mtaka wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.
 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Simiyu  Mhandisi Albert Kent, akimuoesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, nyumba za Mhandisi Mshauri zilizojengwa na mkandarasi wa Kampuni ya CHICO katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, mkoani humo.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, na  Mkuu wa Mkoa wa  Simiyu, Anthony Mtaka  wakikagua kokoto zitakazotumika katika ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, akioneshwa na Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Simiyu  Mhandisi Albert Kent, kazi zinazoendelea katika ujenzi wa daraja la mto Simyu, wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7 kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.
Muonekano wa kazi za ujenzi zikiendelea kwenye daraja la mto Simiyu katika barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa KM 49.7, Mkoani Simiyu
Imetolewa na Kitengo cha  Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na  Mawasiliano.

UJENZI unaondelea wa barabara ya Maswa-Bariadi yenye urefu wa Km 49.7 kwa kiwango cha lami unatarajiwa kufungua mkoa wa Simiyu na mikoa jirani ya Mara, Mwanza na Shinyanga  hivyo kutarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe mkoani Simiyu wakati akikagua barabara hiyo inayojengwa na mkandarasi wa kampuni ya CHICO na kuridhishwa na hatua zilizofikiwa katika ujenzi huo toka ulipoanza mwezi Oktoba mwaka 2017.

"Nimeridhishwa na hatua zilizofikiwa na nina imani mkandarasi atamaliza mapema mradi huu",amesisitiza Waziri Kamwelwe.

Aidha, ameupongeza uongozi wa mkoa huo na Wakala wa Barabara (TANROADS), kwa kusimamia mradi huo usiku na mchana na kuwataka kutoa taarifa muda wowote endapo kutakuwa na changamoto zinazoweza kukwamisha mradi huo.

Akizungumzia kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Simiyu, Mhandisi Kamwelwe amemueleza Mkuu wa Mkoa  kuwa hatua za awali zinaendelea katika kuhakikisha kiwanja hicho kinajengwa ili kufungua mkoa huo katika sekta za usafirishaji na uwekezaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, ameishukuru Serikali kwa kujenga kipande cha barabara hiyo baada ya ile ya Mwigumbi-Maswa kukamilika kwa kiwango cha lami kwa kuwa imekua ni kichocheo cha kuunganisha nchi yetu na nchi za maziwa makuu ambazo ni Uganda, Burundi, Rwanda, Kenya na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).

Naye, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Simiyu Mhandisi Albert Kent amemueleza Waziri huyo kuwa mradi huo mpaka sasa umefikia asilimia 20 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Oktoba mwaka 2019.

Mhandisi Kent ameongeza kuwa kazi zilizofanyika mpaka sasa ni mkandarasi kuanza ujenzi wa madaraja makubwa mawili ya Banhaya na Simiyu na ameshamaliza kujenga madaraja madogo 9 kati ya 12 na makalvati 36 kati ya 58.

Mradi wa Maswa-Bariadi unagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 100 na unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 86. Kukamilika kwa mradi huo kutakamilisha ujenzi wa barabara ya Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi yanye jumla ya urefu wa KM 171.8. 

WAITARA - MIMI SIO MSALITI NIMEFUATA MAENDELEO YA JPM

$
0
0


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Mgombe Ubunge wa jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwita Waitara  amesema yeye sio Msaliti bali amechagua CCM  ili aweze kumalizia alipoishia hususani swala la barabara , Umeme na Maji katika jimbo  hilo. Waitara amesema hayo leo katika Mkutano wake wa Kampuni uliofanyika katika Kata ya kitunda.
"Naomba niwaeleze ukweli kuwa nilikuwa natumia nguvu sana  katika kufanikisha mambo ya Maendeleo yenu huku  kutokana na sehemu niliyokuwa hivyo sasa nimehamia  huku na  kila kitu sasa ni mtelezo" alisema Waitara
Alisema kuwa alikuwa anapigwa marufuku kuongea na viongozi wa CCM lakini hao ndio wenye  mafungu ya Pesa na serikali jambo amblo mie nilikuwa kinyume nao kiasi cha kuanza kuniita Mimi Msaliti. Alisema kuwa hajaanza kuitwa msaliti leo  kwani walimuita msaliti tangu  alivyokuwa ya kuwasaidia   na kuwaletea maendeleo watu ambao  wamemwamini hili wapige hatua katika shughuli Zai za kila siku.
Alisema kuwa kwa  sasa unaweza kuzungumza na Waziri moja Kwa moja natayari Waziri wa Nishati  amemuakikishia kuwa Wakazi wote wa eneo hilo watapata  Umeme Kwa gharama za Rea.
Alisema kuwa katika swala la  barabara  na Maji tayari linqpatiwa ufumbuzi chini ya Serikali ya Chama Cha Mapunduzi.
Kwa upande wake Mjumbe wa Halmashauri Juu ya CCM  Livingstone Lusinde aliwataka watu wa ukonga wasifanye makosa kwani sasa wanachqgua Mbunge wa  jimbo atakayefanya kazi na serikali na sio uchaguzi Mkuu.
Alisema CCM peke yake ndio inatekeleza ilani Kwa kupewa dhamana ya kuongoza dola hivyo wakichahua mgombea kutoka vyama vingine watakuwa wamejitafutia matatizo wenyewe.
 Mbunge wa Jimbo la Segerea , Bonnaha Kaluwa akizungumza na wakazi wa kitunda kuwataka wadumishe ujirani kw akumchagua Waitara wa CCM
 Mbunge wa Ilala , Mussa Hazzan Zungu akizungumza na Wakazi wa Kitunda na kuwaomba wamchague waitara kwa kuwa ni Msikivu.

 Mgombea Ubunge Jimbo la Ukonga kwa Tiketi ya CCM Mwita Waitara akizungumza Wakazi wa Kata ya Kitunda katika moja ya Mikutano yake ya Kampeni
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akimwaga sera za CCM Namna gani Ilanai inatekelezwa kwa Wakazi wa Kitunda wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo Jimbo la Ukonga.
 Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia akiwambaia wakazi wa Kitunda Jimbo la Ukonga kuwa kuhama kwa Waitara sio shida kwnai akuanza yeye kutaka kufata Maendeleo yaliyopo CCM
 Mbunge wa Ilala , Mussa Hazzan Zungu Akiserebuka na wkaazi wa kitunda kabla ya kupanda jukwaani .
 Wabunge waliohudhuria Mkutano huo wakisakata rumba linalopigwa na Bendi ya TOT PLUS
  Mgombea Ubunge Jimbo la Ukonga kwa Tiketi ya CCM Mwita Waitara  Akicheza Ngoma ya Litungu kutoka Mkoani Mara
 Mgombea Ubunge Jimbo la Ukonga kwa Tiketi ya CCM Mwita Waitara  akiagana na wapiga kura waliojitokeza katika Mkutano huo.
Viewing all 39030 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>